minyoo
JF-Expert Member
- May 25, 2013
- 21,640
- 20,366
Tumemsikia mwenyekiti wa CCM Kinondoni akisema majina yote yanakwenda Dodoma na watawachunguza washindi wa kura za maoni kuhoji ushindi wao wameupataje pataje?
Kwa maana nyingine wanatumia vyote vya uchunguzi kupata taarifa, kwa maana hiyo mshindi wa kwanza ikitokea akawa na chuki na wachunguzi au wachunguzi wakiwa na mahusiano na walioshindwa ni lazima watamhujumu mshindi wa kwanza.
Huu ni mfumo wa hovyo na unaweza kupelekea uwepo wa Rushwa kwa washindi kuhitaji taarifa zao ziwe safi pia unaweza kusababisha CCM kuchuja watu safi na kuleta magarasa kwa kisingizio cha uchunguzi wao usio na tija, nini maana ya kura ya maoni? TAKUKURU walikuwepo ni kwa nini hawakumaliza kila kitu huko chini?
Kitendo cha kwenda kumkata mshindi kisha kumleta mtu wa nne au tano ni kuwanyima fursa, kuwakejeli wapiga kura na hapo ndipo upinzani hutumia vizuri madhaifu ya CCM.
Kwa maana nyingine wanatumia vyote vya uchunguzi kupata taarifa, kwa maana hiyo mshindi wa kwanza ikitokea akawa na chuki na wachunguzi au wachunguzi wakiwa na mahusiano na walioshindwa ni lazima watamhujumu mshindi wa kwanza.
Huu ni mfumo wa hovyo na unaweza kupelekea uwepo wa Rushwa kwa washindi kuhitaji taarifa zao ziwe safi pia unaweza kusababisha CCM kuchuja watu safi na kuleta magarasa kwa kisingizio cha uchunguzi wao usio na tija, nini maana ya kura ya maoni? TAKUKURU walikuwepo ni kwa nini hawakumaliza kila kitu huko chini?
Kitendo cha kwenda kumkata mshindi kisha kumleta mtu wa nne au tano ni kuwanyima fursa, kuwakejeli wapiga kura na hapo ndipo upinzani hutumia vizuri madhaifu ya CCM.