Bin Maryam
JF-Expert Member
- Oct 22, 2007
- 685
- 13
Dua,
Mjomba hapa nakubaliana sana na Bin Maryam kwa kutazama vielelezo vilivyotangulia..
Siku zote tunasema Amani yetu imejengwa na Ujamaa lakini mbona hata Zambia na Malawi ambao walikuwa Mabepari nao wana amani kama yetu na Ukabila sii swala kabisa linaloongelewa ndani ya nchi zao... Je, ni kipi ambacho tunafanana nao hawa watu... Utakuta ni kuwa sote tulipata Uhuru wetu kibwelele yaani jitihada za Uhuru wetu hazikuanzishwa na wananchi wenyewe kwa kuingia mwituni isipokuwa sheria za UN ndiuzo zilitupa Uhuru huo laa sivyo labda who knows tungekuwa tukitawaliwa hadi leo. Na trust me kuna tofauti kubwa sana kati yetu bara na Zanzibar na ndio maana tunawaona wao kuwa wana matatizo hali sisi Bara ndio wenye matatizo na hiyo slogan ya amani na utulivu yetu.
Sasa huo utulivu wetu wa amani mahala ambapo haki zetu zinachukuliwa na wachache ati tukiita watu wa amani ni Ujanja kweli ama ndio Ujinga wenyewe?...Mbona Tanzania, Zambia na Malawi ndizo nchi ambazo tunaliwa zaidi na viongozi kila siku kazi yao ni kubadilisha mashati tu.... (Ofisi za kazi). Na sii kwamba hatujui kuwa hawa ni Mafisadi lakini ndio kwanza tunawabeba ktk KURA na kuwaita waheshimiwa.
Sasa ukirudi ktk kuuliza mchango gani Bin Maryam kautoa, mzee wangu hapo utakuwa umechukia.... maanake hapa ni kijiweni tu sote ni Wadanganyika ambao miaka yote tumeukumbatia Ujinga huo wa amani na utulivu...Lakini kama walivyosema wahenga kuwa siku zote idea huanza na mtu mmoja kisha ikapata support na mwishowe ikatumika kuleta mabadiliko na ndio changes tunazopigania hapa. Ni kutokana na michango yenu imenisaidia sana mimi hapa kutokubali kuendelea kuwa chini ya viongozi wabovu.. leo nipo mimi kesho mtampa mtu mwingine na wimbi la msukumo wa fikra hizi utazidi kupanua wigo kati ya Wadanganyika.
Hata hiyo hoja yako ya kuuliza mchango wake nadhani pia ni msukumo wa fikra ambayo kesho itampa nguvu Bin Maryam afikirie kuchangia kivitendo fikra hizi za Mapinduzi ya fikra...
I guess hapa ndipo tulipo sasa hivi ktk Mapinduzi ya fikra na labda jambo kubwa zaidi ni jinsi ya kuzieneza hizi fikra ziwafikie Wadanganyika wengi zaidi.
Dua:
Sidhani Mwafrika wa Kike alipoanzisha thread alikuwa na maana ya kuenzi mchango wa mwalimu kuhusu amani. Hivyo kueleza mchango wangu kulinganisha na Nyerere nitakuwa natoka nje ya mada, lakini kwa sababu umeuliza ngoja tuelimishane kama ifuatavyo.
Kila mtu ana nafasi yake katika jamii na wote hatuwezi kuwa marais kwa kipindi kimoja. Kwa mtaji huu raia yoyote wa Tanzania ambaye ametimiza wajibu wake wa kisheria kwa nchi kama vile kufanya kazi na kulipa kodi, kutofanya uhalifu AMETOA MCHANGO MKUBWA SANA KWA TAIFA KULIKO KIONGOZI WA NGAZI YA JUU AKIWEMO MWALIMU. Ni mchango wa watanzania uliofanya viongozi walipwe mishahara, wapate vyombo vya usafiri, wapate nafasi za kukaa ofisi na kufikiri wakati wengine tunafanya kazi za kutoa jasho.
Mchango wa taifa ni sawa kwenda peponi kwa muumini wa dini. Papa na muumini asiye cheo chochote katika kanisa Katoliki wana nafasi sawa za kwenda peponi, ingawaje papa anachaguliwa na kuzikwa kwa vishindo.
Uhuru wa Tanzania umepatikana kwa amani. Hata Zanzibar kulikotokea mapinduzi uhuru ulipatikana kwa amani.
Zambia, Malawi, Tanzania zilikuwa za nchi za amani ata kipindi wakoloni wapo. Kaunda, Kamuzu na Kambarage walichukua nchi zenye amani cha kujiuliza ni kuwa pamoja na amani na utawala wa muda mrefu hawana vielezo kwanini walishindwa. Kusema kuwa walileta amani ni kutafuta credit kwa kile kilichokuwepo.
Tufafanulie ni kitu gani kilichokuwepo? Au wewe binafsi ni mchango gani umetoa kulinganisha na wa Mwalimu Nyerere (RIP)kuhusiana na amani iliyopo Tanzania.
Sasa huo ndio ufafanuzi wako au unaamua kupindisha kile ambacho umekiandika?
Nakuwekea hapa chini jinsi ulivyoandika:
Swali langu
Kwenye amani unayoiongelea labda kama unataka kusema Kiswahili kuwa lugha ya taifa ni ujamaa? Kwa sababu hiyo ndio nyenzo kubwa ambayo ilikuwa ya kwanza kuweza kuwaunganisha wabongo kabla ya jambo lingine lolote na hapo credit ni kwa Julius au tukupe wewe? Ndio nikauliza where was your contribution if any? Na hili sio jambo dogo kama unavyotaka members hapa wakubaliane na wewe, lingekuwa jambo dogo Uganda, Kenya na baadhi ya nchi zingine wasingeanza kujifunza Kiswahili kwa nguvu zote.
Tukumbuke credit hutolewa kwa wale ambao ni exceptional labda uniambie u-exceptional wako wewe katika kulipa kodi etc. ...................which I believe that's normal to the majority of the citizens.
Mshikamano ambao Julius aliufanya huwezi hata kulinganisha na nchi yoyote Afrika sasa kama hapo hutaki kutoa credit wakati wengi leo hii duniani wanatoa credit napata mashaka na kusudio lako.
Mshikamano ambao Julius aliufanya huwezi hata kulinganisha na nchi yoyote Afrika sasa kama hapo hutaki kutoa credit wakati wengi leo hii duniani wanatoa credit napata mashaka na kusudio lako.QUOTE]
Kaka Dua nadhani hapa hakuna anayetaka kumdiscredit mwalimu, Hapana kabisa wangu, bali watu wanaangalia reality check! Unajua mkuu ufisadi wa kipindi cha Nyerere hata ungekuwepo tulikuwa hatujui (wengi wetu), jamii ilikuwa bado kwenye usingizi, radio ilikuwa ni moja ya RTD, Kipindi hicho akina Slaa walikuwa hawana forum ya kuongelea (unakumbuka akina Mwakitwange na Jumbe waliopinga serikali na chama waliishia wapi?), Jambo Forum haikuwepo nk. Kwa hiyo kusema kwamba wakati wa Mwalimu kulikuwa hakuna UFISADI napata shaka. Kama usingekuwepo naamini kimaendeleo tungekuwa mbali. Iweje watu walivurunda mashirika na kuhamishiwa kwingine? bila kuchukuliwa hatua? ni kwamba tulikuwa hatuna wasomi? I dont buy this idea..its too apologitic.. I agree mkuu wangu kwamba Mwalimu alijitahidi sana kuijenga Tanzania lakini as any other mwananchi napata walakini na umakini wake wa sera zake za kiuchumi.
Again, kwamba watu wa nje wanamsifia mwalimu kwa hiyo na sisi tuna wajibu wa kumsifia naamini mkuu hapo umeteleza, hata WORLD BANK na BUSH si wanampa sifa kila siku Kikwete kwamba uchumi unakuwa...and on and on...je ni kweli watanzania tuna la kujivunia na utawala wa Kikwete? with BALALIS DOING THEIR THINGS UNDER HIS WATCH?? which uchumi unaokua?
Mwalimu did what any responsible citizen should do for his country. kwa hiyo na mlipa kodi, ambaye haiibii serikali, mtu mwadilifu katika utumishi wa umma, nk ni much, much much better kuliko akina Karamagi na Mramba wanao kula kodi zetu bila kuwa accountable. Mwalimu was a great leader in his own way, but its akward that with half a century of independence we are still in the deep bondage of poverty. He cant shoulder responsibility alone, but he is equally responsible, he was our captain for almost a half of that half of the century of independence!
Ni akili ndogo tuu ya waafrika ndio maana tumefeli kila kitu na umaskini unatuandama tangu enzi na enzi,hatuwezi kujisaidia tumekalia kusafiri kwenda kuomba misaada ndio policy ya maendeleo then tunategemea tutaenda mbele,kama sio akili ndogo ni nini? wananchi wanachagua CCM kwa kishindo huku wakijua hao ndio mwanzo wa rushwa kama sio akili ndogo ni nini? rushwa ya billion 133 kwa nchi maskini kama yetu na wanaohusika bado wako kazini kama sio akili ndogo ni nini? mimi naamini hatuna akili ndio maana ni maskini,tungekuwa timamu huko vichwani tusingekula rushwa wala kuchagua wala rushwa wanaotutengenezea mifumo mibovu kwenye jamii yetu...naamini siku tukipata viongozi wenye akili tutaendelea sana.
..Inaelekea Watanzania tumeridhika sana na hali ya umasikini uliotuzunguka.
..Vilevile Watanzania tumeshindwa kuunganisha umasikini wetu na viongozi tunaowachagua.
..Watawala wetu wamevuruga nchi na uchumi lakini hatuishi kuwaenzi na kuwatukuza.
Unajua mkuu ufisadi wa kipindi cha Nyerere hata ungekuwepo tulikuwa hatujui (wengi wetu), jamii ilikuwa bado kwenye usingizi, radio ilikuwa ni moja ya RTD, Kipindi hicho akina Slaa walikuwa hawana forum ya kuongelea (unakumbuka akina Mwakitwange na Jumbe waliopinga serikali na chama waliishia wapi?), Jambo Forum haikuwepo nk. Kwa hiyo kusema kwamba wakati wa Mwalimu kulikuwa hakuna UFISADI napata shaka. Kama usingekuwepo naamini kimaendeleo tungekuwa mbali. Iweje watu walivurunda mashirika na kuhamishiwa kwingine? bila kuchukuliwa hatua? ni kwamba tulikuwa hatuna wasomi?
Ni akili ndogo tuu ya waafrika ndio maana tumefeli kila kitu na umaskini unatuandama tangu enzi na enzi,hatuwezi kujisaidia tumekalia kusafiri kwenda kuomba misaada ndio policy ya maendeleo then tunategemea tutaenda mbele,kama sio akili ndogo ni nini? wananchi wanachagua CCM kwa kishindo huku wakijua hao ndio mwanzo wa rushwa kama sio akili ndogo ni nini? rushwa ya billion 133 kwa nchi maskini kama yetu na wanaohusika bado wako kazini kama sio akili ndogo ni nini? mimi naamini hatuna akili ndio maana ni maskini,tungekuwa timamu huko vichwani tusingekula rushwa wala kuchagua wala rushwa wanaotutengenezea mifumo mibovu kwenye jamii yetu...naamini siku tukipata viongozi wenye akili tutaendelea sana.
Mzalendohalisi:Mzalendohalisi;130189]1. Tunahitaji good and strict leadership patriotic na kuwa 'dictator' kwa miaka say 15 to 20 years! Hii haihusiani na ubepari wala ujamaa! udiktator kuweka extreme strictness ktk matumizi na makusanyo ya raslimali, na kuchukua hatua kali kwa mafisadi!
2. Udiktatoship wa kizalendo pia utarejesha uzalendo wa Taifa ambao naona kama unaanza kupotea! Pia italeta displine ya kazi na kupunguza siasa- na kuzitofautisha na kazi!
3. Then we need strong institutions kusimamia haki i.e mahakama, Bunge, free media n.k and to fairly re-distribute wealth. Mf. Mtu akiiba au haruhusiwi kugombea ubunge au to take any public office!
4. Bado hadi sasa nina wasi2 kama kweli Afrika (Tz) we were ready for Multi-party. Have many parties done good or harm? Hii stage inafaa kama 1-3 have been fullfied!
5. Pia we need to look on ways to cut off foregn AID- ila kwa humanitarian reasons! Misaada ya nje imetulemaza na inaturudisha nyuma kimaendeleo!
Angalia Kenya- wale wote waliokuwa implicated ktk Angloleasing and Golderberg multi-bilion deals -kuwaibia watu maskini wamepata promotion wote ni wabunge na mawaziri! Angalia Tz mawaziri, Makatibu wakuu wana nyumba (na nje ya nchi) na mali zisizilingana na mapato yao- na wanapeta na wanapewa nafasi zaidi! Na wananchi wa kawaida wanaona!
Pia naona kama mfumo wa sheria tuliorithi UK not ideal kwetu Afrika- we need a much stricter laws, na vyombo vya dola!
Ni kama udiktator.. flani ila watu wakishazoea na kuheshimu hizi sheria ndo Afrika we shall take off!
Otherwise I see the near future of our continent glomy![/
Bob Mkandara,
Ukweli utajidhihirisha pale wale wenye nia ya kweli watakapoanza kujitolea bila masharti. Katika miaka yangu 10 ya mitandao hii ya Watanzania, nimejifunza mengi na kuona kwa dhati ni jinsi gani tlivyofanana na CCM na Serikali yetu.!
The amount of money extorted and stolen each year from developing countries is over 10 times the approximately $100bn in foreign assistance being provided by all governments and civil organizations in the world.