Mbaya zaidi kuna mchizi kafa kaadhibiwa kwajili ya wanadamu. wao wanaamini hivyo alafu cha ajabu bado wanaenda kuabudu wakati tayari wamekombolewa.
Umetenda kosa, mzazi wako amekuja kukuwekea dhamani ili uwe huru.
Hiyo inatokea katika maisha yetu ya kawaida duniani.
Utamshukuru sana huyo mzazi wako, siyo?
Vilevile kuhusu mambo ya mbinguni, Kristu ametuwekea dhamana kwa kufa kwa niaba yetu.
Mimi nikila bangi naiona Pepo yangu karibu Sana.
Kumbe zile stori kwamba mnaona hadi mashimo njiani, ni za kweli? Bange mbaya sana!
Je, anaona matatizo ya watu lakini hatatui?
Basi ni aidha hana uwezo, hana upendo, au vyote
Kwa nini unasema hatatui matatizo ya wanadamu?
Dhana yako kuhusu Mungu kutatua matatizo ya wanadamu ikoje?
Eti anakupa chaguo, anajua mpaka utakachochagua lasivyo siyo mjuzi wa vyote
Mungu hayupo ni hadithi hizo tulitunga zamani kipindi hatuelewi dunia
Je, unaweza kuthibitisha hii hoja yako?
Kwa sababu matukio yaliyoandikwa kwenye Biblia ni visa halisi vilivyotokea katika historia.
mantiki ya Mungu kuweza kila kitu nakuumba kila kitu inaleta mkanganyiko sana tena sana!...
Mkanganyiko wa kimantiki hauondoi ukweli wa jambo fulani.
Hapo ni wazi tatizo siyo jambo lenyewe, bali shida iko katika mafikara ya mtu mwenyewe.
Haya ni mambo mawili tofauti.
Lakini ukifikiria kwa kina, utagundua kwamba hakuna mkanganyiko wowote kuhusu dhana juu ya uwepo wa Mungu.
wanasema Yeye ndio chanzo cha kila kitu na hapohapo wanamsema Shetani ndiye chanzo cha mabaya!!..
so sifa ya ubaya Shetani aliitoa kwanani ikiwa Mungu ndie chanzo cha kila kitu..?
kama ubaya haukutoka kwa Mungu basi Mungu sie chanzo cha kila kitu
Mungu ni chanzo cha kila kitu kwa maana kwamba vitu vyote vilitoka katika mikono Yake vikiwa vikamilifu 100%!
Shetani alikuwa Lusifa, kerubi mtakatifu asiye na harufu yoyote ya uovu ndani yake.
Uovu ulianzia moyoni mwake Lusifa mwenyewe.
Hii inamaanisha kuumbwa na Mungu hakuondoi uwezekano wa kutotenda dhambi.
Maadamu tukisema Mungu ni mwema, tayari hapohapo kuna dhana ubaya inayodokezwa.
Mungu anapotajwa kuwa ndiye mwenye upendo, mantiki yake ni kwamba upo upande wa chuki.
Mungu atajwapo kwamba ni mwenye rehema na fadhili, mdokezo wa ukatili na ushururishaji huibuka mawazoni.
Sasa kufuatia utashi alioumbiwa Lusifa na malaika wengine, walikuwa huru kudadisi upande wa pili unaokinzana na silika za Mungu.
Lusifa aliruhusu mawazo yake kufinyanga dhana hizi hadi zikageuka kuwa vitendo halisi.
Udadisi wake uligeuka kuwa majaribio, majaribio yakawa vitendo na utekelezaji hatimaye vikawa sehemu asilia ya tabia yake!
Ni dhahiri hapa kwamba Mungu wala kamwe katu hahusiki na njia potovu aliyojichagulia Lusifa, kinyume kabisa na Muumbaji wake.
Kwa kweli, hatua yake ya kujiendea apendavyo ni uthibitisho mkubwa mno kuhusu aina ya viumbe ambao Mungu aliwaumba--viumbe wenye maarifa na utashi wanaoakisi silika na tabia Zake Mungu Mwenyewe!
inamaana kuna vitu vinatokea hajui vimetokea wapi!,hivyo inapinga sifa yake ya Umungu kuwa Yeye ndie chanzo cha kila kitu!.
Kamwe hakuna kitu kinachotokea kwa kumshtukiza Mungu.
Yeye ni Mungu aonaye mwisho tangu mwanzo.
Kwamba sababu tu hakumzuia Lusifa au Adamu kutenda dhambi, haina maana kwamba hana uwezo huo.
Mungu alipotuumba, akatuweka kwenye mafunzo ya kutufundisha masomo ya kumtumaini na kumtii kama alivyosema.
Angeweza kutuumba kama watu tusioweza kutenda dhambi kabisa, tuonaotii tu ama tuambiwe au tusiambiwe.
Lakini alichagua, kwa hekima Yake, kutupatia akili na maarifa (kama Yeye alivyo na akili na maarifa) ili vituongeze kwanza kumtambua kama Mungu wetu na kisha tumtii katika kila asemacho na kumwabudu kwa jinsi alivyo!
Kila mtu mwenye akili anajua fika kwamba uamuzi huu wa Mungu ulikuwa wenye busara zaidi, licha ya kutiwa dosari na wimbi la dhambi.
pili sifa yake ya uumbaji na uweza wa kila kitu inakuja kuleta tafrani ikiweka ile mantiki ya kuumba kitu anachoweza kukibeba na vilevile asiweze pia!.
Mantiki hii ni ya kipuuzi katika namna zake zote.
Ni sawa na kuhoji iwapo Mungu anaweza kuumba kitu kilichopo na kisichokuwepo kwa wakati mmoja!
Haina tofauti na kuuliza iwapo Mungu anaweza kutenda dhambi?
Hivi ni mfano wa vitu visivyokuwa sehemu ya asili ya Mungu.
hivyo vitabu vya dini ni ulaghai kabisa hamna kitu mule na ndio maana kila siku watu wanaomba na shida ziko palepale!,nani hataki raha..?
Kusudi kuu la Maandiko siyo hasa kumpatia mwanadamu utajiri tu wa kidunia.
Biblia inasema: utafuteni kwanza ufalme wa Mungu na haki Yake ndipo hayo yote mtazidishiwa.
Lipi la maana? Kufa maskini na kuurithi ufalme wa Mungu, au kutajirika kidunia kwa muda halafu mwishowe ukaishia jehanamu?
Aidha, kuhusu mafanikio ya kidunia, Biblia imeahidi kwamba Mungu ametupatia nguvu za kupata utajiri (Kumbukumbu 8:18).
Ukiendekeza uvivu, starehe na anasa, hakika utakuwa maskini hadi siku ya kufa!
unafikiri nani anapenda magonjwa..?
kama huyo Mungu angekuwa anatatua shida zetu kuna mtu asingemuabudu..?
yani aniponye magonjwa,anipe mahitaji yangu yote,afya,ulinzi,chakula na uhakika wa maisha ya milele huko peponi baadae. halafu nisimuabudu basi nitakuwa zwazwa la mwisho..😂
Ndiyo maana kuna mabilioni ya watu wanaomwamini Mungu.
Mungu amebadilisha maisha yao kimwili, kiafya, kijamii, kiuchumi na kiroho; nao wana tumaini la uzima wa milele.
lakini kwa staili hii anayoenda najua kabisa hakuna Mungu wa namna yake labda yupo wa tofauti ambae hata hakuamua kijitapa kama huyo wa kwenye vitabu,ye alitenda kazi yake akamaliza akaendelea na mishe nyengine..😂😅
Kupima uwepo wa Mungu kwa sababu tu ya uchumi ama afya yako kudodora, huko ni kutomtambua Mungu jinsi hasa alivyo.
Wapo watu hapa duniani huenda wamenyimwa mafanikio na utajiri kwa vile kwa namna hiyo tu ndipo wanaweza kuokolewa katika uzima wa milele.
^Maana mawazo Yangu si mawazo yenu wala njia Zangu si njia zenu, asema Bwana. Maana kama vile mbingu zilivyo juu sana kuliko nchi, kadhalika njia Zangu zi juu sana kuliko njia zenu, na mawazo Yangu kuliko mawazo yenu.^ ~ Isaya 55:8, 9.