Saguda47
JF-Expert Member
- May 1, 2016
- 10,777
- 18,656
Nafsi ni utambuzi wa uwepo unaoundwa na muunganiko wa mwili ( physical body/ flesh) na roho ( spirit), ili nafsi iwepo lazima mwili( passive component) uungane na roho ( active component) ambazo kwa pamoja huunda nafsi hai inayojitambua ( conscious ),
Ni vema tukafahamu kuwa nafsi ni muundo tegemezi ambao hauwezi kujitokeza peke yake bila miundo mingine yaani mwili na roho.
Nafsi hutengeneza kujifahamu na kujitofautisha (ID), pia nafsi ndio mhimili wa utambuzi ( conscious).
Je, NAFSI HUENDA WAPI BAADA YA KIFO?
Ni Mara nyingi watu hujiuliza swali hili kwa kurejea kitendo cha kufa, ni vema tufakafahamu kwanza KUFA ni nini hasa? jibu; kufa/ kifo ni hali inayojitokeza katika mwili ( any living organism ) ambapo shughuli na mifumo yote ya kibaiolojia hukoma kufanya kazi zake na kuwa tuli ( passive system).
ni dhahiri kwa tafsiri hiyo kuwa iwapo roho ( activating factor) itaacha/ kustisha kuuhudumia mwili ( passive component), kitendo hiki husababisha NAFSI kupotea na kutokuwepo tena, ni upotoshaji mkubwa ambao hufanywa na wengi kwa kujua au kutokujua kuhubiri na kufundisha kuwa ati baada ya kifo Nafsi huenda mahala Fulani.
Nafsi ni kama moto ulivyo, ili moto uwake lazima kuwepo na vitu / mada au dutu zinazosapoti moto uwake na moto huu hupotea Mara tu baada ya dutu hizi kuisha au kuvurugwa ( mfano kuzimwa).
Kwa mfano moto huenda wapi baada ya kuzima mshumaa au kibatari? je, moto huu huenda kutunzwa mahala ili baadae urudi tena? jibu ni SIYO.
Ndivyo hivyo hata kwa wanadamu tukifa nafsi zetu hupotea na kusahaulika kwa mauti.
Hata maandiko yanasema "..kila NAFSI itaonja MAUTI..."
sote ( utambuzi wetu utapotea na kusahaulika katika ulimwengu wa mwili)
By Emmanuel Mohammed
Philosophy & geography
Ni vema tukafahamu kuwa nafsi ni muundo tegemezi ambao hauwezi kujitokeza peke yake bila miundo mingine yaani mwili na roho.
Nafsi hutengeneza kujifahamu na kujitofautisha (ID), pia nafsi ndio mhimili wa utambuzi ( conscious).
Je, NAFSI HUENDA WAPI BAADA YA KIFO?
Ni Mara nyingi watu hujiuliza swali hili kwa kurejea kitendo cha kufa, ni vema tufakafahamu kwanza KUFA ni nini hasa? jibu; kufa/ kifo ni hali inayojitokeza katika mwili ( any living organism ) ambapo shughuli na mifumo yote ya kibaiolojia hukoma kufanya kazi zake na kuwa tuli ( passive system).
ni dhahiri kwa tafsiri hiyo kuwa iwapo roho ( activating factor) itaacha/ kustisha kuuhudumia mwili ( passive component), kitendo hiki husababisha NAFSI kupotea na kutokuwepo tena, ni upotoshaji mkubwa ambao hufanywa na wengi kwa kujua au kutokujua kuhubiri na kufundisha kuwa ati baada ya kifo Nafsi huenda mahala Fulani.
Nafsi ni kama moto ulivyo, ili moto uwake lazima kuwepo na vitu / mada au dutu zinazosapoti moto uwake na moto huu hupotea Mara tu baada ya dutu hizi kuisha au kuvurugwa ( mfano kuzimwa).
Kwa mfano moto huenda wapi baada ya kuzima mshumaa au kibatari? je, moto huu huenda kutunzwa mahala ili baadae urudi tena? jibu ni SIYO.
Ndivyo hivyo hata kwa wanadamu tukifa nafsi zetu hupotea na kusahaulika kwa mauti.
Hata maandiko yanasema "..kila NAFSI itaonja MAUTI..."
sote ( utambuzi wetu utapotea na kusahaulika katika ulimwengu wa mwili)
By Emmanuel Mohammed
Philosophy & geography