Je, ni Car Security Systems ipi ni bora na ya kisasa?

Mkuu Juakali jr , inasemekana kuwa hizo car alarms ukiweka sumaku juu ya boneti, alarm kimyaa!! Hili lina ukweli?
Hii pia tuwasubiri wajuzi zaidi.
Ila kwa nadharia sioni ukweli wake maana alarm system sio lazima iwekwe kwenye bonet, inaweza ukainstall chini ya kiti cha nyuma na waya zake zikaenda sehemu husika.
Ila kuna wajamaa kariakoo niliona wanafungua bonet ya gari lenye alarm kwa kutumia waya, wanaupitisha chini kwenye bamper la mbele. kuna sehemu kwenye lock huo waya ukifika wakivuta bonet linafunguka.
Then wanatoa battery then ndo unakua mwisho wa alarm maana inatumia umeme kutoka kwenye battery
 

Umesomeka mkuu
 

Shukrani kiongozi
 
AUTO WATCH car security system, hii ipoje? na bei yake?
 
AUTO WATCH car security system, hii ipoje? na bei yake?

Autowatch ni mmoja kati ya makers wa security alarms kama vile toyota alivyo mmoja wa makers wa magari.
Ukifuatilia zaidi utaona kuna models mbalimbali za autowatch na zinatofautiana features
 

Lakini pia kuchora vioo, taa na side mirror kwa namba za gari au jina! Husaidia wezi kuachana navyo pindi wanapokuta namba!!
 
Autowatch ni mmoja kati ya makers wa security alarms kama vile toyota alivyo mmoja wa makers wa magari.
Ukifuatilia zaidi utaona kuna models mbalimbali za autowatch na zinatofautiana features

Ahsante sana mkuu. Ngoja nifuatilie hao Auto Watch.
 
Lakini pia kuchora vioo, taa na side mirror kwa namba za gari au jina! Husaidia wezi kuachana navyo pindi wanapokuta namba!!
Hapa naomba niongezee kidogo.
kwenye uchoraji na rivet(ribit) kwa mtu ambaye anafanya mara ya kwanza kuwa makini sana sababu unaweza ukatajiwa hela kwa kioo/pini ukaona ndogo ila mwishowe ukajikuta umetoa mpunga wa kutosha.
Usikubali waanze mpaka ujue jumla itakugharimu kiasi gani
 

Wanakuwa na usanii wa kubambikia bei?
 
Lakini pia kuchora vioo, taa na side mirror kwa namba za gari au jina! Husaidia wezi kuachana navyo pindi wanapokuta namba!!

Hivi ile huwa wanachora kwa mkono? ama kuna mashine maalum?
 
Lakini pia kuchora vioo, taa na side mirror kwa namba za gari au jina! Husaidia wezi kuachana navyo pindi wanapokuta namba!!

Hivi ile huwa wanachora kwa mkono? ama kuna mashine maalum?
 
Kama umewahi kuwa na Mkebe( Mathematical sets) kuna kiplastic fulani kina herufin A-Z na namba 0 -9 na bijitu vingine.

Hiyo na bikali hutumika kuandikia namba

Okay. Ahsante mkuu kwa kunifahamisha
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…