Jela za wenzetu

MwanaHaki

R I P
Oct 17, 2006
2,401
705
Waheshimiwa,

Kwa mtaji huu, kama hizi jela zingekuja Bongo, watu wengi wangefanya uhalifu wapelekwe 'wakastarehe' huko, maana kama hii ndiyo jela yenyewe, mbona hata nyumbani kwangu hapanogi?


kwi kwi kwi!

Kazi inaanzia hapa!

















I dont think Tanzania will ever reach this standard... maybe 50 years from now!

LOL

./Mwana wa Haki
 
Inabidi tujue kuwa JELA ni mahali pa kurekebisha tabia sio mahali pa mateso.
Mtu yeyote anayefanya kosa hata kama ni makusudi kuna sababu ya kisaikologia iliyomfanya afanye hilo kosa.
 
Hakika jela hii laiti ingekuwa hapa ingejaa kupindukia na labda tungeiita PEPONI JAIL nadhani ubakaji wa watoto wadogo ungeshika kasi ili mahakimu kama Eddy Lyamuya akandamize vifungo vya maisha bila wasiwasisi. Lakini ili kuingia jela kama hii ingekuwa lazima utoe mlungula. Nandhani hata mafisadi wangekuwa wanakiri tu kwamba kweli waliiba pesa za EPA. Hata Chenge alivyo tua jana angefika na kusema "Ndugu waandishi wa habari ni kweli nilihusika sana katika sakata la radar na mikataba mibovu na nitajitahidi kurudisha pesa kama ikiwezekana"
 

Tungefurahi sasa sisi wazawa kupata mafisadi wajasiri namna hiyo wa kujitokeza kifua mbele kukiri ufisadi wao na jinsi walivyoangamizaji wa nchi kiuchumi ili waende huko LUPANGO ya luxury. Bajeti ijayo Waziri Macha aliombe bunge hela za kujenga LUPANGO namna hii pale Mbundya island. Kwa jinsi hii tutawapata mafisadi wengi wakujitoa kwenda huko na hakutakuwa na haja ya kuundwa TUME au kuwepo kwa TAKUKURU!!!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…