Je uliya jua haya kuhusu Clouds Media?

Status
Not open for further replies.
Jamani nani kawambia ukiwa na degree ndio soln ya kufabya kazi kwa ufanisi;sio nawatetea vijana wana vipaji na kama kweli awana elimu vyema washirikishwe kozi ndogo ndogo..labda kwa kifupi tu

ni marubani 5 kati ya 50 walio na degree
na wanaoendesha ndege zetu kwa upande wa atc na precission na wale wasiokuwa na degree
wapo very bright hasa wakikumbana na anga za ajabu ajabu ..ukiacha makosa madogo madogo ya kawaida
so atukatai lakini vyema wakaelezwa kujiendeleza na kujifunza kujua jinsi ya kuheshimu mahali pa kazi ni meona ma dada fulani wanatukana tukana ovyo kwenye redio na vipindi vyao dina na gea kama si kosei ukisikia vipindi vyao haata

Issue sio degree tu .Cheti ni kitambulisho kuwa umesomea hiyo kazi. Hatuwezi kuendesha mambo kwa eti vipaji* Media ni chombo muhimu kwa maendeleo na kama wanaokiendesha ni failures hayo maendeleo yatakujaje? Nashangaa wanaJf wengine wanashabikia vipaji -usanii- .Media is a proffesional institution which ought to be run in a proffessional manner. Lack of that ca'nt be called media rather a caricuture type of . Sio ajabu ndio maana imekuwa ikirusha hewani propaganda za kipuuzi kama zile za kukandia mgomo , na upuuzi kibao kama yale ya akina Zinduka n.k
 
Come on people! Who said you need a degree to be an enternainer? Makazini mnashina na the so called wasomi, do you seriously still need to listen to another bunch of "wasomi" on your way home? They might rub some of you the wrong way but isn't that part of this life? you can't please everyone either!
 
WABEROYA hivi na wewe umeajiliwa clouds ? naona unatoa thanx kwa kila mtu anayewafagilia hao radio mapenzi na ngono kip ya respect bwana ,,
 
WABEROYA hivi na wewe umeajiliwa clouds ? naona unatoa thanx kwa kila mtu anayewafagilia hao radio mapenzi na ngono kip ya respect bwana ,,

Demu wake anafanya kazi huko! Ndo maana anawafagilia LOL
 
Kuannzia lini bongo fleva na shule vinapikika chungu kimoja?

Dah kumbe jamaa vichwa sana.
Hata kama shule hakuna lakini jamaa wana make sasa hivi ni masupa star wa bongo na wanausafiri hata kama corola sio mbaya.
 
You can think bigger than that. I LOL

Hawa vijana wamejitahidi sana kuwa wajasiriamali mpaka wanawazidi hata Maprof wetu.
Safi sana vijana wa Kusaga mmepiga hatu hata wasomi wa nz'i hii hawatii mguu kwenu.
Hata kama una zero lakini upo juu kuliko mwenye Masters big up vijana wetu walio taga wanaiga kwenu kiujasiriamali zaidi.
Mmekuwa kioo cha jamii lakiona msinunuliwe na mafisadi naona wamesha anza kumendewa wanainadi SHISHIEMU sasa.
 
Hawa vijana wamejitahidi sana kuwa wajasiriamali mpaka wanawazidi hata Maprof wetu.
Safi sana vijana wa Kusaga mmepiga hatu hata wasomi wa nz'i hii hawatii mguu kwenu.
Hata kama una zero lakini upo juu kuliko mwenye Masters big up vijana wetu walio taga wanaiga kwenu kiujasiriamali zaidi.
Mmekuwa kioo cha jamii lakiona msinunuliwe na mafisadi naona wamesha anza kumendewa wanainadi SHISHIEMU sasa.

Hii inatia kichefu chefu! Mkuu uko Pub ama umeamka nazo?
 
Nadhani ubaya wa baadhi ya watangazaji wa hiyo Radio ni ile ya kuwakandamiza watu wengine ambao hawana uwezo sawa naoko kwenye kupata air time, ni lazima tukubali kuwa kuna vitu ambavyo huwezi kufanya eti kwa sababu tu wewe una media kwa hiyo ukatumia hiyo power uliyonayo kinyume na kuwakandamiza watu wasiokuwa na uwezo wa kupata nafasi sawa na wewe. Ingekuwa na maana sana kwa mfano kwa swala la mgomo wa TUCTA wao jahazi kusema yale waliyosema kama TUCTA wangekuwepo pale studio, lakini kutoa hukumu zile walizotoa wakina Kibonde na bwana Gadna bila TUCTA kuwepo pale nao waseme side yao ya stori sio kitu kinachokubalika kabisa, na hii ndio imepelekea watu wenye hasira waache kuzungumzia mambo na kuanza kuzungumzia watu ambacho sio kitu kizuri. Nadhani cha msingi wanatakiwa kujua nini wanaweza kufanya na nini hawawezi kufanya hata kama wanayo radio ambayo wana uhuru wa kuzungumza chochote lakini wasivuke mipaka. Radio ndio zilisababisha watu kuuana huko Rwanda mwaka 1994 watu walitumia vibaya hizo radio. Tuwe waangalifu lakini hilo sio la kufanya tuzungumzie watu badala ya mambo.

wanabidii] RE: CLOUDS FM na Porojo Zake


Reply |Selemani ****** to wanabidii, ethinktanktz, mwananchi, wanazuoni
show details Apr 13 (6 days ago)


Wanabidii wote,

Samahani sana naomba kwa ruksa yenu nilete mada mpya kidogo ili tuijadili. Ninahuzunishwa sana na utendaji kazi wa watangazaji wa FM Clouds. Na hapa ni zuri nikawataja majina, hawa ni watangazaji wanaotangaza kipindi cha "Jahazi" nao ni ndugu Kibonde na Gardner Harbash. Hivi hawa ni watangazaji wa wapi!? Je wamesomea hii kazi ya utangazaji? Je wanafahamu maaadili ya utangazaji au wanazingatia maadili ya kazi yao? Naamini kabisa kazi hii ina maadili yake, hivi wanavyotangaza wanazingatia maadili hayo?

Siku mbili zilizopita CCM walizindua kampeni yao kukusanya bilioni 40. Kibonde alikuwa mshehereshaji katika shughuli hiyo. Sina tatizo na hilo kwani anatafuta ugali wa watoto. Nilihisi kuwa baada ya tukio hilo basi kipindi kinachofuata cha Jahazi kitatawaliwa na tukio hilo. Na ikawa hivyo. Ikawa kweli kabisa. Kibonde na Gardner wakatumia kipindi hicho kuwapigia kampeni CCM. Gardner akasema kuwa anaomba aelekezwe namna ya kuchangia kwani anapenda sana mambo yao (CCM), hivyo naye angependa kuchangia. Sina tatizo na yeye kuchangia, lakini ni muhimu ajue kuwa anazungumza na watanzania ambao wana itikadi tofauti. Yeye kama mtangazaji anao wajibu wa kuufanya uchaguzi uwe huru na wa haki. Na katika kufanya hivyo analazimika kutoa nafasi sawa kwa vyama vyote vya siasa. Kama anakipigia chama cha CCM basi ni lazima hakikishe kuwa anavipa nafasi na vyama vingine. Kutokana na na kuzungumza maneno yao yanayokera kwa kujitafutia maslahi yao binafsi, msikilizaji mmoja aliwatumia ujumbe na kuwaambia kuwa "kipindi chenu kimejaa UCCM, vipi mnatafuta ulaji wakati wa uchaguzi?" Walimjibu kwa kejeli lakini naamini ujumbe ulifika na walifahamu kuwa watu hawapendi hizo tabia zao za kuganga njaa na kutafuta ulaji. Labda wana ndoto kuwa watapata nafasi, sijui labda ya ukatibu wenezi msaidizi au uhamasishaji.

Mtangazaji au mwandishi wa habari una wajibu kwa jamii na si kwa watawala. Una wajibu wa kuwafunua macho wananchi ili wafanye maamuzi sahihi na wafanye informed choices. Na si kugeuka kuwa propagandist kwa ajili tu ya kuangalia maslahi yako, na mbinu za kutafuta cheo. Hawa ni lazima wakemewe na wasemwe. Katika kipindi hiki cha uchaguzi tutawaona wengi sana wa namna hii. Kwani kwa bahati mbaya wanajua mshindi ni nani, hivyo wanaanza kujipendekeza mapema ili awape nafasi waweze kujinufasiha wao na familia zao.

Wao kama ni watangazaji wa kweli kwa nini wasiseme wito aliotoa Mwenyekiti kuwa matajiri wawadhamini wagombea wa CCM. Je sheria aliyoipitisha kwa mbwembwe ndio inavyosema hivyo? Kwa nini hawaelimishi watu katika masuala kama haya ya msingi?

Hili ni moja tu, lakini nimewahi kuwasikia mara nyingi wakipotosha au wakisema maneno ambayo ni kinyume kabisa na maadili ya utangazaji. Ipo siku wamewahi kusema kuwa Kingunge ni Waziri anayeshughulikia siasa na jamii. Ilhali nafasi hiyo ilikwishaondolewa. Hata pale msikilizaji alipowakumbusha hawakuomba radhi, kwa sababu hawana maadili na wanadhani watu wanaosikiliza hawana upeo wa kuelewa mambo.

Wao wamekuwa ni wataalamu wa kila kitu, kila jambo wanalitolea ufafanuzi, liwe la kisheria, uchumi, siasa na hata la kidaktari wao ni wataalam!!

Juzi juzi wamemkaraibisha Mrema kwa sababu tu anapinga mgomo wa wafanyakazi. Leo hii amekuwa mtu wa maana na anapewa nafasi ya kuzungumzia suala hilo. Kinachosikitisha ni wao kulichukulia kirahisi sana na kuanza kuwalaumu viongozi wa muungano wa vyama vya wafanyakazi. Kwa nini hawajiulizi hivi kwa nini watu wanagoma? Chanzo cha migomo nchini nini? Kwa nini tumekuwa na wimbi kubwa la migoma nchini katika siku za hivi karibuni? Tumejenga utamaduni kuwa bila kugoma hupati haki yako. Hawa si kwanza; Wafanyakazi wa NMB waligoma wakapewa haki yao, mara ngapi wahadhiri chuo kikuu wanagoma? au kutishia kugoma? wafanyakazi wa reli mara ngapi wanagoma ndio wanapewa mishahra yao? Hapa ni nani wa kumlaumu? anayenyima haki au anayedai haki haki yake kwa kugoma?

Kwa kuwafahamisha, ukiona jamii yoyote inaingia katika utamaduni huu, ujuwe kuwa HAKUNA HAKI, hakuna sheria na kwa kweli kuna ombwe (vacuum) ya uongozi. Wananchi wanaona hawana njia yoyote isipokuwa kugoma. Kwani hawasikilizwi na hawathaminiwi. Wanapoamua kugoma ni lazima mjuwe kuwa wamejaribu njia zote za amani na imeshindikana. Kugoma ni hatua ya mwisho baada ya kuona kuwa madai yao yanapigwa danadana.

Kuhusu maslahi ya wafanyakazi; Kwa mfano kwa nini mpaka leo serikali haijaitoa hadharani ripoti ya Ntukamazina ambayo ilipewa kazi ya kuangalia mishahara ya wafanayakazi na kutoa mapendekezo? Kwa nini kuna usiri? Kwa nini hawazungumzii mabilioni ya pesa yanayotumika kuwalipa vigogo posho, allowances na per diem zisizokuwa na kichwa wala miguu? kwa nini hawazungumzii real issues badla yake wana trivialize issues?

Watangazaji kama hawa ni hatari sana. Hata katika dola ambazo zilikuwa na ukandamizaji mkubwa sana ambao ulileta maafa makubwa, watangazaji na redio kama hizi zilitumika ku perpetuate motives mbaya za watawala. Hata katika mauaji ya kimbali katika sehemu nyingi za dunia na hata kwa majirani zetu, redio zilitumika katika kufanikisha unyama huo. Hatutaki redio za namna hii, ziwe za umma au mtu binafsi hatuzitaki. Hatutarajii redio zitumike katika kuwafumba macho wananchi, tunataka redio zitakazowafanya watu kuhoji, kujiuliza maswali, kutafakari, redio zinazoongeza ufahamu wa watu. Na hilo litatuletea maendeleo ambayo kila mtu atanufaika nayo na si maendeleo tu yako wewe mmoja ya kutaka kupata ulaji ndani ya chama tawala.

Asante

Selemani
Hii post ndio imeibua haya yote.
 
Kapteeeni! Nilijua tu wabongo watawaonea wivu!Nani amekwambia kuwa na degree ndo mtangazaji mzuri!Vipi ulinyimwa kazi nini pale clouds?Ukweli utabaki palepale hata kama kuna makosa madogo madogo wanayoyafanya lakini ni wabunifu wa vipindi mbalimbali vizuri sana na wana vipaji vya hali ya juu!Mbona walibuni kuchangisha michango kwa ajili ya maafa ya Kilosa hamjasema,wako wapi basi hao wasomi wenu wa vituo vingine walifanya nini?HONGERINI CLOUDS.
Mbona waziri mkuu wenu wa zamani alikuwa na diploma ya kilimo toka Tengeru Arusha na hamjasema?Si ameongoza miaka kumi?Je na yule mwingine aliyejiuzulu na elimu yake yako wapi?

Nyie ndo Mkapa aliwaambia 'ACHENI WIVU WA KIKE KIKE''
Chapa kazi CLOUDS
 
Kapteeeni! Nilijua tu wabongo watawaonea wivu!Nani amekwambia kuwa na degree ndo mtangazaji mzuri!Vipi ulinyimwa kazi nini pale clouds?Ukweli utabaki palepale hata kama kuna makosa madogo madogo wanayoyafanya lakini ni wabunifu wa vipindi mbalimbali vizuri sana na wana vipaji vya hali ya juu!Mbona walibuni kuchangisha michango kwa ajili ya maafa ya Kilosa hamjasema,wako wapi basi hao wasomi wenu wa vituo vingine walifanya nini?HONGERINI CLOUDS.
Mbona waziri mkuu wenu wa zamani alikuwa na diploma ya kilimo toka Tengeru Arusha na hamjasema?Si ameongoza miaka kumi?Je na yule mwingine aliyejiuzulu na elimu yake yako wapi?

Nyie ndo Mkapa aliwaambia 'ACHENI WIVU WA KIKE KIKE''
Chapa kazi CLOUDS

Mkuu kabla ya kuongea jaribu kufanya japo kautafiti kidogo juu ya jambo unalotaka kuliongelea, Unajua waanzilishi wa hiyo idea ya kuchangia waanga wa mafuriko ya Kilosa na Same? Basi kwa taarifa yako tu hiyo Idea iliporwa kwa mtu
 
Nilijua tu moto waliouwasha kwa kuishambulia JF hautazimika kirahisi..sasa data zinazidi kuibuka...kweli usianzishe vita vya mawe wakati unakaa kwenye nyumba ya vioo.
 
Big up clouds,kama mna workforce yenye level hii ya shule na bado mnazitoa jasho redio zote hapa nchini,mnastahili pongezi.Hata hivyo ni muhimu kusikiliza maoni ya wasikilizaji wenu.Clouds tv lini?,can't wait.
 
sio wote walioenda shule wana vipaji wengine ni talanta yao.
 
Big up clouds,kama mna workforce yenye level hii ya shule na bado mnazitoa jasho redio zote hapa nchini,mnastahili pongezi.Hata hivyo ni muhimu kusikiliza maoni ya wasikilizaji wenu.Clouds tv lini?,can't wait.
CloudsTV mbona iko hewani toka December mwaka jana Sema Signal yake ni ndogo sana hivyo baadhi ya watu wanashindwa kuipata, hata hivyo wapo hewani kwa majaribio.
 
kibonde alikuwa azania akaondoka na zero

Gadna alikuwa Popatilal akaondoka na zero

Kusaga pia ni almost drop out- alitoka marangu sec na zero
Yaani nilidhani Kibonde na Gadna angalau ndio hao wawili wenye degree za chuo kikuu.
 
sio wote walioenda shule wana vipaji wengine ni talanta yao.

Kabula ambacho umesahau ni kuwa huwezi kuendesha taasisi ukiwa na rundo la vihiyo , haiwezekani, ile ni taasisi inayolisha watu , ni taasisi inayotegemewa kuelimisha umma, huwezi kutegemea Vipaji na talanta bila elimu katika ulimwengu wa leo.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom