JamiiTalks
JF Advocacy Team
- Aug 7, 2018
- 625
- 938
Kwa mujibu wa kifungu cha 53 cha Sheria ya Taifa ya Uchaguzi, Sura ya 343, ikiwa mpiga kura ambaye tayari amekwisha kupiga kura hajaridhishwa na mwenendo wa upigaji kura katika kituo cha kupigia kura, anaweza kutoa malalamiko yake kwa msimamizi wa uchaguzi kwa kujaza Fomu namba 15.
Baada ya kupokea malalamiko yaliyojazwa katika Fomu namba 15, msimamizi wa uchaguzi anatakiwa kuyatafutia ufumbuzi, kisha kuonesha, katika fomu hiyo hiyo namba 15 ni kwa jinsi gani ameyatafutia ufumbuzi malalamiko ya mpiga kura.