Je, ni nani ana tabia kama zangu?

Je, ni nani ana tabia kama zangu?

Utakuwa na matatizo ya akili tafuta daktari wa magonjwa ya akili...sio kwa ubaya lakini sijakuita chizi..matatizo ya akili ni mengi lako pia ni tatizo waone wataalam wakufanyie therapy
Aje atibiwe bure
 
Hello.

Ni nani aliye na Hizi tabia .

1. Nachelewa sana kulala hadi nagombana na mke wangu.

2. Mvivu kupokea simu ,ninaweza kuiona itaita ila nitakupigia au kukutumia sms tu.

3. Ninafanya jambo ninapojisikia Tu,mfano mtu anaweza kunitumia sms kesho nitaiibu muda wowote ninaoutaka mimi hata nikiblue tick.

4. Nakaribia miaka 30 ila sina rafiki yeyote niliyeanza nae tuseme sekondari au chuo wote nimejikuta nawapotezee mara baada ya kuona wao wamenipita mafanikio sijisikii kuendelea kumake bond nao.

5. Niko karibu na watu mbalimbali ila wao uanza kufanikiwa mapema kabla ya mie iwe biashara ,kazi mpaka nahisi nimerogwa.

6. Ni mtu nisiyejali kumtafuta mtu kwa simu labda hadi tatizo hasa msiba ila sina mazoea ya kuwasialiana na watu kwa simu au njia yeyote.

7. Siko Romantic hata mke wangu anaumia Juu ya hilo.

8. Kitu kidogo nawaza mpaka naumwa kichwa nikikosa jibu kama niko free ninaweza kulala kutwa nzima au simu tu.

9. Ni mtu wasiwasi na Muda wote nimekuwa nikiwaza kufakufa tu.

10. Sina interest na mapenzi japo nina mke.
Bro acha kupiga punyeto. Hayo yote yataisha. Ukiendelea, soon macho yataanza kupoteza uwezo wa kuona..
 
Mpaka umesema tayari ni hatua ya kwanza kukubali una tatizo.
Acha nikupe some tips zinaweza kukusaidia.

TENGENEZA PICHA KUBWA YA MAISHA YAKO, YAPE MAISHA YAKO PURPOSE,usiiishi tu kwa kuwa unapumua
Jiulize wewe ni nani na unataka kuwa nani baada ya muda gani!
Unajiona wapi baada ya miaka 5, hakikisha unavunja vunja hiyo miaka mitano kuanzia minne kushuka chini mpka hapo ulipo leo.
kisha utaona unapaswa kufanya nini ili ufike pale.

NI KWELI JITIHADA HAISHINDI KUDRA, ila OGOPA SANA KUPATWA NA KUDRA BILA KUWA NA JITIHADA WALA MIPANGO.

Af u need People!
Wewe sio kisiwa , hata kisiwa kinakaa karibu na maji!
Watu wanatutoa, watu wanatupa deals, watu wnatusikiliza, watu wanatupenda, watu wanatufariji.

Sio Ujanja hata kidogo kuwa bila watu!
Your network is your networth.
Usingizi sana au kukosa usingizi kabisa ni dalili Ya kukata tamaa na maisha!

Sio swala la kuwa romantic, we hata mwenyewe hujipendi utawezaje kuonesha mapenzi?

Af acha kutizama mafanikio yako ukijilinganisha na mafaniko ya wengine
HII ITAKUCHELEWESHA SANA!
Wewe pambana na wewe mwenyewe!
Kabla ya kutizama mwingine kafaulu wapi,we jitizame ndani yako unafanya nini kizuri!
Kisha jiboreshe ZAIDI!
Si rahisi kufanya kila kitu vizuri, chagua maeneo ya kuwa best at!
Miaka 30 bado sana kukata tamaa na maisha!

So yes kuna eneo unatakiwa ulifanyie kazi pia practically!

UTARATIBU WAKO WA SIKU/WIKI/MWEZI
FUNGU LA KWANZA (UTARATIBU WAKO KWA SIKU)
1. Ikifika saa tatu , Zima simu ingia kitandani jilazimishe kulala
2. Kula chakula mapema, kabla ya kulala kunywa maji
3. Asubuhi amka mapema hata kama huendi kazini, kunywa maji ya vuguvugu, fanya mazoezi hata dk 10
4. Andika malengo ya siku hiyo, hakikisha unayapa time frame na unajikagua iwapo umetimiza
5. rudia namba tip namba 1-4 kila siku

FUNGU LA PILI (UTARATIBU WAKO WA WIKI)
Kila Jumatatu Weka malengo ya wiki nzima, yakague kila jumapili
Ona wapi umefaniukisha/umekwama, nani amekukwamisha, nani angeweza kukusaidia (Utaona gap yako)
Malengo ya wiki inayofuata ni kuunga pale uliona gap hasa ya watu kupitia mawasiliano.

FUNGU LA PILI (MWEZI )
Weka malengo tar 01 jikague tar 31.
Ninaposema malengo usiwaze sijui kujenga nyumba sijui kununua gari , Malengo makubwa sana ni mazuri lakini yanakatisha moyo na tujione hakuna tunachofanya

Kuna mengi ya kukusaidia, ILA HEM FANYA HAYA KWANZA !
af uje ulete feedback baada ya siku 90.
Ukifanikiwa tu hii umetoboa
 
Mm pia naugonjwa wa jamaa na hii tiba niliambiwa mahali hakutaja tu valium
Huo ugonjwa ni effect za blue light .....

Then zinasababisha ubongo kupoteza majira yaani mfumo wa muda wa ubongo kitaalam unaitwa Circadian rhythm...au Circadian brain clock.... baada ya mfumo huu kuharibika huwa ni mgumu sana kuurudisha kama ni chronic yaani umeathirka sana yaani unakuwa uko kwenye group la chronic insomania(ugonjwa wa kutopata usingiizi sugu)


Ukiwa chronic insomania ndo unapata madhara hayo aliyoaandika huyo jamaa yote inshort unakuwa depressed yaani depression itokanayo na bluelight iliyoleta chronic insomania


Dawa yake huwa light therapy ..... au melatonin supplements bongo hazipo hizi.....au magnesium glycinate nayo bongo ngumu kupatikana..... unabaki na solution hatari valium aka diazepam... hii ukizengua unakuwa teja so tumia kwa umakini mkubwa
 
wao uanza kufanikiwa mapema kabla ya mie iwe biashara ,kazi mpaka nahisi nimerogwa.
Haujarogwa bali ni hizo tabia zako ndizo zinazokurusisha nyuma....Hakuna mtu anayeweza kumpa dili mtu ambaye anajibu meseji atakpojisikia.
 
Japo umetaka kujua nani yuko kama wewe lakini kabla ya kukujibu ngoja tukupe ushauri wa hayo matatizo yako [maana hayo ni matatizo wala siyo sifa nzuri]

Kwanza hoja yako namba moja tu hiyo huenda ikawa ndo sababu. Je unachelewa ukifanya nini? Jilazimishe ulale mapema walau siku 40 mfululizo

Tukiendelea kwenye namba nne hapo napo kuna tatizo, haiwezekani ujikate na marafiki kwa makusudi tu. Ikiwa marafiki wanakatika kibahati mbaya tu kwa sababu zisizozuilika sawa lakini kama unao karibu au wanakupigia pigia ni muhimu na wewe utoe mrejesho

Kitu muhimu zaidi angalia rafiki mmoja ambaye unahisi anafaa sana halafu shirikiana naye sana huyo atakuwa ni kiungo kikubwa sana kwenye mambo yanayokusibu

Wanasema kuwa wenye matatizo au waliowahi kupatwa na matatizo fulani wanakuwa na ushauri mzuri sana (nasaha) juu matatizo kama hayo yanapompata mwingine.

Kipindi nasoma hayo matatizo yako ilibidi nirudi juu kuhakiki isije ikawa ni mimi niliandika humu bila ya kujua! Yaani yote hayo ni kama mimi kabisa ila hilo la marafiki lilikuja kuniokoa.

Nilipotezea marafiki wote lakini kuna rafiki zangu wa college na rafiki zangu wa kazini hao wamekuwa nguzo muhimu katika kunitoa kutoka katika upweke huo.

Nakumbuka mmoja nilimwambia "ujue mimi sina rafiki wa kudumu ila huwa inategemea kwa muda maalumu nipo kwenye jambo gani na marafiki husika lakini tukimaliza jambo hilo basi urafiki unakoma kwahiyo hata wewe tukiachana hapa nikawa kwingine huko urafiki utakoma!"

Jamaa akanicheki akaishia kuniambia "usiseme hivyo aisee maisha haya hayatabiriki". Kweli yule jamaa akawa karibu na mimi sana mpaka leo ni zaidi ya ndugu kiasi kwamba nikaona kama ameamua kunifunza kwa vitendo zaidi juu ya kile nilichomwambia.

Nikuase, jiweke karibu na Mwenyezi Mungu [maana umetaja gospel hapo chini kwahiyo naassume wewe ni muumini wa kikristu] kwani kujiweka karibu na Mola wako kutarudisha yote hayo yanayohitajika uwe nayo.

Kwa mfano ukiamua kushikamana na dini utaswali, utatoa swadaka, utatembelea wagonjwa, utahubiria wengine neno la Mola, utajali majirani, ndugu na marafiki, utaheshimu watu, mamlaka, na utatii wazazi, utamjali mkeo, utaepuka kupuuza watu kama unavyopuuza sasa simu na kadhalika...

Yote haya yanapatikana kwenye dini kupitia mafundisho mbalimbali na mahubiri ya viongozi kwahiyo ukishikamana na kuyatekeleza utakuta unatoka taratibu au hata haraka sana kwenye matatizo yako

Nakumbuka nilikuwa nikiwa na hali ngumu kiuchumi najifungia nawaza wee mpaka nasinzia nalala nikiamka angalau kichwa kimepoa. Muda mwingine washikaji walikuwa wanaambiana huenda navuta bangi maana sina stori wala sina muda na mtu.

Hali kama hiyo ukiiruhusu sana shetani naye anapata nafasi ya kupenyeza agenda zake mara unashawishika uanze kulewa pombe, bangi au dawa nyingine za kulevya, mara unaanza kujikweza unajiona una akili sana ndomaana huchanganani/ hutangamani na watu, mara unajiona huna thamani kabisa kwenye dunia ni bora ufe! Mara unaanza kuchallenge maumbile (naturals) matokeo yake unageuka akina Kiranga kuona hakuna Mungu!

Kwa sisi waislamu ukiwa unawaza kufa kila mara ni jambo jema sana wala siyo kosa lakini je unafanya nini baada ya kuwaza sana kufa? Ndipo hoja ya msingi ilipo hapo

Siku njema!
 
Madr wenyewe wana shida ya akili
Ni jambo la kawaida hauko peke yako kanye west pia anamatatizo ya akili tafuta tiba itakucost ndugu..wengi tunamatatozo ya akili ila yanapishana lako ni kubwa tafuta ufumbuzi
 
Shida yako ni moja tu "unahitaji kipato cha kuelewela" ukipata hayo mengine yataondoka yenyewe

Hapo kuna tabia mie huwa zinakuja nikiwa sina kabisa hela especially hiyo kutopokea simu, utapiga naangalia tu
 
Back
Top Bottom