Je, nini kimepelekea wajasiriamali (wafanyabiashara) kuwa wengi nyakati hizi? Je, nyakati zijazo kutatokea nini kwenye hili kundi la watu?

Mohamedex121

JF-Expert Member
Jan 27, 2022
1,688
3,142
Habarini wakuu! Toka majuzi nimekuwa nikijiuliza maswali mengi hili suala la wajasiriamali kuwa wengi nyakati hizi tofauti na miaka ya zamani let say 90's.

Kipindi cha miaka ya 90's wajasiriamali na wafanyabishara walikuwa wachache sana, yaani kukuta duka la Mangi moja mtaa mzima au kijiji kizima ilikuwa ni kawaida sana. Mzee wangu anakumbuka nyakati hizo,, wateja walikuwa wanapanga foleni kwa wenye maduka, biashara zilikuwa chache, sijui hili inamaanisha nini au kipindi hicho watu walikuwa Bize na kulima? Ama walikuwa Bize na kusoma ili kuja kuajiriwa?

Katika miaka hiyo nahisi watu suala la biashara kipindi hicho haikuwa kipaumbele chao, watu walikuwa Bize na masuala ya elimu kusoma ili kuajiriwa serikalini ama sekta binafsi au pia inawezekana watu wengine walikuwa vijijini wako Bize na kilimo na pengine walishindwa kuja mjini na hivo kuliacha kundi la watu wachache kufanya biashara ama wengine huwa wajasiriamali hasa maeneo mbalimbali ya miji.

Miaka ya 90's hakukuwa na soko la kariakoo ilo mnaliona miaka hii karibuni, bali soko kubwa la jiji la Dar lilikuwepo posta na mnazi mmoja.

Sasa sijui nini kulipeleka kukuwa kwa masoko mengi ya wafanyabishara nyakati hizi ukianzia soko la kariakoo, tegeta, Manzese, Buguruni, Mbagala, ubungo (ilikuwa zamani), na hata hapa Mbezi mwisho nilipo, wajasiriamali tumejaa kila kona. Ukipita mitaa ya Mbagala kila nyumba inafremu la duka la Mangi na sio Mbagala tu hata huku mitaani maduka ni mengi. Mama ntilie ndio usiseme wemejaa kila kona, kuna wanauza chai na uji wakitembeza kwenye vijiwe na majumbani achilia mbali wale wamama wanaouza mihogo akitembea mtaa kwa mtaa, mama zangu wa mbogamboga wamejaa kila mahali.

Yaani siku hizi kila mtu ni mjasiriamali haijalishi huyu kuajiriwa ama hajaajiriwa , haijalishi huyu ni mtoto wa au ni mtu mzima yaanj naona madogo siku hizi nao wamo kwenye gemu ya ujasiriamali, achilia mbali wanasiasa, wazee , wamama nao siku wamechangamka tofauti na wamama wa miaka ya 90's waliokuwa wakishinda nyumbani, ila siku hizo wote tupo nao masokoni kila mtu ni mjasiriamali aliyesoma na asiyesoma wote tupo kwenye gemu la ujasiriamali yaani daah shiiiiidaaaa hili ni bomu soon nahisi litalipuka tu kama zilivyo kwenye ajira za wasomi.

Huwa najiuliza baada ya haya yote ya kila mtu kuwa mjasiriamali je nini kitatokea miaka ya baadaye je kutakuwa na mfumo mpya na option mpya za watu kufanya shughuli nyingine tofauti na ujasiri na kama zitakuwepo ni zipi hizo?? Watu watakuwa na mishe gani mbali na ujasiriamali?

#Natanguliza_shukurani_wakuu
 
Jibu sahihi ni kwamba miaka ile kulikuwa na mgawanyiko mzuri wa ajira kutokana na population pia idadi ya watu waliopo kwenye miji na wengine waliobaki waliridhika kufanya shughuli za kilimo vijijini/mashambani.

Hii ilifanya kuwe na wafanyabiashara wachache ambao walikuwa na moyo wa kuipenda biashara kutoka moyoni yaani hawakufanya biashara kwa sababu ya kukosa kazi ya kuajiriwa bali walizikataa kazi za kuajiriwa na kuithamini biashara/ujasiriamali.

Kwa miaka ya sasa kuna kundi kubwa la watu wanajiingiza kwenye ujasiriamali/biashara si kwa kupenda bali wanalazimisha kufanya kutokana na kukosa ajira hivyo na wanaingia kwenye biashara wakiamini hiyo ndio njia ya kujikwamua hata kama hawana kipaji au msukumo wa biashara.

Nina mifano mingi ya wazee wa zamani ambao walizikataa ajira wakajiingiza kwenye ujasiriamali na hawakuwa na hawakuwa na vyeti vya elimu.

Lakini sasa hivi kuna watu wengi wamesoma wana vyeti lakini kupata kazi ni kazi hapo ndipo wanapoanza kujiita wajasiriamali bila kupenda.
 
Mageuzi ya kiuchumi na kifikra! Wananchi wamegundua ajira ni utumwa bila kuwa na plan B maisha yatakuw na changamoto nyingi mbeleni
Watu washahama kwenye ajira wengi tumekuwa wajasiriamali. Je! Napo pia watu watahama kwenye huu ujasiriamali? Na kama wakihama watahamia kwenye shughuli gani?? Maana kila zama na nyakati zake.
 
Jibu sahihi ni kwamba miaka ile kulikuwa na mgawanyiko mzuri wa ajira kutokana na population pia idadi ya watu waliopo kwenye miji na wengine waliobaki waliridhika kufanya shughuli za kilimo vijijini/mashambani.

Hii ilifanya kuwe na wafanyabiashara wachache ambao walikuwa na moyo wa kuipenda biashara kutoka moyoni yaani hawakufanya biashara kwa sababu ya kukosa kazi ya kuajiriwa bali walizikataa kazi za kuajiriwa na kuithamini biashara/ujasiriamali.

Kwa miaka ya sasa kuna kundi kubwa la watu wanajiingiza kwenye ujasiriamali/biashara si kwa kupenda bali wanalazimisha kufanya kutokana na kukosa ajira hivyo na wanaingia kwenye biashara wakiamini hiyo ndio njia ya kujikwamua hata kama hawana kipaji au msukumo wa biashara.

Nina mifano mingi ya wazee wa zamani ambao walizikataa ajira wakajiingiza kwenye ujasiriamali na hawakuwa na hawakuwa na vyeti vya elimu.

Lakini sasa hivi kuna watu wengi wamesoma wana vyeti lakini kupata kazi ni kazi hapo ndipo wanapoanza kujiita wajasiriamali bila kupenda.
Na huu mwisho wa kila mtu kuwa mjasiriamali kama zilivyokuwa kwenye ajira ni lini? Je, watu watahamia kwenye shughuli gani? Maana kila chenye mwanzo kina mwisho. Unaweza kutufungua kidogo japo nasi tuondoke kwenye hili la wajasiriamali maana tumeshakuwa wengi ni bomu soon litalipuka.
 
Nafikiri ujasiliamali na Biashara kwa level zake zote ndo kikomo cha Ukuaji wa Uchumi wa Mataifa, Tutazidi tu kuexpand uzalishaji na Masoko ila Taifa litageuka la kibiashara kama Dubai. Hata kilimo na Ufugaji wa sasa umekaa kijasiliamali usisahau hivyo hivyo Elimu ya sasa au ijayo itawajenga watu Kujiajili kupitia Taaluma zao. Hii itaacha huduma za jamii zote mikononi mwa Raia wenyewe Serkali itabaki kutawala na Kuendesha shughuli zake zingine Nyeti.
 
Watu washahama kwenye ajira wengi tumekuwa wajasiriamali. Je! Napo pia watu watahama kwenye huu ujasiriamali? Na kama wakihama watahamia kwenye shughuli gani?? Maana kila zama na nyakati zake.
Sasa ndio mwanzo wa enzi za teknolojia,wajanja wachache washawahi huko,hapo baadae hayo unayoyaona aidha uwepo au usiwepo hutayaona watu watakuwa busy online tu,kwa wenzetu biashara nyingi kwa sasa ziko online na sisi ndio tunaelekea huko.

Zamani ilikuwa vishoka wanashinda tu pale posta na mtaa wa mkwepu kazi Yao kubwa ni kubrush viatu vya watu wanaofanya kazi maofisi ya serikali na sekta binafsi,huku wakiwasaidia shuguli ndogo ndogo kama kuwafatia chakula na vinywaji kwenye migahawa,kulipia bili za maji, kulipia bili za umeme,kulipia ada za shule,kulipia Kodi za ardhi, kulipia Kodi za magari wakati wa road license, kufanya transfer za magari,kuchakata document mbalimbali kama kupata passport na mihuri muhimu.

Ila ilipokuja technology kwanza M-Pesa tu kwa mfano ikaja ikaondoa baadhi ya hizo mishemishe,ikaja technology ya control number ndio kabisa,mambo mengi yakakata, technology ya Instagram na whatsapp nayo ikaja kuleta kazi ingine ya delivery sasa watu siku hizi wanauza chakula na bidhaa zingine online tu, bill za umeme tunanua tu unit kwa njia ya simu,mambo mengi kwa sasa tunafanya kwa njia ya simu Kodi na Tozo nyingi za serikali mpaka ada za mashule tunafanya kwa njia ya simu, tunalipa bill za maji kwa njia ya simu tu.Vibali vingi siku hizi tunavipata online kama mfano export permit, import permit,tunalipa ushuru online yaani mambo mengi sana online.

Zamani Matangazo kulikuwa na Yale magari yanapita mitaani yanatangaza na mziki juu makelele siku hizi jambo lolote linatangazwa online kwenye social media.

Zamani asubuhi asubuhi tu watu wamejazana kwa wauza magazeti siku hizi hata sura ya gazeti mtu pengine hajui Tena kwa sababu habari zote anazipata kiganjani kwake.

Vijana siku hizi wanafanya Hadi biashara ya digital asset online tu na wanaingiza pesa ndefu. Sio miaka mingi kuanzia sasa watu wengi shughuli zao zitahamia majumbani Kwao huku platform kubwa za wateja itakuwa online tu.

Na hii itawaweka wengi sana juu ya mawe kama unaweza kuona mbali kwa jicho la tatu ndio wakati muafaka sasa kuanza kuwekeza kwenye ardhi haswahaswa huko mikoani,pamoja na mambo yote haya yatakayotokea hapo baadae asset muhimu sana ukitoa pesa itakuwa ardhi.

Kwa maana kwenye ardhi itakuwa rahisi kuwa na dhamana na uhakika wa chakula mbali na mambo mengineyo.
 
Nafikiri ujasiliamali na Biashara kwa level zake zote ndo kikomo cha Ukuaji wa Uchumi wa Mataifa, Tutazidi tu kuexpand uzalishaji na Masoko ila Taifa litageuka la kibiashara kama Dubai. Hata kilimo na Ufugaji wa sasa umekaa kijasiliamali usisahau hivyo hivyo Elimu ya sasa au ijayo itawajenga watu Kujiajili kupitia Taaluma zao. Hii itaacha huduma za jamii zote mikononi mwa Raia wenyewe Serkali itabaki kutawala na Kuendesha shughuli zake zingine Nyeti.
Na soko la ushindani litakuwa kubwa, pengine wauzaji wa bidhaa tutakuwa wengi kuliko wanunuzi (wateja). Nadhani unafahamu athari za kuwa na competition kwenye biashara wenye nguvu za hela watabaki kubwa juu huku wajasiriamali wadogowadogo wakibaki kubwa masikini.

Na endapo nchi ikaexpand kibiashara na kuifikia dubai pangine nchi zingine tunazolingana nazo kiuchumi zitafika level hio, hofu yangu ni kubwa kuhusu international trade inamaana kutakuwa na ushindani kibiashara baina nchi na nchi na mwishowe kuleta vita vya kiuchumi na solution sijui itakuwa ni nini je watu watahama kwenye huo mfumo wa biashara na ujasiriamali?? Na kama wakihama watahamia kwenye shughuli gani?? Maana naona technolojia kila inazidi kukua na sijui tunakoelekea hasa kwenye la ujasiriamali.
 
Sasa ndio mwanzo wa enzi za teknolojia,wajanja wachache washawahi huko,hapo baadae hayo unayoyaona aidha uwepo au usiwepo hutayaona watu watakuwa busy online tu,kwa wenzetu biashara nyingi kwa sasa ziko online na sisi ndio tunaelekea huko.
Zamani ilikuwa vishoka wanashinda tu pale posta na mtaa wa mkwepu kazi Yao kubwa ni kubrush viatu vya watu wanaofanya kazi maofisi ya serikali na sekta binafsi,huku wakiwasaidia shuguli ndogo ndogo kama kuwafatia chakula na vinywaji kwenye migahawa,kulipia bili za maji,kulipia bili za umeme,kulipia ada za shule,kulipia Kodi za ardhi,kulipia Kodi za magari wakati wa road license,kufanya transfer za magari,kuchakata document mbalimbali kama kupata passport na mihuri muhimu.Ila ilipokuja technology kwanza M-Pesa tu kwa mfano ikaja ikaondoa baadhi ya hizo mishemishe,ikaja technology ya control number ndio kabisa,mambo mengi yakakata, technology ya Instagram na whatsapp nayo ikaja kuleta kazi ingine ya delivery sasa watu siku hizi wanauza chakula na bidhaa zingine online tu,bill za umeme tunanua tu unit kwa njia ya simu,mambo mengi kwa sasa tunafanya kwa njia ya simu Kodi na Tozo nyingi za serikali mpaka ada za mashule tunafanya kwa njia ya simu,tunalipa bill za maji kwa njia ya simu tu.Vibali vingi siku hizi tunavipata online kama mfano export permit, import permit,tunalipa ushuru online yaani mambo mengi sana online.
Zamani Matangazo kulikuwa na Yale magari yanapita mitaani yanatangaza na mziki juu makelele siku hizi jambo lolote linatangazwa online kwenye social media.
Zamani asubuhi asubuhi tu watu wamejazana kwa wauza magazeti siku hizi hata sura ya gazeti mtu pengine hajui Tena kwa sababu habari zote anazipata kiganjani kwake.
Vijana siku hizi wanafanya Hadi biashara ya digital asset online tu na wanaingiza pesa ndefu.
Sio miaka mingi kuanzia sasa watu wengi shughuli zao zitahamia majumbani Kwao huku platform kubwa za wateja itakuwa online tu.
Na hii itawaweka wengi sana juu ya mawe kama unaweza kuona mbali kwa jicho la tatu ndio wakati muafaka sasa kuanza kuwekeza kwenye ardhi haswahaswa huko mikoani,pamoja na mambo yote haya yatakayotokea hapo baadae asset muhimu sana ukitoa pesa itakuwa ardhi.
Kwa maana kwenye ardhi itakuwa rahisi kuwa na dhamana na uhakika wa chakula mbali na mambo mengineyo.
Hakika nimekupata vyema. Kweli naona baadhi ya nchi zilizoendelea wengi wamehamisha shughuli zao majumbani na sio kwenye masoko na stendi za magari kama tunavyofanya huku kwetu.

Umenena vyema bro ngoja nasi tujaribu kuhamia huko , umetufungua akili
 
Na huu mwisho wa kila mtu kuwa mjasiriamali kama zilivyokuwa kwenye ajira ni lini?? Je watu watahamia kwenye shughuli gani??? Maana kila chenye mwanzo kina mwisho. Unaweza kutufungua kidogo japo nasi tuondoke kwenye hili la wajasiriamali maana tumeshakuwa wengi ni bomu soon litalipuka
Biashara au ujasiriamali ni asili ya mwanadamu haiwezi kuisha ila staili na mbinu ndio zinabadilika. Zamani ilikuwa ukihitaji kununua mchele au vyombo kama sufuria,sahani n.k ilikuwa lazima ukapange foleni kwenye duka la Mangi lakini leo hii una uwezo wa kuagiza kwa simu yako ukiwa kitandani na unaletewa hadi mlangoni.
 
Hii ni kweli lakini huu mrundikano wa wajasiriamali umekithiri zaidi hapa jijini Dar es salaam, huko mikoani utakuta bado hakujachanganya kihivyo.

Ila hii ya Dar kufulikia inachangiwa na mengi, ikiwemo kurahisishwa kwa njia za uchukuzi, hivyo imeweza kumfanya hata mtu anayeishi nje ya mji kuwa na biashara zake mjini huku akiishi nje ya mji au mkoa jirani.

Hapo nisikwambie wingi wa wakazi ambao nao wameamka sasa kuanza kufanya biashara, plus wale wanaotoka mikoani kuja Dar kwa lengo la kuanza maisha.

Hivyo kuna haja ya mamlaka kuongeza juhudi katika kuongeza mizunguko ya pesa mikoani pia ili kupunguza hii mirundikani ya wajasiriamali katika huu mji.
 
Biashara au ujasiriamali ni asili ya mwanadamu haiwezi kuisha ila staili na mbinu ndio zinabadilika.
Zamani ilikuwa ukihitaji kununua mchele au vyombo kama sufuria,sahani n.k ilikuwa lazima ukapange foleni kwenye duka la Mangi lakini leo hii una uwezo wa kuagiza kwa simu yako ukiwa kitandani na unaletewa hadi mlangoni.
Usiseme ni asili ya Mwanadamu,, watu walikuwa na shughuli za kufanya kabla ya kuja kwa mfumo wa biashara, ukirudi kwenye hostori kabla ya barter trade system watu walikuwa na shughuli nyingi za kufanya.

Ingekuwa ujasiriamali ni asili ya mwanadamu pengine barter trade ingeanza pindi tu binadamu wanapoumbwa
 
Back
Top Bottom