Roho, Nafsi na Mwili ni nini?

Roho, Nafsi na Mwili ni nini?

Thad

JF-Expert Member
Joined
Mar 14, 2017
Posts
13,402
Reaction score
31,658
Wasalaam wanaJF wenzangu!

Wakuu naomba kufahamishwa maana ya roho, nafsi na mwili.

Asante
 
Nafsi ni kanuni inayojenga mwili. Nafsi ni roho inayojidhihirisha kupitia mwili.
 
1.Mwili Ni Nyumba ya roho

2.Roho Ni nishati inayoipa nguvu mwili,

3.Nafsi Ni kiunganishi Cha roho na mwili.
Mtu akifa, roho na nafsi vinaenda wapi?
 
Wasalaam wanaJF wenzangu!

Wakuu naomba kufahamishwa maana ya roho, nafsi na mwili.

Asante
Watu wengi bado hawaelewi kuwa tafsiri sahihi ya neno "Nafsi" ni "uwepo wa/presence of" na hawaelewi kuwa mwanadamu/binadamu anazo nafsi tatu ambazo ni:- (1)nafsi mwili,(2)nafsi akili na hisia,(3) nafsi roho. Hivyo ni kusema binadamu ni mwili,hisia/akili na roho. Uwepo wa vitu hivi vitatu ndivyo vinavyotengeza uwepo wa Mtu! Mtu anapokufa uwepo wake kimwili, kihisia/akili huondoka ila kiroho huendelea kuishi( wanaita mizimu).

Mmesikia Wakristo wakisema wanaamini Mungu mmoja katika nafsi tatu( utatu mtakatifu) yaani Mungu baba, Mungu mwana na Mungu roho Mtakatifu na Kila nafsi Ina kazi yake ndivyo ambayo hata binadamu/Mtu ameumbwa katika nafsi/uwepo wa utatu mtakatifu yaani Mtu mwili,Mtu akili/hisia na Mtu Roho. Na hii ni kwasababu binadamu/Mtu ameumbwa Kwa mfano wa Mungu kwa ufanano wa idadi ya nafsi ili kuonesha ushirika katika utimilifu.
Somo hili ni pana sana na linahitaji utulivu wa Nafsi(mwili,roho na akili/hisia kulielewa)
 
Mwili, moyo, pumzi na ubongo tu Ayo mengine ni uongo mtupu hakuna roho wala nafsi
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom