JEJE: Video ya wimbo Mkali toka Diamond

JEJE: Video ya wimbo Mkali toka Diamond

Kama wimbo huwezi kuuangalia sebuleni na watoto ujue ni uchafu tu.
Kama wimbo hauna dira ya kusikilizika miaka kadhaa ijayo ujue hauna hadhi ya kupigiwa debe.
Wapi mzee Kinkikiii...... vijana wameishiwa!
Ukiona huwezi kuungalia jua wewe sio mlengwa.!
 
Hata atoe wimbo mbaya kuna punda wake wataipenda. Kuna wengine hata watow wimbo mzuri kiasi gani bado hazitapendwa

Sent using Jamii Forums mobile app
Diamond ni kama Bakhresa...alishawekeza kwenye kuweka msingi wa nguvu kwa muda mrefu...sasa watu wote hamna jinsi inabidi kufuata mapigo yake kama nyumbu...hata kama ukipinga vipi lazima utatumia bidhaa za Bakhresa kama si unga, mchele, juisi, pipi, soda,aishikirimu nk nk...kwa mfano ashikirimu za ukwaju ni za kawaida sana ,...sasa ona maajabu yake sokoni !!!ndivyo ilivyo kwa Diamond ...ni lazima utazikililiza nyimbo zake popote pale ziwe za kawaida au la!...ameshavuka ule mstari wa kubembeleza watu wampende...utampenda kwa lazima ...kumbaf
 
sijawahi kuona diamond platnamz ametoka wimbo halafu watu msiuponde.. huwa mnaponda hivi hivi afu mwisho wa siku akitoa next song mnaanza kusema the last one was the best .. swali ni kwanini wabongo mnapenda sana kusifia wakati uliopita badala ya uliopo.?

leo hii utakuta mtu anakuambia nyimbo za diamond zilikuwa ni inama, the one, nk lakini cha ajabu kipindi zimetoka hakuzisifia . tuache unafiki ndugu zangu. hii ndio sababu tunasifiaga marehemu kuliko mtu akiwa hai

Sent using Jamii Forums mobile app
Ni kawaida, hata kwenye siasa, leo JPM akihamia ACT, atapewa sifa zote za kugombea urais.
Zitto atakana yote aliyekua anayaongea.
 
Hovyo !!! hovyo kabisa sio lazima atoe wimbo kama hajajiandaa. Angewkuwa na washauri wazuri kwa level anayokubalika sasa hasa afrika magharibi angetafuta colabo na wasaniii wa nchi hizo lakini sii nigeria na aimbe kwa lugha ya kifaransa kwa hata kurudia nyimbo zake zilizobamba ili kuendelea kujenga imani zaidi kwenye nchi hizo na sio kutuletea kapambio kasiku na mizani wala vina , kasikokuwa na ujumbe wowote tena kafuuuupi!!!! hovyo kabisa
 
Hata atoe wimbo mbaya kuna punda wake wataipenda. Kuna wengine hata watow wimbo mzuri kiasi gani bado hazitapendwa

Sent using Jamii Forums mobile app
kupenda au kutokipenda kitu ni hisia za mtu na si kosa, hivyo sio sawa kuwaita wenzio mapunda just bcz hukubaliana na wanachokipenda, mana hata wewe kuna unavyovipenda lakini wengine hawavipendi tuliumbwa kuwa tofauti, kwahiyo kama kitu hakijakufurahisha isemee nafsi yako basi inatosha lakini usisemee wala usitukane nafsi za wengine
 
Jeje ni "Copy And Paste" ya wimbo wa Oyoyo Skales Ft Harmonize... Melody, Mpaka Intro
 
Back
Top Bottom