je, Watanzania hawa wanayo haki ya kulia?

je, Watanzania hawa wanayo haki ya kulia?

omujubi

JF-Expert Member
Joined
Dec 6, 2011
Posts
4,444
Reaction score
2,702
Habari wanajf,

Nilifuatilia mlolongo wa matukio ya mji wa Dar es Salaam kupitia mvua kubwa zilizonyesha tarehe 21 December 2011 ambapo kiukweli maafa makubwa ya watu wengi kupoteza maisha yalitokea.
Serikali ilichukua hatua na kuwapimia viwanja wenye nyumba na wapangaji vya bure kule Mabwepande na kuweka huduma za msingi japo hazikuwa nzuri kihivyo.

Kilichotokea baada ya hapo ni baadhi yao kuvikataa ili waendelee kuishi 'karibu na mjini'.

Sasa hiki kilio wanamlilia Mungu, Serikali, ccm, cdm ....

mafuriko.jpg mafuriko1.jpg nawasilisha.
 
Umasikini ndio unawapeleka mabondeni. Serikali iwape nyumba kama msaada.
 
sasa serikali inapotoa viwanja
tu hela za kujenga watoe wapi?
pole yao mweeeeeeh!
 
Habari wanajf,

Nilifuatilia mlolongo wa matukio ya mji wa Dar es Salaam kupitia mvua kubwa zilizonyesha tarehe 21 December 2011 ambapo kiukweli maafa makubwa ya watu wengi kupoteza maisha yalitokea.
Serikali ilichukua hatua na kuwapimia viwanja wenye nyumba na wapangaji vya bure kule Mabwepande na kuweka huduma za msingi japo hazikuwa nzuri kihivyo.

Kilichotokea baada ya hapo ni baadhi yao kuvikataa ili waendelee kuishi 'karibu na mjini'.

Sasa hiki kilio wanamlilia Mungu, Serikali, ccm, cdm ....

View attachment 88114View attachment 88115nawasilisha.


Hapana, hawa hawana haki ya kulia kwani hapa ni Jangwani (Dar Es Salaam), na hawa watu walishalipwa pesa zao za kuhama hii sehemu siku nyingi sana. Wengi wao walikula tu pesa kufkiri ni za msaada wa kuishi pale Jangwani na wengine wenye akili na kutihi amri walihama. Hawa kimekula kwao.
 
Walie nini mkuu? Watanzania ni wabishi kufuata plan za mipango miji,ukijenga bondeni lazima ujue kuogelea
 
ndio wa tz hao, hapo halaumiwi Mungu, alishakupa akili. Mi nailaumu serikali kwa kutokuwa wakali na hawa watu wanarudi mara kwa mara bila kutii maagizo. Eti serikali itoe viwanja na hela za ujenzi!!!! hakuna kitu kama hicho ukizingatia kwamba viwanja havikupimwa vilijengwa kiholela, labda serikali ilaumiwe tena na tena kwa kutochukuwa hatua tangu hapo awali.
 
Umasikini ndio unawapeleka mabondeni. Serikali iwape nyumba kama msaada.
mi natamani wangesombwa na maji kabisa!!umasikini gani hapo ni kibri ndo kinawasumbua!!serikali imewapa viwanja mabwepande tena vilivyo pimwa!!na juzi mheshimiwa rais alionyesha dhamila yake ya kuwapatia mifuko 100 ya cement ili kuwasaidia kujenga,wao wameviacha viwanja hivyo wanajirudisha town!!!SIWAHURUMII
 
ukiona mtu mzima analia mbele za watu ujue kuna jambo (msondo ngoma band)

Hasa kama ameshika kitumbua, huwa tunaimba, "Kitumbua changu upande mmoja kimeungua kama ni uongo kamuulize Kisura", mwanangu hilo ni nukuu la michezo ya 1947.
 
mi natamani wangesombwa na maji kabisa!!umasikini gani hapo ni kibri ndo kinawasumbua!!serikali imewapa viwanja mabwepande tena vilivyo pimwa!!na juzi mheshimiwa rais alionyesha dhamila yake ya kuwapatia mifuko 100 ya cement ili kuwasaidia kujenga,wao wameviacha viwanja hivyo wanajirudisha town!!!SIWAHURUMII
jana mmoja wa waathirika alisema kuna kujuana wengine walikosa! I am not sure to what extent is that statement true anyway!
 
Back
Top Bottom