Je, wajua kuwa kuna uwezekano Tanzania sio nchi halali Kisheria (De Jure) Bali ni De Factor?!

Jina Tanzania ni jina alilokwenda nalo Nyerere wakati wa kuunganisha Nchi mbili ,hivyo Tz ni jina Mali ya Tanganyika ,hata siku muungano ukivunjika huku kwenye Utajiri wa madini na rasilimali nyingi Pataitwa Tanganyika a.k.a Tanzania.
 
Mkuu tatizo la baadhi ya wasomi wetu muungano lazima uandikwe kwa kizungu kilichojaa maneno ya kilatini na kukubalika na walimu wa kizungu waliowafundisha darasani kuongea kizungu.

Babu yangu na bibi na baba yangu na mama yangu waliungana kuoana bila kuandikiana popote wala kusainiana popote lakini miungano yao ilidumu vizuri.

Muungano wowote ule uwe wa kuandikwa au kutoandikwa uwezeshe maisha ya watu kwenda hayo mambo mengine ya kilatini sijui DE JURE na DE FACTOR yanafaa kuyaongelea mtu akishalewa pombe za kizungu.

Wazo langu mm ni tanganyika tu
lakini kwa mada hii naona pasco kachemka kitu chochote kwanza ni makubaliano ya kile kitu mnacho lenga kuwanzisha mfano ni ndowa kama alivyochangia mchangiaji hapo juu ila maneno tu yanaweza tosha kabisa kuwa muungano. Mm na mke wangu atujandikiana kuwa kitu kimoja lakini maneno yetu ndio yametufanya kuwa kitu kimoja hayo yenu ya. De jure nafocter mm siaelewi
 
Wewe mwenyewe umethibitisha na kuhitimisha kuwa either tz iliundwa kwa de factor au de jure zote ni halali. Sasa tujadili nn tena hapa
 
Muungano huu wa Mdomo ni
muungano wa Ajabu sana uliosalia Duniani,kwani muungano huu licha ya
kudumu kwa miaka 50 ,ni muungano wenye Ukiritimba wa ajabu,mianya ya
Mafisadi kujilia pesa za Umma kiulaini kwa kisingizio cha kumaliza kero
za muungano, kero za muungano na mladi wa watu wachache ambao hawataki
Amani ZNZ ili fungu la kumaliza Kero liendelee kupewa bajeti na wao
huvuna hizo pesa kirahisi,hao watu hawataki kusikia Serikari 3 Maana
zitakimbiza Ulaji wao.

mchakato wa katiba mpya unapaswa kutoa tiba ya kudumu ya kero hizo.
 
Kwa tulipofikia mabadiliko ni muhimu maana Muungano umeshakuwa na dosari watu hawaoni manufaa wanaokazania ni wezi wanaonufaika kwa jina la muungano
 
Jee ile dhana ya kuwa makubaliano rasmi kati ya karume na nyerere yalikua ni wawepo ndani ya muungano huo kwa miaka 10? Then kila nchi itaamua kivyake kama mwanzo.
Hii ni kwasabu muungano huu haukua wa hiari kati ya nyerere na karume bali shinikizo la marekani ndio makubaliano yakawa 10 years kueousha shari ya kuvamiwa znz kufanywa kituo cha USA.
Lakini karume akauliwa kabla ya miaka 10 na hatimae zile hati zikayayuka.
Kuanzia hapo kila aliyesema kuhudu muungano akapata mkongoto wa nyerere
 
Inaitwa 'consent' sijapata tafsiri nzuri ya hili neno lakini nadhani inaitwa dhamira. Uhalali wa mkataba au makubaliano unaanzia hapo kwenye consent au dhamira ya pamoja ya wanaoingia makubaliano au mkataba(mutual consent).
Pasco uhalali wa mkataba upo mikononi mwa waliokatibiana na si vinginevyo, ndo maana UN hawana na hawakuwa na jinsi ispokuwa kuheshi makubaliano yetu "hata kama haikidhi matakwa ya sheria ya mikataba"

kwa maan hiyo ondoa porojo zako hapa.
 
Last edited by a moderator:
Wewe mwenyewe umethibitisha na kuhitimisha kuwa either tz iliundwa kwa de factor au de jure zote ni halali. Sasa tujadili nn tena hapa

Kwanza ni defacto na si defactor, baada ya hapo de facto ie ki muktadha inakubalika, kama ni hivyo ni kuifanyia iwe de jure ie by law kama wadau watakubali
 
Mkuu Pasco mi naona kama vile maswala mengine tungewaachia tu wataalamu wa sheria wayatolee ufafanuzi na tuache kudhani shivji ndio mwenye authority pekee. Maana hili jukwaa linaingiwa na majirani zetu wa nchi za mpakani ambao licha ya umbea unaowaleta vilevile wanatupima na uwezo wetu wa kuchanganua mambo katika kupambana na sisi huko EAC.

Wewe ukiwa kama mwandishi wa habari surely unaweza kwenda kutafuta mawakili waliobobea na kuandika kwa facts, maana kwa wasomaji tusio elewa sheria na ambao atuna muda wa kupekuwa unaweza kutuaminisha vitu sivyo na kutupa ufahamu usio sahihi katika uelewa wa muungano wa taifa letu na uhalali wake.

Sielewi kuna umuhimu wa kwanini (ingawa kwa ufahamu wangu mdogo) ni lazima hiyo 'article of the union' ionekane leo ndio uhalali wa muungano ujulikane. Hila ninachoelewa kisheria ingawa ni 101, ni kwamba mkataba wowote unaanza na 'invitation to treat' ambayo inaenda zaa offer. Offer ambayo inakubaliwa au inakatiliwa, ukishakubali offer either kama ilivyokuja au kwa ku-negotiate other terms to suit you na wote mkaridhia inamaana tayari wewe umesha kubali na hiyo ndio agreement yenyewe aijalishi hipo kwenye karatasi au hipo kwenye maongezi na kuanzia hapo legal binding zinaanza.

Sasa basi si tu kwamba JKN na bwana Karume waliweka makubaliano tu ikaishia hapo tuseme ni muungano wa watu wawili na wengine wamelazimishiwa, hapana bali walienda mbali zaidi hili kuweza kuhalalisha makubaliano yao kwa wananchi na wafikie mkataba ambao unatambulika kimataifa (Kwenye Kitabu cha Pius Msekwa anaongelea ili). Namna walizotumia kuhalalisha makubaliano yao ni kupitia mabunge yao ya wananchi (indirect democracy ambayo inakubalika kimataifa) ambapo ilitakiwa kila bunge independently liliridhie kwa 2/3 ili muungano uanze na kote walipata zaidi ya idadi hiyo ina maana hakuna nguvu iliyotumiwa wala ulaghai wowote uliotumika vitu vilikuwa wazi kabisa na wananchi walishirkiswa kupitia wawakilishi wao (ZnZ wanaopinga ni wale wale tu wa Jamsheed, lakini vitu vilifanyika kwa huwazi na kidemokrasia).

Kuhusu hadithi za watu wengine sijui mkataba ulisema hivi Nyerere akaupoteza na leo ni siri ambapo muungano autakiwi kuwepo according to the time frame ya mkataba etc; hayo ni yaleyale ya kujianzia tu kwa hisia za muungano depending on who's talking, seriously hiyo hoja ni ya kipuuzi mno.

Kisheria za mikataba offer lazima ieleweke na pande zote mbili ili mkataba utambulike as legal binding. Sasa unataka kuniambia JKN na Karume waliwaeleza nini wabunge wao hili wapige kura ya kuungana, cha muhimu ni uelewa wa wabunge waliopiga kura hawa ndio wanahalalisha muungano kwa ridhaa ya wananchi. Hivyo hoja inatakiwa kuwa wabunge walielewa ni muungano gani wanaukabali na si article inasemaje kwa sana.

Na watakuwa wapuuzi sana (JKN na Karume) kama walipanga au waliandika kingine na walicho waeleza wabunge wao maana kama ni mahakamani watataka kujua wabunge walichoelewa sanasana. Kwa sababu huko ndipo legal binding za muungano zilipo halalishwa na kama kuna any vague (kwenye uelewa wa wabunge) na siasa za muungano zilivyoendela wao ndio ilikuwa wawe wakwanza kutoa kasoro mbona amkutuambia hayo. Maana mahakama kwa sana itatakujua walichoelewa wabunge sio article inasemaje kwa sana.

Worst-of kwa wale mnaotafuta hizo hati sijui uhalali wa muungano, contract huwa azibaki vile vile kwa kuwa muungano ulipata baraka za mabunge tu bila ya kura za maoni, mahakama lazima zizingatie 'third party rights' leo, regardless hata kama wanasiasa wanataka kuvunja mkataba wanaita 'frustrating event' kitu kitakacho angaliwa je raia walijua hata kama kweli article ilisema ten years. Maana watu wamefanya decisions based on awareness promoted.

Sasa hapo kuna mlolongo wa mambo mengi sana ya mchanganuo huko mahakamani kama human rights na mambo mengine ya ajabu kwa sisi ambao si wanasheria yanachosha kuyaelewa vitu kama subsequent illegality, radical changes in circumstances, ukitupia na mambo ya siasa: ndio maana wenzetu wakifikia hatua kama hizi kitu muhimu ni-kura ya maoni, as in Scotland habari za mfalme Stewart sijui nani alikubalina hiki sio kile no one wants to know, hapa wananchi waamue. Vinginevyo ni hadithi tu za kwenda sijui 'New York' kutafuta makarabasha, sijui Nyerere katuzulumu etc to do with tosh.
 
  1. Ili makubaliano yoyote yaitwe mkataba ni lazima yawe na sifa kuu 4 za mikataba, zinazoitwa vipengele, na kikikosekana kimoja wapo cha sifa hizo, then huo sio mkataba bali ni makubaliano tuu ambayo nayo ni halali. Makubaliano hayo ya Muungano hayana zile sifa kuu 4 za mkataba. Jee sifa hizo kuu 4 za mkataba ni zipi?!. (Hii sio thread ya contents za Hati za Muungano bali presence ya hati hizo). Ili kujua kwa nini hati za muungano sio mkataba bali ni makubaliano, then itakubidi unitembelee hapa!- Jee Wajua Kuwa Tanzania Hatuna Mkataba wa Muungano?. Kilichopo ni Makubaliano Tuu!.
.

Sasa nimeanza kuelewa kwanini CUF (ZNZ) na UAMUSHO wanang'ang'ania Muungano wa MKATABA. Wakati sisi Watanganyika upeo wa kuona mambo yetu hauzidi urefu wa pua zetu. Wenzetu Wazanzibari they are miles away. Masikini Tanganyika!
 
Sasa nimeanza kuelewa kwanini CUF (ZNZ) na UAMUSHO wanang'ang'ania Muungano wa MKATABA. Wakati sisi Watanganyika upeo wa kuona mambo yetu hauzidi urefu wa pua zetu. Wenzetu Wazanzibari they are miles away. Masikini Tanganyika!

Povu la nini huu unao sainiwa uko wapi? Butiama?
 

Attachments

  • 1396773586194.jpg
    1396773586194.jpg
    31.6 KB · Views: 122
Kwa tulipofikia mabadiliko ni muhimu maana Muungano umeshakuwa na dosari watu hawaoni manufaa wanaokazania ni wezi wanaonufaika kwa jina la muungano

Sababu Za Nyerere na karume kuunganisha Tanganyika na Zanzibar ,zilikuwa ni Usalama kwa kuhofia Marekani kuweka Kambi ya kijeshi hapo Visiwani kisha Tanganyika ikawa Mashakani huku Pia Walikuwa na Lengo la kuja Kuwa na Serikali moja tu ambayo ingepunguza Gharama za kuendesha Nchi mbili . Ukichunguza muungano wa zamani haufanani na muungano wa sasa,Muungano sasa umegeuka biashara, Dili,na Mladi wa Wajanja Wachache ambao wananufaika na Pesa za mgao wa Zanzibar toka Hazina iliyopo Tanganyika , hicho kikundi cha wajanja kipo Pande zote lakini wengi wapo Zanzibar na Tanganyika ni wachache sana wananifaika na muungano , huku CCM wakiwa Kinara kwa kuvuna Ruzuku kubwa ya pande zote mbili na maujanja mengineyo mengi tu,kwa kifupi Mkataba wa Muungano haupo labda wajanja wauchakachue na kujidai ndio mkataba harisi . Muungano wa makubaliano ya wawili sasa umechukua sura ingine , Zanzibar wao wameshatangulia wapo mbali lakini Tanganyika bado kalala, huku ccm akiwa macho anatafuna vyake akiwa anawachungulia Watanganyika Kama wameamka.
 
Zanzibar ipo macho inasonga mbele kwa Speed ya Radi huku ccm wakiwa Ubavuni mwao, Tanganyika bado wapo usingizini hawajaamka ndio Maana ccm imetumia fursa hiyo kulazimisha serikali mbili ili kulinda masilahi Yao .huu muungano wa makubaliano sasa ni Kama haupo kwani Zanzibar imevunja katiba inajifanyia yake itakavyo na Tanganyika kubaki wakisema Ndio mzee.
 
Sasa nimeanza kuelewa kwanini CUF (ZNZ) na UAMUSHO wanang'ang'ania Muungano wa MKATABA. Wakati sisi Watanganyika upeo wa kuona mambo yetu hauzidi urefu wa pua zetu. Wenzetu Wazanzibari they are miles away. Masikini Tanganyika!
Wasemaji wa Tanganyika ndio hao hao wanaonufaika kupitia mapungufu na kasoro za muungano hawapendi serikari moja au tatu wanajua zitafichua mengi na wao kuumbuka sasa wamekituma kizee Shivji kianzishe mkanganyiko ili waendelee kula pesa mpaka watu kuja kushituka baadae watakuwa tayari wameshiba na kuja na mbinu zingine za kuwahadaa watanganyika.
 
Kweli Tanzania sio nchi ila ni muungano wa Nchi mbili Tanganyika na Zanzibar. mie huwa nashangaa ifikapo tarehe 9/Desemba kila mwaka tunasherehekea Uhuru, lakini hakuna anayetamka sherehe za Uhuru wa Tanganyika utasikia Uhuru wa Tanzania Bara, hakuna nchi Tanzania Bara au Tanzania iliyopata uhuru Tarehe hiyo. Hebu Jamani tuwe wa kweli!!!!
 
Tanganyika ni kubwa sana ki population na eneo lakini ukienda kifikra na mawazo wanaotumia akili zao na walio active na ulimwengu ki pacentage ni ndogo sana wengi wana buruzwa tu, dalili hii ni pale Zanzibar inapo kata kuburuzwa na pamoja na udogo na uchache wao nahisi Zanzibar na wapemba ni maarufu duniani kuliko the huge Tanganyika./
 
Back
Top Bottom