Je, ni kweli Michael Jackson alikuwa analala kwenye chemba maalumu ili aishi milele?

Scars

JF-Expert Member
Apr 8, 2017
44,384
105,226
Hii haiwezi kuwa habari mpya sana kwa wengi wetu humu.

Makala nyingi zimeandika habari hiyo kuwa ni kweli. Lakini mimi naijumuisha katika moja ya conspiracy theories. Ni kawaida sana kwa mtu mashuhuri kuwekewa habari nyingi za uongo kwa media ili ku catch attention ya watu.

Kumbuka 27 Januari 1984 Michael Jackson akiwa jukwaani akifanya show kwa ajili ya tangazo la Pepsi, aki-perfom nyimbo yake maarufu ya Billie Jean

Kulikuwa kuna zile pipe za kutolea moto kwa ajili ya manjonjo ya show (pyro effects) zilikuwa jirani na usawa wa kichwa chake wakati anacheza.

Moto ulidaka nywele zake, nayeye aliendelea kucheza akiwa hatambui kuwa nywele zimeshika moto. Washirika aliokuwa nao kwenye kikosi cha kuchukua hiyo filamu ya hilo tangazo ndio waliomvuta kumtoa kwenye moto. Lakini wakati huo tayari madhara ya moto yalikwisha fanyika.

Aliugulia majeraha ya moto kwa kiwango kilichohatarisha kupoteza hadi uhai wake. Kufuatia ajali hiyo, Pepsi ilimlipa mamilioni ya dola za kimarekani kama fidia, ambapo kwenye hizo pesa alijitolea kujenga clinic kwa ajili ya kusaidia kutibu wahanga wa moto.

Katika kujenga hiyo clinic Michael Jackson alinunua vifaa vya kisasa kwa ajili ya kurudisha hali ya ngozi iliyoharibiwa na majeraha ya moto. Moja ya kifaa hicho ilikuwa ni hyperbaric oxygen chamber.

Tazama picha hapa chini.

1681932502615.png


Hicho ni kifaa ambacho kinamuwezesha muhanga wa moto kuweza kupokea hewa nzuri ya oxygen iliyochujwa pamoja na kumuongeza mtiririko mzuri wa damu. Hutumika kurejesha ngozi ambayo imehathiriwa na majeraha ya moto.

Sasa Michael Jackson alipoinunua kwa ajili ya Clinic yake, wakati wa uzinduzi aliamua kujaribu mwenyewe kisha kuruhusu watu wapige picha akiwa ndani ya hiyo chemba.


1681932761455.png



1681933013155.png

Baada ya hapo ndio wale haters wa "Wape picha stori watatunga wao," wakaanza kuzusha propaganda kuwa analala humo ili kufanya aishi miaka mingi. Mara Michael Jackson anaogopa uzee hivyo analala kwenye chemba ili kuepuka asizeeke.

Wakati hiyo chemba yenyewe hutakiwi kulala zaidi ya masaa mawili kwasababu inaweza kusababisha upoteze maisha.

********************†***************
Nawasalimu kwa jina la Hip Hop.
 
Bro hiyo machine ipo. But haifanyi uishi milele but inafanya usizeeke haraka ,ipo Kama Tan Bed...umri unasogea but ngozi yako inachelewa
 
Bro hiyo machine ipo. But haifanyi uishi milele but inafanya usizeeke haraka ,ipo Kama Tan Bed...umri unasogea but ngozi yako inachelewa
Kama ipo basi sio hiyo ambayo nimeielezea hapo.

Ambayo ndio alikuwa amelala Michael Jackson
 
Umesema ukweli mtupu hakuna ulichokosea,
Hiyo siku alikua anazindua akaona atoe mfano basi ikawa nongwa na kuzusha mengi tu,

Aendelee kupumzika kwa Amani, alituburudisha japo Dunia haikumtendea haki akaishi kwa mateso badala ya furaha aliyostahili.
 
Ningeweza kuishi milele ,ningebakia mstari wa mbele,nawapa hoja zenye uzima watu wanasisimka mpaka nywele,omba pepo siyo unaomba uzima wa milele,duniani nimeona mengi lakini jicho halijafika kilele,siwaahidi kuishi miaka 100 kama alivyoahidi hayati Nyerere.
 
Hii haiwezi kuwa habari mpya sana kwa wengi wetu humu.

Makala nyingi zimeandika habari hiyo kuwa ni kweli. Lakini mimi naijumuisha katika moja ya conspiracy theories. Ni kawaida sana kwa mtu mashuhuri kuwekewa habari nyingi za uongo kwa media ili ku catch attention ya watu.

Kumbuka 27 Januari 1984 Michael Jackson akiwa jukwaani akifanya show kwa ajili ya tangazo la Pepsi, aki-perfom nyimbo yake maarufu ya Billie Jean

Kulikuwa kuna zile pipe za kutolea moto kwa ajili ya manjonjo ya show (pyro effects) zilikuwa jirani na usawa wa kichwa chake wakati anacheza.

Moto ulidaka nywele zake, nayeye aliendelea kucheza akiwa hatambui kuwa nywele zimeshika moto. Washirika aliokuwa nao kwenye kikosi cha kuchukua hiyo filamu ya hilo tangazo ndio waliomvuta kumtoa kwenye moto. Lakini wakati huo tayari madhara ya moto yalikwisha fanyika.

Aliugulia majeraha ya moto kwa kiwango kilichohatarisha kupoteza hadi uhai wake. Kufuatia ajali hiyo, Pepsi ilimlipa mamilioni ya dola za kimarekani kama fidia, ambapo kwenye hizo pesa alijitolea kujenga clinic kwa ajili ya kusaidia kutibu wahanga wa moto.

Katika kujenga hiyo clinic Michael Jackson alinunua vifaa vya kisasa kwa ajili ya kurudisha hali ya ngozi iliyoharibiwa na majeraha ya moto. Moja ya kifaa hicho ilikuwa ni hyperbaric oxygen chamber.

Tazama picha hapa chini.

View attachment 2593415

Hicho ni kifaa ambacho kinamuwezesha muhanga wa moto kuweza kupokea hewa nzuri ya oxygen iliyochujwa pamoja na kumuongeza mtiririko mzuri wa damu. Hutumika kurejesha ngozi ambayo imehathiriwa na majeraha ya moto.

Sasa Michael Jackson alipoinunua kwa ajili ya Clinic yake, wakati wa uzinduzi aliamua kujaribu mwenyewe kisha kuruhusu watu wapige picha akiwa ndani ya hiyo chemba.


View attachment 2593417


View attachment 2593420
Baada ya hapo ndio wale haters wa "Wape picha stori watatunga wao," wakaanza kuzusha propaganda kuwa analala humo ili kufanya aishi miaka mingi. Mara Michael Jackson anaogopa uzee hivyo analala kwenye chemba ili kuepuka asizeeke.

Wakati hiyo chemba yenyewe hutakiwi kulala zaidi ya masaa mawili kwasababu inaweza kusababisha upoteze maisha.

********************†***************
Nawasalimu kwa jina la Hip Hop.
Ukiachana na mashudu unayotoa kuhusu makolo, membo mengine unaongea ya maana.
 
Back
Top Bottom