Je, Rais Magufuli "amechemka" kuhusu serikali yake kununua zao la korosho?

Mystery

JF-Expert Member
Mar 8, 2012
15,484
30,159
Tumemsikia Waziri wa kilimo, Mheshimiwa Japhet Hasunga, akiongea na waandishi wa habari, akielezea mpango "mpya" utakaotumika katika ununuzi wa zao la korosho, katika msimu ujao

Katika Maelezo yake amesema serikali itasimamia tu zoezi hilo, lakini haitajihusisha na ununuzi huo wa zao hilo la korosho kwa nchi nzima. Akaendelea kueleza kuwa wanunuzi watakuwa wafanyibiashara wa korosho na mtindo utakaotumika utakuwa ni wa wazi na wa kutumia zabuni.

Maelezo ya Waziri Hasunga ni tofauti kabisa na msimamo aliokuwa nao Rais Magufuli mwaka Jana.

Msimamo wa Rais wa mwaka jana ulikuwa kwa serikali kununua korosho yote iliyozalishwa na wakulima na ndicho kitu kilichosababisha kilio kikubwa sana kwa wakulima wa korosho wa mikoa ya Kusini, ambao hawakulipwa na serikali hiyo pamoja na kutamba kufanya hivyo kwa mbwembwe nyingi.

Hata wabunge wa CCM wa kutoka mikoa hiyo ya Kusini walitishiwa kuvuliwa ubunge wao, iwapo wangeendelea kuwasemea wakulima wao wa korosho, kuwa serikali yetu imewadhulumu korosho Zao na hata Waziri Mkuu wetu, Kassim Majakiwa, akatishiwa kupigiwa shangazi zake, iwapo hizo "ngebe" zisingekoma!

Hivi nani hakuona "mbwembwe" za wanajeshi wetu kumiminika na malori yao huko Kusini mwa nchi yetu, walikoamriwa kwenda kwa ajili ya kwenda kusomba korosho hiyo na hata tukaambiwa kuwa hao wanajeshi wetu wana uwezo wa kuzibangua korosho zote zilizovunwa??

Wanasiasa wengi na wananchi kwa ujumla wao walitahadharisha mno kuwa njia hiyo wanayoitumia viongozi wetu wa serikali ya awamu ya tano siyo sahihi

Tujikumbushe tena namna Waziri mkuu, Kassim Majakiwa "alivyoumbuliwa" na Rais Magufuli, pale aliposema kuwa ametafuta kampuni moja ya kichina, ambayo imekubali kununua korosho yetu yote na kuisafirisha

Jibu alilopewa Waziri mkuu, bado tunalikumbuka sisi sote, kwa kuambiwa kuwa aachane na kampuni hiyo ya kichina na Rais wetu akaongea kwa mbwembe na kujiamini kuwa serikali yake itakuwa tayari kununua korosho yote iliyozalishwa nchini kwa shilingi 3,300 kwa kila kilo moja

Vile vile katika sakata hilo la korosho, halikuacha kula vichwa vya watu, akiwemo aliyekuwa Waziri wa kilimo, Charles Kizeba na Waziri wa Biashara Charles Mwijage

Sasa Taifa limepiga U turn kwa kurejea utaratibu uliokuwa ukitumika awali wa kuwaachia wafanyibiashara wa korosho wanunue korosho za wakulima

Tumejifunza nini katika sakata hilo la korosho??

Kama Taifa tumejifunza kuwa ubabe na maamuzi ya kukurupuka hayalisaidii Taifa hili na badala yake yanaliingizia Taifa hili hasara kubwa!
 
Tumemsikia Waziri wa kilimo, Mheshimiwa Jahet Hasunga, akiongea na waandishi wa habari, akielezea mpango "mpya" utakaotumika katika ununuzi wa zao la korosho, katika msimu ujao

Katika Maelezo yake amesema serikali itasimamia tu zoezi hilo, lakini haitajihusisha na ununuzi huo wa zao hilo la korosho kwa nchi nzima. Akaendelea kueleza kuwa wanunuzi watakuwa wafanyibiashara wa korosho na mtindo utakaotumika utakuwa ni wa wazi na wa kutumia zabuni.

Maelezo ya Waziri Hasunga ni tofauti kabisa na msimamo aliokuwa nao Rais Magufuli mwaka Jana.

Msimamo huo wa Rais kuihusisha serikali kununua korosho yote iliyozalishwa na wakulima, ndiyo iliyosababisha kilio kikubwa sana kwa wakulima wa korosho wa mikoa ya Kusini, ambao hawakulipwa na serikali hiyo pamoja na kutamba kufanya hivyo kwa mbwembwe nyingi.

Hata wabunge wa CCM wa kutoka mikoa hiyo ya Kusini walitishiwa kuvuliwa ubunge wao, iwapo wangeendelea kuwasemea wakulima wao wa korosho, kuwa serikali yetu imewadhulumu korosho Zao na hata Waziri Mkuu wetu, Kassim Majakiwa, akatishiwa kupigiwa shangazi zake, iwapo hizo "ngebe" zisingekoma!

Hivi nani hakuona "mbwembwe" za wanajeshi wetu kumiminika na malori yao huko Kusini mwa nchi yetu, walikoamriwa kwenda kwa ajili ya kwenda kusomba korosho hiyo na hata hao wqnajeshi wetu kuhakikishiwa kuwa wana uwezo wa kuzibangua korosho zote zilizovunwa??

Wanasiasa wengi na wananchi kwa ujumla wao walitahadharisha mno kuwa njia hiyo wanayoitumia viongozi wetu wa serikali ya awamu ya tano siyo sahihi

Tujikumbushe tena namna Waziri mkuu, Kassim Majakiwa "alivyoumbuliwa" na Rais Magufuli, pale aliposema kuwa ametafuta kampuni moja ya kichina, ambayo imekubali kununua korosho yetu yote na kuisafirisha

Jibu alilopewa Waziri mkuu, bado tunalikumbuka sisi sote, kwa kuambiwa kuwa aachane na kampuni hiyo ya kichina na Rais wetu akaongea kwa mbwembe na kujiamini kuwa serikali yake itakuwa tayari kununua korosho yote iliyozalishwa nchini kwa shilingi 3,300 kwa kila kilo moja

Vile vile katika sakata hilo la korosho, halikuacha kula vichwa vya watu, akiwemo aliyekuwa Waziri wa kilimo, Charles Kizeba na Waziri wa Biashara Charles Mwijage

Sasa Taifa limepiga U turn kwa kurejea utaratibu uliokuwa ukitumika awali wa kuwaachia wafanyibiashara wa korosho wanunue korosho za wakulima

Tumejifunza nini katika sakata hilo la korosho??

Kama Taifa tumejifunza kuwa ubabe na maamuzi ya kukurupuka hayalisaidii Taifa hili na badala yake yanaliingizia Taifa hili hasara kubwa sana!
Mpaka muhula huu uishe tutaona mengi. Yetu macho. No comment your honour.
 
Mpaka muhula huu uishe tutaona mengi. Yetu macho. No comment your honour.
Ubaya wa Tanzania ya Leo, mwananchi yeyote hatakiwi kukosoa mwenendo wa serikali, hata kama "imebugi" vipi......

Serikali hii haina tofauti ya simulizi ya yule mfalme aliyekuwa akitembea uchi hadharani, hadi pale yule mtoto mdogo aliposema, mbona Mfalme yuko uchi??

Akaonywa vikali na mama yake na kuambiwa kuwa hatutakiwi tuseme hivyo hata kama tunaona kwa macho wenyewe!
 
Kiþu unachoshindwa kuelewa ni kidogo sana.

Rais Magufuli kwanini aliamua Serikali inunue korosho mwaka jana?

Ukikielezea hicho utakuwa na jibu.

Jibu:
Serikali Ilitaka Kutumia Nguvu Kwenye Mambo Yanayo Hitaji Akili.
Bei Ya Biashara Yoyote Hujieleza Yenyewe kutokana Na Hali Ya Soko,Huwezi Kumlazimisha Mfanya Biashara Anunue Bidhaa Yako Kwa Bei Kubwa Wakati Sokoni Hiyo Bidhaa Imeshuka Bei.

Huu Ndio Msingi Wa Tatizo•
 
Madame Faiza hapa tunaongelea kuhusu ununuzi wa zao la korosho.......

Kama wewe unataka kuongelea kuhusu kuliwa kwa ruzuku ya Chadema, bora ungeifungulia topic yake......
Huuoni uhusiano uliopo kati ya korosho na ruzuku?

Zote ni siasa maji taka.
 
Jibu:
Serikali Ilitaka Kutumia Nguvu Kwenye Mambo Yanayo Hitaji Akili.
Bei Ya Biashara Yoyote Hujieleza Yenyewe kutokana Na Hali Ya Soko,Huwezi Kumlazimisha Mfanya Biashara Anunue Bidhaa Yako Kwa Bei Kubwa Wakati Sokoni Hiyo Bidhaa Imeshuka Bei.

Huu Ndio Msingi Wa Tatizo•
Huwezi pia kuuziwa kitu kwa bei uitakayo wewe tu. Hiyo ndiyo biashara.
 
Huwezi Kupanga Bei Wakati Unacho Kiuza Ni Malighafi Hebu Elewa Hilo.

Je! Baada Ya Wafanya Biashara Kuwaachia Korosho Zetu Ili Mnunue Wenyewe Na Kwenda Kuziuza Hivi Hilo Zoezi Limefanikiwa Kwa Ngapi %.
100%

Korosho zimenunuliwa na zimeshauzwa kwa bei nzuri, mengine ni changamoto tu za kubadilisha mfumo.

Wewe unauza au unanunua korosho?
 
Chelewa ufike, korosho yote imenunuliwa na imeanza kusafirishwa, wakulima wote watalipwa, japo wamecheleweshwa, lakini mwisho wa siku korosho yote imenunuliwa na wakulima wote watalipwa!, better late than never.
P.
Tatizo kubwa la wadanganyika ni ubinafsi na kutojali shida na mateso ya watu wengine mradi tu hayajakukuta au unatafuta uteuzi hivyo kila kitu unautetea hata kama hakifai,sio sahihi au ni cha hovyo!!

Wametia watu hasara na umasikini bila hata kuwalipa fidia kisa tu kusaka kiki za kisiasa alafu kwa ujinga wa watu kama wewe unatetea!!

Ingekuwa ni katika nchi za wenzetu(zenye binadamu halisi) hata mkulu angetakiwa kujiuzulu au Bunge lingemuwajibisha ila Bongo wajinga na wabinfsi wako busy kutetea kila kitu hata vile vya kijinga kisa tu kutaka uteuzi au kulinda vibarua vyao na masilahi yao mengine.

Tumekuwa Taifa la wabinfsi kupindukia!!

Mmmenda shule kupata makaratasi tu na si elimu!!
 
Tumemsikia Waziri wa kilimo, Mheshimiwa Jahet Hasunga, akiongea na waandishi wa habari, akielezea mpango "mpya" utakaotumika katika ununuzi wa zao la korosho, katika msimu ujao

Katika Maelezo yake amesema serikali itasimamia tu zoezi hilo, lakini haitajihusisha na ununuzi huo wa zao hilo la korosho kwa nchi nzima. Akaendelea kueleza kuwa wanunuzi watakuwa wafanyibiashara wa korosho na mtindo utakaotumika utakuwa ni wa wazi na wa kutumia zabuni.

Maelezo ya Waziri Hasunga ni tofauti kabisa na msimamo aliokuwa nao Rais Magufuli mwaka Jana.

Msimamo huo wa Rais kuihusisha serikali kununua korosho yote iliyozalishwa na wakulima, ndiyo iliyosababisha kilio kikubwa sana kwa wakulima wa korosho wa mikoa ya Kusini, ambao hawakulipwa na serikali hiyo pamoja na kutamba kufanya hivyo kwa mbwembwe nyingi.

Hata wabunge wa CCM wa kutoka mikoa hiyo ya Kusini walitishiwa kuvuliwa ubunge wao, iwapo wangeendelea kuwasemea wakulima wao wa korosho, kuwa serikali yetu imewadhulumu korosho Zao na hata Waziri Mkuu wetu, Kassim Majakiwa, akatishiwa kupigiwa shangazi zake, iwapo hizo "ngebe" zisingekoma!

Hivi nani hakuona "mbwembwe" za wanajeshi wetu kumiminika na malori yao huko Kusini mwa nchi yetu, walikoamriwa kwenda kwa ajili ya kwenda kusomba korosho hiyo na hata hao wqnajeshi wetu kuhakikishiwa kuwa wana uwezo wa kuzibangua korosho zote zilizovunwa??

Wanasiasa wengi na wananchi kwa ujumla wao walitahadharisha mno kuwa njia hiyo wanayoitumia viongozi wetu wa serikali ya awamu ya tano siyo sahihi

Tujikumbushe tena namna Waziri mkuu, Kassim Majakiwa "alivyoumbuliwa" na Rais Magufuli, pale aliposema kuwa ametafuta kampuni moja ya kichina, ambayo imekubali kununua korosho yetu yote na kuisafirisha

Jibu alilopewa Waziri mkuu, bado tunalikumbuka sisi sote, kwa kuambiwa kuwa aachane na kampuni hiyo ya kichina na Rais wetu akaongea kwa mbwembe na kujiamini kuwa serikali yake itakuwa tayari kununua korosho yote iliyozalishwa nchini kwa shilingi 3,300 kwa kila kilo moja

Vile vile katika sakata hilo la korosho, halikuacha kula vichwa vya watu, akiwemo aliyekuwa Waziri wa kilimo, Charles Kizeba na Waziri wa Biashara Charles Mwijage

Sasa Taifa limepiga U turn kwa kurejea utaratibu uliokuwa ukitumika awali wa kuwaachia wafanyibiashara wa korosho wanunue korosho za wakulima

Tumejifunza nini katika sakata hilo la korosho??

Kama Taifa tumejifunza kuwa ubabe na maamuzi ya kukurupuka hayalisaidii Taifa hili na badala yake yanaliingizia Taifa hili hasara kubwa!
Ya mwaka jana yalishapita. Acha kufukua Makaburi usije ingia mzima kaburini kabla ya wakati relax
 
100%

Korosho zimenunuliwa na zimeshauzwa kwa bei nzuri, mengine ni changamoto tu za kubadilisha mfumo.

Wewe unauza au unanunua korosho?
Mimi Ni Mkulima.



Kama Zoezi Limefanikiwa Kwa 100% Tena Kwa Kuuza Korosho Kwa Bei Kubwa Sasa Kwanini Serikali Isiendelee Kununua Korosho Ili Tuwabane Hawa Wafanya Biashara Wenye Lengo La Kutunyonya Wakulima?. Iweje Mpira Urudishwe Kwa Kipa (Wafanya Biasha)Wanunue Korosho Wakati Mwaka Jana Serikali Imetuambia Wafanya Biashara Wanatunyonya Wakulima Au Mwaka Huu Kuna Wafanya Biashara Tofauti Na Wamwaka Jana?.
 
Mimi Ni Mkulima.



Kama Zoezi Limefanikiwa Kwa 100% Tena Kwa Kuuza Korosho Kwa Bei Kubwa Sasa Kwanini Serikali Isiendelee Kununua Korosho Ili Tuwabane Hawa Wafanya Biashara Wenye Lengo La Kutunyonya Wakulima?. Iweze Mpira Urudishwe Kwa Kipa (Wafanya Biasha)Wanunue Korosho Wakati Mwaka Jana Serikali Umetuambia Wafanya Biashara Wanatunyonya Wakulima Au Mwaka Huu Kuna Wafanya Biashara Tofauti Na Wamwaka Jana?.
Hongera sana, kwa kumpa vidonge vyake huyo wa "praise team for Magufuli"
 
Back
Top Bottom