GUSSIE
JF-Expert Member
- Dec 2, 2014
- 3,866
- 11,100
Wanabodi, Mimi sio mtaalamu wa lugha ya mawasiliano"Communication skills".Ingawa natambua kwa kila neno utakaloongea au kuropoka (Transfering message) lazima usubiri mrejesho mzuri au mbaya( Feedback)
Mbunge umepewa dakika kumi za kujenga hoja na kutoa suluhisho la matatizo Bungeni, Unatumia dakika tano kumsifia Mkuu wa nchi kuwa ameshinda kwa kishindo wakati yeye mwenyewe Mkuu wa nchi alisema hataki kusifiwa kwani kama sifa alishasifiwa sana anahitaji kazi ionekane na dakika tano zilizobaki unatumia kuwashukuru watoto wako, Baba yako, Marafiki mliocheza nao rede, kombolela na wote ulioimba nao nzu nzu we Mama nyuki lia eeh, luka mbali kutafuta ua nzuri la asali na dakika kumi zinakuwa zimekwisha, Hii sio sahihi kabisa
Nakuomba ndugu Humprey Polepole natambua wewe unafahamu jambo hili na miezi michache iliyopita nilikuona pale udsm kwenye taasisi ya "Institute of Development studies" au IDS ukimalizia PhD yako .Naomba uwape semina hawa wabunge wetu kwa kutumia uwezo wako toka hapo IDS ambapo marehemu Prof. Mpangala alikuwa akishusha nondo miaka hiyo
Kwa dakika kumi yampasa Mbunge atumie dakika tano kuchambua tatizo na kulielezea nini chanzo na madhara yake kiuchumi au kijamii hapa akihusisha na mazingira ya jimbo lake au nchi kwa ujumla.Yampasa mbunge kushawishi wabunge wenzake juu ya ukubwa wa tatizo na athari kiuchumi au kijamii
Dakika tano za mwisho Mbunge yampasa atoe suluhisho jinsi ya kutatua tatizo hilo kwa mifano halisi au kwa nadharia. Nguvu yake ya ushawishi na suluhisho ndio hupelekea hoja yake kukubalika mbele ya Bunge na wananchi
Ni muhimu kabla ya kuingia Bungeni wabunge wakafanya utafiti hata wa kupokea takwimu na Data toka kwenye taasisi au Majimboni kwao. Kutumia dakika kumi kusifia na kushukuru bila kujadili mustakabali wa nchi yetu sio sahihi, Leo hii dunia inasonga mbele kwa teknolojia ni muda wa kujadili mambo yafuatayo
Mosi, Lini tutapeleka chombo chetu katika anga la juu. Tutatumia watu gani na kwa muda gani?
Pili, lini elimu yetu tutaifungamanisha na teknolojia ya kisasa ili kuzalisha watendaji na sio wasimamizi
Yote Dkt Charles Kimei alijitahidi sana kuelezea kuhusu ishu ya elimu yetu kuwa lazima iwe elimu ya kuwawezesha vijana kufanya kazi kwa teknolojia ya kisasa na Bodi ya mikopo iwekeze kwenye mfumo huo wa elimu
Mwisho, Wapiga kura na wasiopiga kura hatukuwatuma Bungeni kusifia na kushukuru kwa dakika zote unazopewa, Tuliwatuma kujenga hoja na kutoa suluhisho la matatizo
Mbunge umepewa dakika kumi za kujenga hoja na kutoa suluhisho la matatizo Bungeni, Unatumia dakika tano kumsifia Mkuu wa nchi kuwa ameshinda kwa kishindo wakati yeye mwenyewe Mkuu wa nchi alisema hataki kusifiwa kwani kama sifa alishasifiwa sana anahitaji kazi ionekane na dakika tano zilizobaki unatumia kuwashukuru watoto wako, Baba yako, Marafiki mliocheza nao rede, kombolela na wote ulioimba nao nzu nzu we Mama nyuki lia eeh, luka mbali kutafuta ua nzuri la asali na dakika kumi zinakuwa zimekwisha, Hii sio sahihi kabisa
Nakuomba ndugu Humprey Polepole natambua wewe unafahamu jambo hili na miezi michache iliyopita nilikuona pale udsm kwenye taasisi ya "Institute of Development studies" au IDS ukimalizia PhD yako .Naomba uwape semina hawa wabunge wetu kwa kutumia uwezo wako toka hapo IDS ambapo marehemu Prof. Mpangala alikuwa akishusha nondo miaka hiyo
Kwa dakika kumi yampasa Mbunge atumie dakika tano kuchambua tatizo na kulielezea nini chanzo na madhara yake kiuchumi au kijamii hapa akihusisha na mazingira ya jimbo lake au nchi kwa ujumla.Yampasa mbunge kushawishi wabunge wenzake juu ya ukubwa wa tatizo na athari kiuchumi au kijamii
Dakika tano za mwisho Mbunge yampasa atoe suluhisho jinsi ya kutatua tatizo hilo kwa mifano halisi au kwa nadharia. Nguvu yake ya ushawishi na suluhisho ndio hupelekea hoja yake kukubalika mbele ya Bunge na wananchi
Ni muhimu kabla ya kuingia Bungeni wabunge wakafanya utafiti hata wa kupokea takwimu na Data toka kwenye taasisi au Majimboni kwao. Kutumia dakika kumi kusifia na kushukuru bila kujadili mustakabali wa nchi yetu sio sahihi, Leo hii dunia inasonga mbele kwa teknolojia ni muda wa kujadili mambo yafuatayo
Mosi, Lini tutapeleka chombo chetu katika anga la juu. Tutatumia watu gani na kwa muda gani?
Pili, lini elimu yetu tutaifungamanisha na teknolojia ya kisasa ili kuzalisha watendaji na sio wasimamizi
Yote Dkt Charles Kimei alijitahidi sana kuelezea kuhusu ishu ya elimu yetu kuwa lazima iwe elimu ya kuwawezesha vijana kufanya kazi kwa teknolojia ya kisasa na Bodi ya mikopo iwekeze kwenye mfumo huo wa elimu
Mwisho, Wapiga kura na wasiopiga kura hatukuwatuma Bungeni kusifia na kushukuru kwa dakika zote unazopewa, Tuliwatuma kujenga hoja na kutoa suluhisho la matatizo