Je, Wasanii wa nchi hii wanatumiwa na watawala wetu kama askari wa kukodiwa?

Ulikuwapo kwenye ufunguzi wa kampeini za UKAWA wewe? Huyo hapo ni nani



Kikubwa hapa tugawane mbao!!

Kisa cha Roma mpaka leo hakijulikani hadharani ila hiyo pia haizuii kupambana!!

Vyama pinzani Tz uwanja uko huru tangazeni dau kwa wasanii mnaowahitaji! Wakikataa basi jibu mtakua nalo na wakikubali twenzetu!!

Jibu la mjinga kwenye ufahamu ni vitendo + ukimya!! Mengine chokochoko!
 
Si kwamba chadema au act ndiyo vyama bora sana, hapana, ilaccm inabidi waondoke wasababu wamelewa mno madaraka na sasa wamekuwa waonevu sana na wakatili.
Kila raia sasa anatishwa tishwa ovyoovyo. Kweli uhuru hakuna. Ccmwaondoke.
 
Si kwamba chadema au act ndiyo vyama bora sana, hapana, ilaccm inabidi waondoke wasababu wamelewa mno madaraka na sasa wamekuwa waonevu sana na wakatili.
Kila raia sasa anatishwa tishwa ovyoovyo. Kweli uhuru hakuna. Ccmwaondoke.
Ni kweli ccm wanatakiwa waondoke ila pia ni muhimu zaidi kumjua huyo atakayeingia baada ya ccm,ishu ni kuondoa tatizo na sio tu kumtoa ccm madarakani.
 
Tumeshuhudia wasanii wote wenye majina makubwa wasiopungua 200, wakishiriki kwa pamoja kwenye tamasha lililoandaliwa na CCM, katika uwanja wa Uhuru hapo jana, kwa kile kiliichoitwa tamasha kubwa kabisa la kimuziki, kwa wasanii hao wote wanaodaiwa kuwa ni mashabiki wakubwa na wanaiunga mkono CCM katika uchaguzi mkuu ujao, unaotarajiwa kufanyika mwezi wa October mwaka huu.

Wengi wetu tutakuwa tunajua kuhusu hao wanaoitwa askari wa kukodiwa, au kwa jina lingine wanaitwa mamluki, ambao kwa lugha ya kiingereza wanaitwa "mercenaries" kwa tabia zao za kupenda pesa na wako tayari kwa atakayewapa pesa watakayoridhika nayo kupigana kwa yeyote, hata kama watafahamu kuwa hao wanaotakiwa kupigana nao ni ndugu zao wa kuzaliwa, ili mradi tu umewapa pesa watakayokubaliana nayo kwa ajili ya kazi hiyo!

Hiyo ndiye tabia ya "mercenaries" kuwa wapo tayari kupigana na adui yeyote, ilimradi yule aliyewakodi, atakuwa ameweka mezani "kibunda" ambacho wataridhika nacho.

Hiyo tabia ya "mercenaries" siwezi kuitofautisha na wasanii wetu waliojitokeza kwa wingi pale uwanja wa Uhuru ili kuwaunga mkono CCM, katika kuwakandamiza wazalendo ambao maisha yao yameathirika vibaya kutokana na utawala huu wa CCM wa miaka yote 60 baada ya Uhuru.

Tunajua kabisa tabia ya wasanii wa nchi yetu kuwa huwa hawaendi kwenye "show" yoyote kabla ya kuwekewa donge nono, ambalo wenyewe watakuwa wamekubaliana nalo, ndipo hapo wanapotokea kwenye onyesho hilo.

Hawa jamaa tunawajua kwa tabia yao kuwa hawana mapenzi na mtu, bali kinachopendwa ni pesa tu, ndiyo itakayoamua kuwa waende kwenye onyesho hilo au laa.

Kutokana na tabia hiyo ya wasanii wetu, kwa hiyo tunakuwa na uhakika kuwa CCM "imekamuliwa" pesa za kutisha ili kuwaleta kwa pamoja wasanii wakubwa wote tuliowaona jana.

Kwa upande wa ile "nyomi" iliyojazana pale katika uwanja wa Uhuru, hao CCM wasichukulie kuwa ule umati wote uliojazana pale kiwanjani, kuwa ni wafuasi wao na wenye ukereketwa wa kindakindaki wa chama chao cha CCM, bali ule umati ulijazana pale uwanjani kuja kuwashangaa kina Diamond na Ali Kiba katika show hiyo ya bure na wala sivyo watakavyokuwa wanachukulia viongozi waandamizi wa CCM kuwa ule umati wote ni mashabiki wao wa CCM!
Uchaguzi wa Mwaka huu CCM mwisho itawakusanya Mpaka Wapinzani iwaombe Kura
 
Back
Top Bottom