Arusha kama zilivyo sehemu nyingi za Tanzania elimu inatukosesha mengi..
Bado wengi wetu hatujawa na uwezo wa kuchagua kiongozi bora wa kutuwakilisha sisi na matatizo yetu bungeni na pia kusimamia rasilimali tulizonazo kwa manufaa yetu sisi!
Tulifanya kosa kuwavumilia CCM ya Mrema kwa kipindi kirefu sana tukiamini kuna amani na uchumi wa mkoa ni mzuri kupita maelezo,awamu hii tena tumefanya kosa kuchagua kiongozi wa vurugu na maandamano!
Wenye uwezo wa kugundua udhaifu wa Lema wanamchagua kutokana na mapenzi ya Chadema tu na wasio na uwezo kiakili wanamchagua wakidhani mtu anayeingia kwenye ugomvi na serikali kila mara ndo "Mandela" au mkombozi wao!
Kiongozi bora ni zaidi ya kufanya vurugu na maandamano,Lema hanaga hoja nzito zinazomatch na potential ya jiji la Arusha,ana bahati sana wakazi wa Arusha ni "vurugu oriented" ndo maana anaeleweka kwa ujinga anaoufanya na anatumia vurugu kama mtaji wake!
Mimi nasema Lema kwa Arusha HAPANA!
Chadema au chama kingine chochote chenye watu potential zaidi ya Lema tunaomba mtuletee tuwapime!
Hoja over Chama! Kama mtu anafaa hata akitoka CHAUSTA aje Tue.
Lema kapumzike aisee.