Je, nikawashitaki au nikubali yaishe?

Je, nikawashitaki au nikubali yaishe?

MENEMENE TEKERI NA PERESI

JF-Expert Member
Joined
Mar 11, 2022
Posts
9,316
Reaction score
25,443
Salamu sio makusudio ya mada yangu pendwa.

Ndugu zanguni, Mimi naishi kijijini Sana na Mimi ni mtumishi wa serikali ngazi niliobarikiwa ambayo ninyi haiwahusu na siwezi kuwaambia ng'o.

Sasa Jana mtendaji wa kata yetu ambaye ni rafiki yangu na pia Mimi ndiye mshauri wake mkuu ,alinieleza kuwa kutakuwa na kikao siku ya leo na Mimi anaomba nihidhurie bila kukosa ,Sasa kwasababu Mimi ndiye mshauri mkuu.

Nilipatwa na fadhaa iweje aweke kikao bila kuniuliza walau nimpe ushauri basi nikamezea Ila nikamuhoji kikao hiki Cha Kijiji kinahusu nini akawa anang'ata maneno.

Sasa leo asubuhi mida ya saa mbili kikao kimekaliwa.

Wananchi wananisema Mimi kuwa huduma ninayotoa natoa nikiwa nimelewa hivyo hawana Imani na Mimi ,Sasa kwa ushamba wao eti wananishitaki kwa diwani kuwa aniondoe hapa kwenye kata yao 😭

Sasa kichekesho ni kuwa Mimi sipo chini ya diwani na Wala hawezi kunipanga Jambo lolote kuhusu kazi zangu ,alafu diwani mwenyewe Mimi ndiye mshauri wake mkuu juu ya masuala ya kampeni na pia ameomba nimuazime Corolla yangu kampeni zikianza ili azunguke vijiji vyote vya kata kupiga kampeni na Mimi ndiye mpambe wake mkuu hivyo kwa hili ni sawa na kusema mbuzi kafia kwa muuza bucha.

Ila sasa nipende kudeclare interest zangu kuwa ni kweli pombe nakunywa Ila sio muda wa kazi, Mimi nakunywa kuanzia saa tisa na pombe sinywi za kizungu tena maana hela Sina, Mimi nakunywa ulanzi hivyo kwa kunisema mbele ya watu Mia Saba na ushee nimeona ni Kama wamenidharau na kuniabisha nawaza niwashitaki au nikubali waning'atue.

Nasema nikubali waning'atue maana hawa wanakijiji wanakuwaga na namba za mpaka watu wa mkoani na wilayani hata wizarani maana wakija uwa wanajipendekeza ili waanze kututisha tukizingua.

Ndugu zangu wa damu wanajamiiforums hilo la pombe limeniuma Sana Ila sanjari na hilo Jambo lilioninyima amani mpaka nikaamua nijifiche kwenye hiki chumba Cha mikutano ili nitoe ya moyoni ni habari ya mwananchi mmoja kuthubutu kusema niliachwa na mke wangu sababu ya umalaya ilihali si kweli na pia akamalizia kuwa wake zao wako matatani maana napenda kutongoza wake zao.

Ndugu zanguni Mimi kwanza natoka Dar es salaam kwenye kila aina ya wanawake waliojaaliwa na kila kitu, hivi kweli nianze kutongoza tuwanawake twa huku? Kwanza ni tweusi, tumekondeana na zaidi hawana sifa nizitakazo (hasa ukubwa wa mpini) kwa maneno hayo huyu mwananchi naye kaiharibu asubuhi yangu na kuniboa Sana.

Nisiwchoshe nilitaka tushauriane Jambo maana kwanza niliwaza nifungue jalada hapa kwenye kata baadaye twende mahakamani ili wathibitishe waliyonituhumu nayo au wanilipe wakishindwa Ila kingine nikawaza labda nikubali waning'oe niende kwingine japo hapa niahaweka mizizi yangu kutoka kizembe ni kuhatarisha uchumi wangu.

Lakini la mwisho na linalonizunguka kichwani ni kuwa kwakuwa wasemaji wa huo upuuzi wote nimewaona basi niwape kipondo either kwa kutuma vijana wenye nguvu wawakung'ute alafu Mimi nisubirie hatma yangu.

Naomba ushauri wenu, niko vibaya najihisi hasira na aibu Sana hasa ukizingatia hapa job sinaga time na washikaji wamefurahi Sana maana nawaona wakiniangalia wanatamani kucheka Ila wanajizuia na Mimi Sina time nao.

Karibu ndugu zangu mwenzenu siko sawa leo.

=====

Suluhisho limepatikana, ahsanteni kwa ushauri.

Ukijikuta limbeya limbeya basi scroll kushuka chini kujua nini kilijiri hususani kwa ambao hamkujua mwenzenu nilikumbwa na nini.

Mchana mwema.
 
Hao wanakijiji wanajua namna ya kukushughulikia kuliko vile unavyofikiria.

Yaani unaamini diwani atasimama na wewe kisa corola wakati wapiga kura wamemtuma kazi ya kukutoa 😂

Ila kama upo local government jua huyo diwani akikusagia kunguni kwenye council unatolewa hapo Zahanati mapema sana ndugu mfamasia.

Jua ni miongoni kwa displinary authority kwako ndugu mtumishi.
 
Hao wanakijiji wanajua namna ya kukushughulikia kuliko vile unavyofikiria.

Yaani unaamini diwani atasimama na wewe kisa corola wakati wapiga kura wamemtuma kazi ya kukutoa 😂

Ila kama upo local government jua huyo diwani akikusagia kunguni kwenye council unatolewa hapo Zahanati mapema sana ndugu mfamasia.

Jua ni miongoni kwa displinary authority kwako ndugu mtumishi.
Sipo local government Ila najua mpaka inafika huko ni kuwa diwani na mtendaji ni wanafiki Sana maana wameruhusu vipi mikutano wa Mimi kuchambwa na wao ni marafiki zangu na haya waliyajua ?

Aisee nitaondoka na kichwa Cha mtu ,kwa upuuzi huu ikiwa sitatolewa hapa naapa ifikapo 2025 simpi Corolla yangu abadani
 
Kaongeze elimu mkuu. Uondokane na io adha koz kata zote zipo ivo ivo ma diwani wanafki kinouma na wenyeviti wao
 
Hao wanakijiji wanajua namna ya kukushughulikia kuliko vile unavyofikiria.

Yaani unaamini diwani atasimama na wewe kisa corola wakati wapiga kura wamemtuma kazi ya kukutoa 😂

Ila kama upo local government jua huyo diwani akikusagia kunguni kwenye council unatolewa hapo Zahanati mapema sana ndugu mfamasia.

Jua ni miongoni kwa displinary authority kwako ndugu mtumishi.
Atakua police kata mkuu haswa haswa ndio watu huonana sana mfamasia ni mara chache na siasa pia sio rahisi
 
Sipo local government Ila najua mpaka inafika huko ni kuwa diwani na mtendaji ni wanafiki Sana maana wameruhusu vipi mikutano wa Mimi kuchambwa na wao ni marafiki zangu na haya waliyajua ?

Aisee nitaondoka na kichwa Cha mtu ,kwa upuuzi huu ikiwa sitatolewa hapa naapa ifikapo 2025 simpi Corolla yangu abadani
Tulia na utulize akili.Usipotulia yale yote yaliyosemwa yatadhaniwa kuwa ni kweli.Kubali kubadilika.
 
Kaongeze elimu mkuu. Uondokane na io adha koz kata zote zipo ivo ivo ma diwani wanafki kinouma na wenyeviti wao
Kaka kuhusu elimu Mimi si haba ndugu ,isitoshe nishafanya kazi kwenye taasisi nyingi za serikali mpaka vyombo vya usalama japo nilitimuliwa Ila sio kwa huu mfumo wa Mimi kuchambwa mbele ya wanakijiji ambao hata ningeamua kuwajibu kwa kingereza hayupo hata mmoja angenielewa .

Mimi kusoma tena siwezi Kaka ,akili ilishakubali elimu nimimaliza kwangu mimi
 
Ila sasa nipende kudeclare interest zangu kuwa ni kweli pombe nakunywa Ila sio muda wa kazi
Basi, Nimepata jibu. Wewe sio mlevi bali ni mnywaji tena nje ya muda wa kazi. Wana lao jambo Kuwa nao karibu, Wapo waungwana wanao kukubali na kukuelewa watakueleza nini hasa kinachopelekea hayo yote.
 
Kaka kuhusu elimu Mimi si haba ndugu ,isitoshe nishafanya kazi kwenye taasisi nyingi za serikali mpaka vyombo vya usalama japo nilitimuliwa Ila sio kwa huu mfumo wa Mimi kuchambwa mbele ya wanakijiji ambao hata ningeamua kuwajibu kwa kingereza hayupo hata mmoja angenielewa .

Mimi kusoma tena siwezi Kaka ,akili ilishakubali elimu nimimaliza kwangu mimi
mhhh uko na shida, halafu una ka uhaya fulani
 
Back
Top Bottom