mzee, huko ilembula njombe hawaishi wahehe, wanaishi wabena. wahehe waliokuwa wanakula mbwa ilikuwa zamani sana, inawezekana hata wewe ulikuwa haujazaliwa. na maeneo waliyokuwa wanakula mbwan i maeneo ya uhehe halisi (Wahehe wanatofautiana, wale wa mkwawa na wahehe wa dabaga). wale wa dabaga wanaitwa wa milimani hao hawana historia ya kula mbwa na hata lugha kidogo wanatofautiana na wahehe wa Tanangozi, isimani, kalenga hadi mafinga. ukiangalia utakuta Dabaga ina chakula kingi sana, matunda mengi sana na ukijani mbichi lakini huku tanangozi ilula hadi mafinga kuna ukame fulani uliowafanya hawa wahehe halisi kula hadi mbwa kwasababu hakukuwa na wanyama wengine na chakula ni scarce sana hadi leo. ukipita hata leo mimawe tu imejaa kwenye milima hakuna ardhi nzuri. ila ukienda dabaga kuna vyakula na wanyama wa pori wapo na wanafuga ng'ombe. Tanangozi walikuwa wanakula mbwa, ifunda, mafinga, kalenga ,isimani etc.
kaka yangu ameoa mtu wa asili ya dabaga na tulishaenda kutoa mahari huko na ninakufahamu sana. wahehe wa dabaga na wahehe wa kalenga (mkwawaz) ni tofauti na hao tu ndio waliopigana vita enzi zile, hao wa milimani wanaitwa wadzungwa na hawana historia yeyote ya kula mbwa au kupigana vita. hivyo kwa uzoefu nilionao naweza kusema wahehe halisi wale wa kwenye vitabu wa kalenga, ifunda, mafinga, ilula, isimani, isimila etc walikuwa wanakula mbwa kweli lakini ni zamani, kizazi cha sasa hakuna hata mbwa anayeweza kuliwa. vilevile ni utani tu wa makabila, mhehe hata kama amezaliwa mwanza na hajawahi kufika iringa ukimwuliza kuwa unakula mbwa atakwambia ndio kwa utani tu lakini uhalisia sio kweli kwasasa, zamani walikula sawa.