Mfilisti
JF-Expert Member
- Sep 24, 2015
- 3,727
- 19,465
Ni jambo la kusikitisha kuona jinsi wagombea wa nafasi za juu katika siasa za leo wanavyonyamazishwa au kwa Maksudi kabida kutoonyesha msimamo dhahiri kuhusu mapambano dhidi ya ufisadi na utawala mbovu. Hoja hii muhimu inapuuzwa, hakuna Mgombea yoyote mwenye kuonyesha hatua atakazo fanya kupambana na majizi na mafisadi na wananchi tunabaki na wasiwasi kuhusu hatma ya mustakabali wa taifa letu.
Tukirudi nyuma Kampein za uchaguzi mkuu 2010 Chama cha CHADEMA kilionyesha dhamira kuu ya kupambana na Mafisadi mara watakapoingia madarakani. Japo walishindwa kuendeleza ajenda hii pale 2015.
2015 tuna kumbukumbu za kampeni za marehemu Rais John Magufuli, aliyeonyesha dhamira ya kweli ya kupambana na ufisadi kwa kuanzisha Mahakama ya Mafisadi / kuimarisha utawala bora na nidhamu ya kazi. Ilikuwa ni hatua ya kihistoria, ikionyesha kuwa serikali inaweza kuchukua hatua madhubuti dhidi ya tatizo hili. Hata hivyo, utekelezaji wa ahadi hizo umeonekana kusuasua na kushuka kasi mara alipoingia madarakani na hata baada ya kifo chake.
Kwa sasa, taifa letu linaonekana kupotea polepole kutokana na ukosefu wa viongozi wenye hofu ya kweli na hasira inayostahili dhidi ya ufisadi na utawala mbovu sio watawala CCM au vyama vya Upinzani. Wote wanaimba nyimbo zao wanazojua wenyewe, najiuliza Taifa linakwenda wapi?
Tunahitaji viongozi wapya wenye dhamira thabiti na ujasiri wa kuendeleza mapambano dhidi ya ufisadi na utawala mbovu sio hawa wachumia matumbo yao na Makundi yao yanayowaweka madarakani. Viongozi wa mfano, wasioogopa kuwajibika, wanaoweza kuleta mabadiliko halisi yanayolenga kuinua taifa letu na kuimarisha imani ya wananchi.
Tukirudi nyuma Kampein za uchaguzi mkuu 2010 Chama cha CHADEMA kilionyesha dhamira kuu ya kupambana na Mafisadi mara watakapoingia madarakani. Japo walishindwa kuendeleza ajenda hii pale 2015.
2015 tuna kumbukumbu za kampeni za marehemu Rais John Magufuli, aliyeonyesha dhamira ya kweli ya kupambana na ufisadi kwa kuanzisha Mahakama ya Mafisadi / kuimarisha utawala bora na nidhamu ya kazi. Ilikuwa ni hatua ya kihistoria, ikionyesha kuwa serikali inaweza kuchukua hatua madhubuti dhidi ya tatizo hili. Hata hivyo, utekelezaji wa ahadi hizo umeonekana kusuasua na kushuka kasi mara alipoingia madarakani na hata baada ya kifo chake.
Kwa sasa, taifa letu linaonekana kupotea polepole kutokana na ukosefu wa viongozi wenye hofu ya kweli na hasira inayostahili dhidi ya ufisadi na utawala mbovu sio watawala CCM au vyama vya Upinzani. Wote wanaimba nyimbo zao wanazojua wenyewe, najiuliza Taifa linakwenda wapi?
Tunahitaji viongozi wapya wenye dhamira thabiti na ujasiri wa kuendeleza mapambano dhidi ya ufisadi na utawala mbovu sio hawa wachumia matumbo yao na Makundi yao yanayowaweka madarakani. Viongozi wa mfano, wasioogopa kuwajibika, wanaoweza kuleta mabadiliko halisi yanayolenga kuinua taifa letu na kuimarisha imani ya wananchi.