Jenerali Ulimwengu: Sioni ajabu mapinduzi ya kijeshi Guinea. Yatafika haraka nchi za Kusini mwa Jangwa la Sahara

Jeshi lafaa likatae zuluma na sio kuvizia teuzi,jeshi la teuzi linachoweza labda kupindua meza na sio kupindua dhuluma.
Jeshi linapokuwa sehemu ya dhuluma hilo sio jeshi la wananchi
 
Akihojiwa na kipindi cha BBC kinachorushwa na television ya star TV tarehe 7 mwezi huu kuhusu mapinduzi ya Guinea, Jenerali Ulimwengu amesema yeye haoni ajabu Kwa yale yaliyotokea Guinea.

Na akatabiri pia kuwa hali hiyo ya kimapinduzi ya kijeshi itafika Kwa Kwa haraka sana ktk nchi zote zilizo Kusini mwa Jangwa la Sahara.

Alipoulizwa kwanini anawaza hivyo alisema kuwa kilichokuwa kinafanywa na Alpha Conde ya ukandamizaji, dhurumati, kutokujali demokrasia, na uvunjifu wa haki za binadamu ,vitendo hivyo viovu vinafanywa pia na baadhi ya Serikali zilizo Kusini mwa Jangwa la Sahara na nchi zetu za Afrika Mashariki.

Jenerali aliendelea kushangaa kuona AU na ECOWAS wakilaani mapinduzi hayo huku wakiwa walishindwa kukemea matendo mabaya ya Rais Conde.

Alisema hali hiyo ya kimapinduzi ya kijeshi hayana muda mrefu itafika ktk nchi zetu wakati wowote kuanzia sasa.

Jenerali Ulimwengu ambae kwasasa ni mtu mzima na mwenye busara ni mtu asiyependa unafiki na hupenda kusema ukweli na maneno yake mara nyingi hutimia kama anavyotabiri.
Hongera Generali Ulimwengu. Kwa uzoefu wake wa Siasa za nchi hizo, na ukizingania amekuwa ndani ya siasa hizo kwa miongo takribani 4 hivi, anajua kabisa nini kinaenda kutokea soon.

Watu wanasahau kuwa hao wanaofanya mapinduzi si ndugu wala wajomba au mashangazi wa watawala.

Ndugu zao ni hao wanaodhurumiwa haki zao, wanateswa na kufungwa kwa sababu za uongo, ni hao wanaobebeshwa mizigo ya Kodi na matozo ya kila aina...hao ndio ndugu zao, wajomba, shangazi, Baba wakubwa na wadogo, Mama wakubwa na wadogo nk.

Ukiona mwanasiasa kuntu kama Ulimwengu anasema hayo, ujue hata huko ndani ya wanaofanya mapinduzi kuna yanayoendelea yenye mlengo huo.

Siku atatokea shujaa mmoja na wenzake, watahakikisha hawafanyi makosa km yalebya miaka ya 80...

Ahsante Kaka Ulimwengu, kuwaeleza ukweli na kupeleka ujumbe kwa wahusika kuwa wanaweza kufanya kwasababu sababu zipo, nia ipo na uwezo wanao.
 
Akihojiwa na kipindi cha BBC kinachorushwa na television ya star TV tarehe 7 mwezi huu kuhusu mapinduzi ya Guinea, Jenerali Ulimwengu amesema yeye haoni ajabu Kwa yale yaliyotokea Guinea...
Kuna mambo mawili Jumuia iliyostaarabika haiwezi kuvumilia, inatakiwa kuwa na ZERO TOLERANCE: ugaidi na mapinduzi ya kijeshi. Ukiona mtu anatoa lisingizio, chochote kile, ukimchimba utakuta ana lake jambo ukilitafuta utalipata tu. It is conclusive evidence we have lost this person.
 
AU ni club ya viongozi wa nchi za kiafrika kukutana kupongezana jinsi wanavyo watesa wananchi wao. Mmoja wao akipinduliwa hukauka makookwa kupiga kelele aachiwe.
 
Akihojiwa na kipindi cha BBC kinachorushwa na television ya star TV tarehe 7 mwezi huu kuhusu mapinduzi ya Guinea, Jenerali Ulimwengu amesema yeye haoni ajabu Kwa yale yaliyotokea Guinea...
Baada ya mapinduzi,maisha ya wa Guinea yameshakuwa bora au wanashangilia upepo huku akina Bounay ndio wakibadili kula jikoni? 😂😄😄😄
 
Mapinduzi bado sio njia salama
Nchi nyingi Sana zimepindua lakini hakuna cha maana kimefangika ni kubadili walaji jikoni.

Mapinduzi yenye tija labda yaongozwe na wananchi tuu sio wanajeshi kuanzia mali,Mauritania,Egypt na nchi nyingi za Western Afrika lakini hakuna kipya
 
Akihojiwa na kipindi cha BBC kinachorushwa na television ya star TV tarehe 7 mwezi huu kuhusu mapinduzi ya Guinea, Jenerali Ulimwengu amesema yeye haoni ajabu Kwa yale yaliyotokea Guinea...
Itakuwa vzr,tuyatoe haya majitu serikalini,tuweke damu mpya,

Nikisikia haya majina,Ndugai,Samia,Maghufuri, Kikwete, Mkapa, Mwigulu, Jafo, Majaliwa nahisi kichefu chefu,
 
Akihojiwa na kipindi cha BBC kinachorushwa na television ya star TV tarehe 7 mwezi huu kuhusu mapinduzi ya Guinea, Jenerali Ulimwengu amesema yeye haoni ajabu Kwa yale yaliyotokea Guinea...
China na Russia hakuna mapinduzi kwani haki za binadamu ni kwenye karatasi tu.
 
Hongera Generali Ulimwengu. Kwa uzoefu wake wa Siasa za nchi hizo, na ukizingania amekuwa ndani ya siasa hizo kwa miongo takribani 4 hivi, anajua kabisa nini kinaenda kutokea soon...
Mm bwana Niko pamoja Na wewe kwakweli kwanguvu zetu tumeshindwa kuondoa udharimu, lbs wao wanaweza saidia.

Unajua hats Guinea wananchi walishindwa kabisa kumuondoa konde HADI jeshi lilipoingilia kati
 
Lkn kama serikali iliyopo madarakani inatumia wanajeshi kutesa watu, kupiga watu Na kuumiza watu, ajabu inakua wapi jeshi hilo hilo likiwageuka wao?
 
Alipoulizwa kwanini anawaza hivyo alisema kuwa kilichokuwa kinafanywa na Alpha Conde ya ukandamizaji, dhurumati, kutokujali demokrasia, na uvunjifu wa haki za binadamu ,vitendo hivyo viovu vinafanywa pia na baadhi ya Serikali zilizo Kusini mwa Jangwa la Sahara na nchi zetu za Afrika Mashariki.
Mwisho wa kunukuu.
 
Lkn kama serikali iliyopo madarakani inatumia wanajeshi kutesa watu, kupiga watu Na kuumiza watu, ajabu inakua wapi jeshi hilo hilo likiwageuka wao?
Kama wanapewa mgao hutokaa usikie hadi Yesu anarudi.
Ukiona Dikteta ana savaivu ujue anaelewa kula vizuri na hawa watu
 
Anachoongea Jenerali ni sahihi kwa mujibu wa historical calculations wala sio utabiri.

Hauhitaji akili kubwa kuona yajayo East Africa ni km ya Guinea ndio maana Museveni alilaani sana hayo mapinduzi akijua yeye ni next.

A.U. nayo inatakiwa kuondolewa kimapinduzi tu haina maana tena,inalinda maslahi ya madikteta.
A.U ni uchuro tu hapa Africa.
 
Back
Top Bottom