Je, Mfalme wa Morocco ana habari ya tetemeko la ardhi Kagera?

Jacobus

JF-Expert Member
Mar 29, 2011
4,681
1,698
Wakuu,

Mpaka sasa ukisikiliza Radio One pana tangazo la mkuu wa mkoa wa Kagera akiomba mchango kwa ajili ya janga la tetemeko la ardhi lililotokea huko.

Bahati njema nchi yetu inatembelewa sasa hivi na mfalme wa nchi ya Morocco na tumetiliana mikataba takribani 20 hivi na nje ya hapo bwana huyu kajitolea kujenga msikiti mkubwa hapo Mzizima achilia mbali ombi la Rais wetu la kujengewa uwanja mkubwa wa michezo Dodoma.

Sasa najiuliza kama mheshimiwa mfalme kaambiwa kuhusu tetemeko hilo ni tegemeo langu angetoa pesa ili kumaliza kabisa zoezi la michango kwa jambo hili.

Maadam bado yupo nchini kwani ni jana tu kaelekea Zanzibar basi taarifa apelekewe au mkuu huyo wa Kagera aruhusiwe kumuona na kumweleza jambo hilo. Tuwe na utaratibu wa kufikia tamati kwa kila jambo.
 
Pesa zmeshatosha huko kagera,hiv kiwanja na msikit kaviomba raisi au huyo mfalume ndo alikuwa kapanga hvo
 
Wakuu, mpaka sasa ukisikiliza Radio One pana tangazo la mkuu wa mkoa wa Kagera akiomba mchango kwa ajili ya janga la tetemeko la ardhi lililotokea huko.

Bahati njema nchi yetu inatembelewa sasa hivi na mfalme wa nchi ya Morocco na tumetiliana mikataba takriban 20 hivi na nje ya hapo bwana huyu kajitolea kujenga msikiti mkubwa hapo Mzizima achilia mbali ombi la Rais wetu la kujengewa uwanja mkubwa wa michezo Dodoma.

Sasa najiuliza kama mheshimiwa mfalme kaambiwa kuhusu tetemeko hilo ni tegemeo langu angetoa pesa ili kumaliza kabisa zoezi la michango kwa jambo hili.

Maadam bado yupo nchini kwani ni jana tu kaelekea Zanzibar basi taarifa apelekewe au mkuu huyo wa Kagera aruhusiwe kumuona na kumweleza jambo hilo. Tuwe na utaratibu wa kufikia tamati kwa kila jambo.
Wabongo tuna mambo!?
Yaani tumeshajitoa kabisa katika kutimiza wajibu wetu tunataka kila jambo tutembeze bakuli! Aibu hii.

BTW, Tujiulize zile zilizokwisha changwa zimewasaidia vipi waathirika?
 
Duhh,Mkuu
Ile budget inakuwa ya Serikali yake kwa Tanzania
Mbona Obama alikuja hapa na kutuacha na Shida zetu.

Maisha sio rahisi namna hiyo mkuu,kwamba msaada mmoja basi unalazimisha kila shida yako itatuliwe.Wakati kuna Nchi nyingi zinahitaji Misaada

Kwanza Tujiulize,sie wenyewe tumechangia nini?

We Simba na Yanga huwa wanajaza uwanja na mamilioni ya pesa yanapatikana
Hivi watu wanashindwa Kuandaa shindano maalum,maana Simba na Yanga huwa hawana mechi za kirafiki,wao kila mechi ni vita kwao.
Sasa wangekutanishwa kwa shindano la (NANI MKALI WA USAJILI),ili kutoa hamasa,badi naamini hata wasio washabiki wangejaza uwanja na pesa hizo kwenda kwa wahanga.

Lakini kwa vile wapiga dili ni wengi na watanzania ni wa kulalama tu bila kusaidia na kila kitu kusema serikali,hapa ndio inabidi tuwe wapole.
Ni sawa na kuona Panya road wanalaza wanaume wote wa Dar,na kila mmoja kuona kwamba la mwenzie sio lake mwisho wa siku wote mnavikwa kanga.Ila kama watu wakiwa wamoja basi suala la Bukoba tunaliweza wenyewe wananchi.Ila kama ni kuandika humu mitandaoni basi wema tupo wengi saana na wanafiki tupo telee



 
Awe na Habari ya tetemeko ambalo halipo nchini kwake ili limsaidie nini?
 
Wakuu, mpaka sasa ukisikiliza Radio One pana tangazo la mkuu wa mkoa wa Kagera akiomba mchango kwa ajili ya janga la tetemeko la ardhi lililotokea huko.

Bahati njema nchi yetu inatembelewa sasa hivi na mfalme wa nchi ya Morocco na tumetiliana mikataba takriban 20 hivi na nje ya hapo bwana huyu kajitolea kujenga msikiti mkubwa hapo Mzizima achilia mbali ombi la Rais wetu la kujengewa uwanja mkubwa wa michezo Dodoma.

Sasa najiuliza kama mheshimiwa mfalme kaambiwa kuhusu tetemeko hilo ni tegemeo langu angetoa pesa ili kumaliza kabisa zoezi la michango kwa jambo hili.

Maadam bado yupo nchini kwani ni jana tu kaelekea Zanzibar basi taarifa apelekewe au mkuu huyo wa Kagera aruhusiwe kumuona na kumweleza jambo hilo. Tuwe na utaratibu wa kufikia tamati kwa kila jambo.
Jamaa hana tamati ni mtu wa mchakato mpaka dunia ilale...japo alitupumza kuwa hato hitaji michakato..ila kwa hizi michakato ya ukaguzi wa watumishi mara tukusanya misaada ya tetemeko kila leo na wahanga bado wanaambulia patupu
 
Na nyie hamchoki kuandika, ile ilikuwa ziara ya kiserikali na tetemeko halikuletwa na serikali. Hebu fanya kazi.
 
Nyie watu, hivi tetemeko mnaliona ni a very big issue kila mtu atangaziwe. Kwa taarifa yenu, hilo tetemeko sii lolote, sii chochote, wala sio issue kuubwa kivile ndio maana sisi wengine hatuna time kabisa hata kutia mguu, tuko bize na mambo mengine muhimu zaidi kwa taifa.

Yes kuna watu walipoteza maisha siku zao ndio ilikuwa imefika na pole ya maandishi tulitoa.

Kwa vile tetemeko halikusababishwa na serikali yetu, tafadhalini sana tuache kuisakama serikali. Waliobomokewa nyumba wajenge wenyewe. Kama bado kuna malalamiko mlaumuni aliyesabibasha tetemeko na sio kuilaumu serikali yetu.

Pasco
 
Na nyie hamchoki kuandika, ile ilikuwa ziara ya kiserikali na tetemeko halikuletwa na serikali. Hebu fanya kazi.
Sawa tetemeko halikuletwa na serikali, lakini mbona serikali inahamasisha na kupokea michango ya tetemeko hilo?
 
Back
Top Bottom