Je, nikawashitaki au nikubali yaishe?

Je, nikawashitaki au nikubali yaishe?

Wananchi unaosema wapo karibia 700 ndo hao watakaompigia kura diwani,inasaidia nini hata umpe gari ya kampeni diwani na kuwa mpambe wakati anaweza kukosa hata kura zao kwa ajili yako.

Watu 700 haiwezekani wote wawe na wivu na wewe kuna kitu hujaweka sawa
 
Achana na hizo pombe.
Watakufunza discipline sasa hivi.
 
mhhh uko na shida, halafu una ka uhaya fulani
Uhayani ni kwa wajomba ,shida Sina Ila wewe ndiye una shida na Mimi Sasa makabila ya watu kuyataja ili iweje ?

By the way ni vibaya kusema uhalisia wangu kuwa kielimu Mimi si haba ?

Njoo PM nikutumie CV yangu uhakiki nisemacho
 
Wananchi unaosema wapo karibia 700 ndo hao watakaompigia kura diwani,inasaidia nini hata umpe gari ya kampeni diwani na kuwa mpambe wakati anaweza kukosa hata kura zao kwa ajili yako.

Watu 700 haiwezekani wote wawe na wivu na wewe kuna kitu hujaweka sawa
Waliosema ujinga ni wanakijiji wawili tu ,kwa pale walioshangilia tuhuma zangu kusemwa ni Kama Mia mbili Sasa hapo utasema hawanipendi kweli Kaka ?
 
Ujue umekaa kipombe pombe,
Na wanakumulika, halafu hata mke huna, upo tu kama mhuni
Dada sio hivyo ,nilioa miaka ya nyuma kidogo na alhamdulilah mwanamke walipata kumuona pamoja na wanangu wawili.

Dada sababu za kihisia kwa wifi yako nilipatwa na kesi nikawekwa ndani nimekaa hapo Keko magereza kwa muda wa mwaka na miezi kadhaa .

Nilipotoka rasmi nikapewa talaka na mke wangu mzuri ,nilikuwa na vimali vya urithi hapa Dar es salaam kutoka kwa baba pamoja na baadhi ya vitu katika mkoa huu ,ikabidi vigawanwe .

Dada kidogo nikapewa Mimi ,kikubwa akapewa yeye kwakuwa yupo na watoto ,bad enough siku si nyingi baada ya hayo akadai hata watoto si wangu .

Nikajipigiliza kwa watoto kila Mara nionanane nao walau wajue Mimi ni baba yao ,dada watoto wakaanza nao kunikataa kwa kusema wao mbona wanajua Mimi si baba yao wanaye baba mwingine .

Dada ,wifi yako kaolewa Sasa na aliyemuoa ndiye anasema ni baba wa wanaye .

Uhuni wangu uko wapi hapo ? Natamani kuoa Ila nitamuoa Nani ilihali bado nampenda mke wangu sijaamini kuwa ameniacha naamini labda atarudi panapo majaaliwa .

Dada siishi kihuni ,ninazo heshima zangu na ninayo mipaka yangu na wanakijiji Ila ni vile dunia inaamua kunihukumu kwa mfumo huu .
 
Back
Top Bottom