Je, Mtanzania, una imani Bunge linaloendelea Dodoma?

Je, Mtanzania, una imani Bunge linaloendelea Dodoma?

Erythrocyte

JF-Expert Member
Joined
Nov 6, 2012
Posts
137,669
Reaction score
272,507
Inasemekana kwamba hata ambaye amenyimwa macho basi angalau anapewa uwezo wa kunusa na kupapasa, hanyimwi vyote.

Ukweli niliouona (maana macho ninayo) ni kwamba wananchi wengi wamelipuuza na kulidharau kabisa bunge jipya linaloendelea Mjini Dodoma, wadau hawana habari nalo wala hawataki hata kufuatilia yanayojiri, taarifa zinaonyesha kwamba namna wabunge hao walivyopatikana na namna uchaguzi wa 2020 ulivyoendeshwa ndio sababu kubwa ya wananchi kulipuuza bunge hili.

Hawaoni kama wabunge walioingizwa bungeni kwa mbeleko ya chuma huku wengine wakiingizwa ndani ya bunge bila kuwakilisha chama chochote cha siasa kama Katiba ya nchi inavyotaka, kuna mashaka mazito kama wabunge hawa wa kutengeneza maabara wanaweza kuhoji masuala ya msingi , kwa ujumla wananchi wameamua kujitenga na bunge hili japo juhudi za kulitangaza zimekuwa kubwa mno !

Nakulilia Tanzania .
 
Yani bunge ndo kwanza limeanza Leo Ila wewe umeshafanya tathmini ya Tanzania mzima kujua ni watu wangapi wanalifatilia loh🧐
Ni Kama huwajui wa tz bado tupo kwenye ishu ya Corona hakuna ajabu lolote bungeni kwa sasa subiri kitu kitokee huko ndo utakua Kama linafatiliwa ama laaa
 
Back
Top Bottom