Je ndoa ya serikali inatambulika Kimungu

Je ndoa ya serikali inatambulika Kimungu

mbiza

JF-Expert Member
Joined
Feb 8, 2014
Posts
539
Reaction score
147
Natumai mtakuwa mpo na afya tele wanammu.

Swali langu nitakalo kuuliza ni je ndoa ya serikali inatambulika kimungu hasa kwenye ukristo?

Na je kama wanandoa waliofunga ndoa ya serikali halafu ni wakristo wakiachana inaruhusiwa kuoa au kuolewa tena,

asanteni
 
Kikristo, mwanaume akilala na mwanamke wameunganishwa kwenye ndoa (Ambayo si takatifu) since Mungu hakushirikishwa. Consummation of marriage is the real marriage kwa sababu hata mkila viapo kanisani consummation isipotokea hiyo si ndoa.

Sasa basi kwa sababu Mungu alisema tiini mamlaka. Ndoa ikifungwa serikalini ni ndoa halali (japo si takatifu since Mungu hakushirikishwa). Hata kama viongozi wa dini hawajaikubali.
Kama unamwogopa Mungu ni ndoa. Kama unawaogopa viongozi wa dini (honestly sijui huwa wanaichukuliaje), ila aliyeshiba neno anajua ni ndoa. Vigezo na masharti ya ndoa za kikristo kuzingatiwa! Yani kama ya kanisani vile.
 
Mungu wa wapi?Ya Kaisari mpe Kaisari, na ya Mungu mpe Mungu.
 
Kwani serikali inaamini Mungu? maana haina dini isipokuwa watu wake ndo wanadini
 
inatambulika! sasa si bora hyo kuliko ile ya zile dini za tumpapase bwana? unapiga kiroba halaf unazama ndani ukiwa mtupu khaaa
 
Kikristo, mwanaume akilala na mwanamke wameunganishwa kwenye ndoa (Ambayo si takatifu) since Mungu hakushirikishwa. Consummation of marriage is the real marriage kwa sababu hata mkila viapo kanisani consummation isipotokea hiyo si ndoa.

Sasa basi kwa sababu Mungu alisema tiini mamlaka. Ndoa ikifungwa serikalini ni ndoa halali (japo si takatifu since Mungu hakushirikishwa). Hata kama viongozi wa dini hawajaikubali.
Kama unamwogopa Mungu ni ndoa. Kama unawaogopa viongozi wa dini (honestly sijui huwa wanaichukuliaje), ila aliyeshiba neno anajua ni ndoa. Vigezo na masharti ya ndoa za kikristo kuzingatiwa! Yani kama ya kanisani vile.

Naunga mkono hoja hii,inatambulika, kwa nyongeza kama mlifunga ndoa ya serikali mnaenda kanisani mnaombewa ili

kuiweka ndoa yenu mikononi mwa Mungu, na kumbuka cheti cha ndoa ni kimoja na hutolewa na serikali,kwenye cheti

tu pale aliyefungisha anaonyesha ni ndoa ya aina gani imefungwa.
 
Serikali haina dini

Sasa hyo ndoa inakuwaje?
 
kwa wakristo inatambulika kwa mungu wao kwani mungu wao alishawaambia wayatii mamlaka yaliyopo duniani
 
Mungu alisema kuwa mwanamke na mwanaume wataishi pamoja hakusema waoane kanisan au msikitin, je ikiwa wamependana watu wa dini tofaut itakuwaje? cha msingi ni mapenz ya watu wawili na wazazi wa pande zote 2 wakubaliane
note:kazi ya mch/padre/sheikh si kufungisha ndoa bali ni kuthibitisha agano la watu wawili, kwa sisi wakristo tunasema," mimi..ninakubali kumuoa/olewa na..hata kifo kitakapotutenganisha." Kama sipo sawa prove me wrong
 
Tatizo watu hawajui maana ya ndoa.
Ukifanya tendo la ndoa ndiyo ndoa ni kukutana kimwili kati ya mtu me na mtu ke..ni tofauti ma mkataba..mkataba wa ndoa na ndoa ni vitu tofauti. Mkataba ukitolewa kanisani na kwa mwanasheria ni sawa tu kuhalalisha ndoa na si kwamba hiyo ndiyo ndoa.

Fanyeni tendo la ndoa mkielewa vitu..msikurupukie vitu vinavyowazidi umri.
 
Ndoa ni mpango wa mungu kakini ametoa mamlaka ya kufunga na kusimamia sheria ya ndoa.

Dini ni mawakala tu wa serekali katika kufunga ndoa ndio maana zile hati (cheti cha ndoa) za ndoa zinatoka serekalini na imeandikwa Jamuhuri ya muungano wa tanzania hati ya ndoa.

Ndoa iwe imefungwa kanisani au,bomani zote zina hadhi sawa na zinatambulika kisheria.
 
Jamani nielimisheni ndoa ya serikali ndio ndoa gani ? 👰
 
Mungu alisema kuwa mwanamke na mwanaume wataishi pamoja hakusema waoane kanisan au msikitin, je ikiwa wamependana watu wa dini tofaut itakuwaje? cha msingi ni mapenz ya watu wawili na wazazi wa pande zote 2 wakubaliane
note:kazi ya mch/padre/sheikh si kufungisha ndoa bali ni kuthibitisha agano la watu wawili, kwa sisi wakristo tunasema," mimi..ninakubali kumuoa/olewa na..hata kifo kitakapotutenganisha." Kama sipo sawa prove me wrong

mafundisho na masharti ya ndoa za kikisto yanakinzana na uhalisia wa maisha ya binadamu. NB: ndoa ya serikali hakubaliki katka uislam na sio mafundisho ya uislam.
 
Mungu anaitambua ndoa iliyotoka mikononi mwake kwa ajili ya kusudi lake jema kwa maisha ya wawili hao,nyingine mbwembwe tu! "Bwana asipoujenga mji waujengao wafanya kazi bure!"
 
Back
Top Bottom