Jenerali Ulimwengu: Sioni ajabu mapinduzi ya kijeshi Guinea. Yatafika haraka nchi za Kusini mwa Jangwa la Sahara

Akihojiwa na kipindi cha BBC kinachorushwa na television ya star TV tarehe 7 mwezi huu kuhusu mapinduzi ya Guinea, Jenerali Ulimwengu amesema yeye haoni ajabu Kwa yale yaliyotokea Guinea.

Na akatabiri pia kuwa hali hiyo ya kimapinduzi ya kijeshi itafika Kwa Kwa haraka sana ktk nchi zote zilizo Kusini mwa Jangwa la Sahara.

Alipoulizwa kwanini anawaza hivyo alisema kuwa kilichokuwa kinafanywa na Alpha Conde ya ukandamizaji, dhurumati, kutokujali demokrasia, na uvunjifu wa haki za binadamu ,vitendo hivyo viovu vinafanywa pia na baadhi ya Serikali zilizo Kusini mwa Jangwa la Sahara na nchi zetu za Afrika Mashariki.

Jenerali aliendelea kushangaa kuona AU na ECOWAS wakilaani mapinduzi hayo huku wakiwa walishindwa kukemea matendo mabaya ya Rais Conde.

Alisema hali hiyo ya kimapinduzi ya kijeshi hayana muda mrefu itafika ktk nchi zetu wakati wowote kuanzia sasa.

Jenerali Ulimwengu ambae kwasasa ni mtu mzima na mwenye busara ni mtu asiyependa unafiki na hupenda kusema ukweli na maneno yake mara nyingi hutimia kama anavyotabiri.
Mama ajiandae Unguja padogo.
 
Msukosuko wake hautakua mdogo, unaweza kuichafua nchi isitawalike tena na kuvuruga mipango yote. Kila mmoja wetu ataathirika kwa namna moja ama nyingine.

Ikitokea, ipangwe na kuratibiwa vizuri utekelezaji wake, vinginevyo ni shida tupu.
Mkuu, ebu acha kukariri.....
Sio kila mapinduzi lazima damu imwagike, and sometimes lazima tupigane ili tuheshimiane..😎
 
Wale mashahidi wanne wa ambowe Ni wajeda
Tuanzie hapo
Hata kama unadhani mapinduzi ni kitu kidogo ee, fatilieni vizuri,akina Ulimwengu walitakiwa kuwapa upinzani planing nzuri kuhusu kueneza siasa katika hali kama hizi, Imani ya mtu ktk siasa,hakuna wakuibadilisha,kwa hiyo wapinzani waje vizuri na mipango mbadala.
Kutegemea mapinduzi ya kijeshi mpaka CCM wenyewe wafarakane kila mumoja abebe fito ya jengo, ndo tutegemee hayo. Lakn wakikaa wamoja tutahangaika sana kwenye kuwatoa.
Sababu upinzani wenyewe hatuko kitu kimoja,kila mumoja anajiona bora sana. Inaumiza sana, Ulimwengu, Lwaitama na wasomi wengine, wahubili kuleta Falisafa moja ya Upinzani,kwamaa wakubali mawazo mbadala,na changamoto zote wazimalize ndani ya vyama vyao badala ya kunza kufukuzana.
 
Kama ni utabiri wa kweli basi Waafrika tumeshindwa kujitawala. Tulipiga kelele wakoloni watuache tujitawale wenyewe lakini baada ya miaka zaidi ya 60 tunawaza mambo ya mapinduzi ya kijeshi. Junta au utawala wa kijeshi siyo jibu la matatizo yetu. Ni dalili ya kuwa demokrasia imetushinda na tumeshindwa kujitawala. Tungewaacha tuu wakoloni watawale mpaka tujifunze kwao jinsi ya kujitawala. Nchi kama South Africa ilichelewa kupata uhuru lakini iliwasaidia watu wake wajifunze jinsi ya kujitawala na kuendesha nchi. Sisi wengine tulikuwa na kiherere tukawafukuza mapema.

#FailedStates
Afrika bila wazungu hatusogei, South Sfrica bila Kabuluz wasingelikuwa hapo walipo.
 
Mkuu, ebu acha kukariri.....
Sio kila mapinduzi lazima damu imwagike, and sometimes lazima tupigane ili tuheshimiane..😎

Umesoma vizuri sehem ya mwisho ya andiko langu? Nimetoa angalizo umakini wa mipango na utekelezaji makini wa mapinduzi, kama itabidi ili kuepusha vurumai.

Kama ni lazima damu imwagike au tupigane ili tuheshimiane, kitu gani kinazuia hadi sasa?
 
Msukosuko wake hautakua mdogo, unaweza kuichafua nchi isitawalike tena na kuvuruga mipango yote. Kila mmoja wetu ataathirika kwa namna moja ama nyingine.

Ikitokea, ipangwe na kuratibiwa vizuri utekelezaji wake, vinginevyo ni shida tupu.
Hakuna mapinduzi yanayopangwa na kuratibiwa vizuri, ni maonevu kwa kwenda mbele wala tusijidanganye.

Na wanajeshi wakichukua ndiyo mbaya zaidi, hata wakimuweka raia kutawala, anakuwa controlled na remote tu na wanajeshi.
 
Shida vingozi wetu wanashindwa kusoma alama za nyakati
Huu utabiri wa Jenerali unanikumbusha ya Ghadaffi walimuonya juu ya Arab Revolution akasema kwa jeuri kuwa huku hayatafika...kilichomtokea imebaki kwenye kumbukumbu ya vitabu vya historia....waswahili tunasema...lisemwalo lipo, kama halipo laja
 
Huu utabiri wa Jenerali unanikumbusha ya Ghadaffi walimuonya juu ya Arab Revolution akasema kwa jeuri kuwa huku hayatafika...kilichomtokea imebaki kwenye kumbukumbu ya vitabu vya historia....waswahili tunasema...lisemwalo lipo, kama halipo laja
Gadafi na sadam waliamini Sana nguvu za kijeshi kuliko umoja wa kitaifa.
Hata uwe na jeshi imara intelligence imara ndani ya taifa lisilo na umoja ni bure.
Unaundiwa vikundi vya waasi vitakuondoa tu.
 
Akihojiwa na kipindi cha BBC kinachorushwa na television ya star TV tarehe 7 mwezi huu kuhusu mapinduzi ya Guinea, Jenerali Ulimwengu amesema yeye haoni ajabu Kwa yale yaliyotokea Guinea.

Na akatabiri pia kuwa hali hiyo ya kimapinduzi ya kijeshi itafika Kwa Kwa haraka sana ktk nchi zote zilizo Kusini mwa Jangwa la Sahara.

Alipoulizwa kwanini anawaza hivyo alisema kuwa kilichokuwa kinafanywa na Alpha Conde ya ukandamizaji, dhurumati, kutokujali demokrasia, na uvunjifu wa haki za binadamu ,vitendo hivyo viovu vinafanywa pia na baadhi ya Serikali zilizo Kusini mwa Jangwa la Sahara na nchi zetu za Afrika Mashariki.

Jenerali aliendelea kushangaa kuona AU na ECOWAS wakilaani mapinduzi hayo huku wakiwa walishindwa kukemea matendo mabaya ya Rais Conde.

Alisema hali hiyo ya kimapinduzi ya kijeshi hayana muda mrefu itafika ktk nchi zetu wakati wowote kuanzia sasa.

Jenerali Ulimwengu ambae kwasasa ni mtu mzima na mwenye busara ni mtu asiyependa unafiki na hupenda kusema ukweli na maneno yake mara nyingi hutimia kama anavyotabiri.

Kwa kweli wametuchelewesha sana
 
Mapinduzi ya Kijeshi sio suala la kupigia debe, labda hapo huyo Mhutu atakaposhika hatamu ndio kutakua na umuhimu lakini tunamuombea Mungu ili afe ndani ya miaka hii ya Samia.
 
Mzee aache kututisha, wao wamekula maisha kukiwa hamna vita kipindi chao sasa iweje leo atutabirie dhiki?

Huna neno lolote kwa hiyo mikono munene hapa nyuma?

IMG_20210911_000004_180.jpg


Hiiiiii bagosha!
 
Hilo ndo jeshi la wananchi sio SAwa na lile la kukimbia na masanduku ya kura.
 
Hilo ndo jeshi la wananchi sio SAwa na lile la kukimbia na masanduku ya kura.
 
Nchi kama Uganda, Rwanda na sasa Tanzania ni 'candidates' wazuri sana wa hayo aliyoyaelezea Ulimwengu. Nje ya hizo tatu katika maeneo ya huku Afrika Mashariki na Kusini sioni mfano mwingine kwa sasa. Labda Mnangagwa wa Zimbabwe na yeye awe king'ang'anizi!
 
Hilo ndo jeshi la wananchi sio SAwa na lile la kukimbia na masanduku ya kura.
 
Back
Top Bottom