Khalu
JF-Expert Member
- Oct 3, 2017
- 525
- 565
Wakuu salaam.
Wakuu nimeona nishee na nyinyi hili tukio.
Kuna siku moja nikiwa maeneo ya Mbagala nikitembea pembezoni mwa barabara kuelekea stendi kwa ajili ya kupanda gari, nilitupia macho upande wa barabara kubwa (kilwa road) kwa mbali kidogo nikamuona baba mmoja mtu mzima akivuka barabara kutokea upande niliokuwepo.
Yule baba alikuwa akivuka barabara huku akitoa kitambaa -cha kufutia jasho- katika mfuko wa nyuma wa suruwali yake kwa ajili ya kujifuta jasho, alikitoa kwa kukivuta hivi kidogo, kile kitambaa kilichomoka pamoja na noti tatu, zile noti zikaangukia barabarani pasi na yeye kujua, kwa rangi ya zile noti bila shaka zilikuwa ni noti ya shingi elfu tano, elfu mbili na elfu moja.
Sekunde chache baada ya tukio hilo kutokea, walitoka vijana watatu wa bodaboda, kutokea upande aliotokea yule baba, wakizikimbilia zile noti na kuziokota, kisha wakarejea walipo kuwa.
Yule baba hakuwa na habari ya kilichotokea nyuma yake, yeye aliendelea kujifuta jasho, huku akiangalia magari ili amalizie kuvuka barabara kuelekea upande wa pili.
Binafsi nilishindwa kushangaa, na kubaki nikijiuliza maswali.
Je, ni uungwana kweli mtu kuokota kitu huku anamuona aliye kiangusha na asimrudishie?
Jaribu kuvuta picha ungelikuwa ni wewe umeangusha ni sahihi usirudishiwe?
NB; Huenda nikawa sio mwandishi mzuri lakini nadhani nimeeleweka.
Wakuu nimeona nishee na nyinyi hili tukio.
Kuna siku moja nikiwa maeneo ya Mbagala nikitembea pembezoni mwa barabara kuelekea stendi kwa ajili ya kupanda gari, nilitupia macho upande wa barabara kubwa (kilwa road) kwa mbali kidogo nikamuona baba mmoja mtu mzima akivuka barabara kutokea upande niliokuwepo.
Yule baba alikuwa akivuka barabara huku akitoa kitambaa -cha kufutia jasho- katika mfuko wa nyuma wa suruwali yake kwa ajili ya kujifuta jasho, alikitoa kwa kukivuta hivi kidogo, kile kitambaa kilichomoka pamoja na noti tatu, zile noti zikaangukia barabarani pasi na yeye kujua, kwa rangi ya zile noti bila shaka zilikuwa ni noti ya shingi elfu tano, elfu mbili na elfu moja.
Sekunde chache baada ya tukio hilo kutokea, walitoka vijana watatu wa bodaboda, kutokea upande aliotokea yule baba, wakizikimbilia zile noti na kuziokota, kisha wakarejea walipo kuwa.
Yule baba hakuwa na habari ya kilichotokea nyuma yake, yeye aliendelea kujifuta jasho, huku akiangalia magari ili amalizie kuvuka barabara kuelekea upande wa pili.
Binafsi nilishindwa kushangaa, na kubaki nikijiuliza maswali.
Je, ni uungwana kweli mtu kuokota kitu huku anamuona aliye kiangusha na asimrudishie?
Jaribu kuvuta picha ungelikuwa ni wewe umeangusha ni sahihi usirudishiwe?
NB; Huenda nikawa sio mwandishi mzuri lakini nadhani nimeeleweka.