mr pipa
JF-Expert Member
- Jul 26, 2021
- 2,330
- 4,853
Kuna jamaa yangu mmoja yeye ni mtu wa kupenda kesi, huyu jamaa ikipita wiki hajafanya tukio jua atakuwa anaumwa.
Moja ya tukio lililoniacha mdomo wazi na kujiuliza kama huyu mwenzangu ni binadamu wa kawaida au vipi?
Kuna siku kaja kwangu anahitaji kibarua cha kulima basi nikamwambia nenda kwa jamaa anataka mfanyakazi wa kulima na kweli akapelekwa site akaoneshwa akaanza kazi, baada ya wiki akampigia simu boss wake uje upande nimemaliza, basi boss akabeba mbegu zake kwenda kupanda kufika kule boss anakuta kamlimia matuta mawili na tayari kashakula pesa nusu.
Mwenye shamba akachukia sana akamtia makofi na kumpeleka polisi, wakamuweka ndani wiki na kuambiwa alipe jamaa akadai anamtafutia pesa yake. Imepita wiki jamaa kapewa pesa yake kumbe alienda tafuta wateja kuuza shamba lile lile la jamaa, hapa ninapoongea kesi ipo mahakamani.
Kiufupi huyu jamaa ana matukio ya ovyo mfano hakuna na wala habadiliki wala kujifunza.
Je, ushawahi kukutana na watu wa aina hiyi kwenye jamii yako?
Moja ya tukio lililoniacha mdomo wazi na kujiuliza kama huyu mwenzangu ni binadamu wa kawaida au vipi?
Kuna siku kaja kwangu anahitaji kibarua cha kulima basi nikamwambia nenda kwa jamaa anataka mfanyakazi wa kulima na kweli akapelekwa site akaoneshwa akaanza kazi, baada ya wiki akampigia simu boss wake uje upande nimemaliza, basi boss akabeba mbegu zake kwenda kupanda kufika kule boss anakuta kamlimia matuta mawili na tayari kashakula pesa nusu.
Mwenye shamba akachukia sana akamtia makofi na kumpeleka polisi, wakamuweka ndani wiki na kuambiwa alipe jamaa akadai anamtafutia pesa yake. Imepita wiki jamaa kapewa pesa yake kumbe alienda tafuta wateja kuuza shamba lile lile la jamaa, hapa ninapoongea kesi ipo mahakamani.
Kiufupi huyu jamaa ana matukio ya ovyo mfano hakuna na wala habadiliki wala kujifunza.
Je, ushawahi kukutana na watu wa aina hiyi kwenye jamii yako?