Je, ni sawa mwanaume kumfulia nguo mwanamke?

Je, ni sawa mwanaume kumfulia nguo mwanamke?

Frankton

Member
Joined
Jun 2, 2012
Posts
33
Reaction score
6
Katika pita pita zangu nkakutana na mwanaume anafua nguo za kike, hata nilipojaribu kusogeza karibu mboni za macho yangu ili kushuhudia kitendo hiki jamaa alichokuwa anakifanya, ndipo macho yetu yalipokutana na kumuona jamaa akijiskia aibu na kuanza kuangalia chini, naam hali hii ilinifanya nijiulize je haya ni mapenzi au adhabu.

Tujadili hili wakuu
 
Mkuu achana na haya mambo. Nyumba zina mambo mengi. Ina maana wewe huwezi mfulia mkeo nguo?
Yawezekana anaumwa

Au yawezekana huyo mwanaume yupo kazini yaani DOBI
Conclusion it depends on the situation. ( Mimi huwa nikiwa naumwa au kipibdi mjamzito au nimejifungua huwa ananifulia)
 
Kuna shida gani kuchukua na kuzitupa kwenye washing machine unabonyeza dakika unaziacha kwa muda kisha dili kwisha..mbona ni kitu kawaida kwa haya maisha ya Dot.com?

Swissme
 
Acha ushamba wako: dunia ya leo unajiuliza ni sawa fulani kumfanyia fulani? Ishi na tembelea jamii mbalimbali utajua ni sawa. Tena bila hata ya kuumwa mwanaume anafua kwa roho nyeupe it al depends na amezoaje alivyokuwa na amekuwa exposed kiasi gani na anafanya kwa nia gani . Period
 
Kuna shida gani kuchukua na kuzitupa kwenye washing machine unabonyeza dakika unaziacha kwa muda kisha dili kwisha..mbona ni kitu kawaida kwa haya maisha ya Dot.com?

Swissme

Sio kila mtu ana hiyo washing machine_hoja hapa ni je..ni halali kumfulia mwanamke nguo..?
Jibu la Igwe ni...sio halali ila ni kawaida.
 
Labda huyo mwanaume ni houseboy analipwa kufanya kazi hiyo, lakini kama ni suala la mahusiano ya kimapenzi hii haijakaa poa kabisa...

Nakupa hongera kwa kujitambua mkuu,watu wengi wanaolalamika kuchapiwa na kusumbuliwa na wanawake ni wale wasiojitambua kwa kuhalalisha huu ujinga wa kuwanyenyekea na kupoteza mamlaka ya asili_nafikiri ni kujaribu kukwepa majukumu yao ya msingi ndio mwanzo wa kukumpromaizi kwa kila kitu.
 
Explain

swissme.

Wewe unaona ni sawa sawa kuwa na mwanaume anayekufulia nguo!?, utakua ni mwanamke wa ajabu sana kutaka kuwa na mwanaume inferior, imagine mwanaume wako mtaani wanamuita Bushoke sababu ya kukufulia nguo utakua unajisikiaje!?
 
Kwa mahubiri ya jana ya mzee wa upako nilitegemea mada kama hii JF, hakuna ubaya wowote alimradi anafanya hivyo kwa moyo wa upendo na si kulazimishwa.

Yeah..hapo kidogo nakubaliana na wewe,...ila wanaume wengi wanaofanya hivyo wana kila dalili za umario.
 
Kuna shida gani kuchukua na kuzitupa kwenye washing machine unabonyeza dakika unaziacha kwa muda kisha dili kwisha..mbona ni kitu kawaida kwa haya maisha ya Dot.com?

Swissme

Kwanini usiziweke mwenyewe kwenye hayo madude yenu ya dot com?
 
wewe unaona ni sawa sawa kuwa na mwanaume anayekufulia nguo!!??, utakua ni mwanamke wa ajabu sana kutaka kuwa na mwanaume inferior, imagine mwanaume wako mtaani wanamuita Bushoke sababu ya kukufulia nguo utakua unajisikiaje!!??

Bado naona uko njema so far.Watu inabidi tuelewe na tuwe na mipaka ya hii kitu inayoitwa ku-care.
 
ni sawa tu, ingekuwa si sawa basi madobi wa kiume wangefua za kiume tu, kwa kuwa hakuna madhara yoyote kwamba ukifua utabadilika jinsia mie naona haina tatizo.
 
Hii ni moja ya sababu wanaume wanawaogopa wanawake wenye 'status', wanaume tunapenda kua superior na ndo maana wengi wanaishia kuoa walioishia la pili.
 
Kwanini usiziweke mwenyewe kwenye hayo madude yenu ya dot com?
I don't know how to explain to you by the way. Unaweza lakini sio kwa kulazimishwa my be she's doing something else or she's sick just like that.but not by force

swissme
 
Nakupa hongera kwa kujitambua mkuu,watu wengi wanaolalamika kuchapiwa na kusumbuliwa na wanawake ni wale wasiojitambua kwa kuhalalisha huu ujinga wa kuwanyenyekea na kupoteza mamlaka ya asili_nafikiri ni kujaribu kukwepa majukumu yao ya msingi ndio mwanzo wa kukumpromaizi kwa kila kitu.

Yaani hizi fikra za dot.com zinawafanya baadhi ya wanawake kukwepa majukumu yao, eti anafurahia mwanaume kumfulia nguo anasahau kuwa na yeye pia anajidhalilisha kwa kuwa na mwanaume anayeonekana kituko mbele ya jamii kwa maana hayo sio mapenzi bali ni ubwege wa hali ya juu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom