Missile of the Nation
JF-Expert Member
- May 24, 2018
- 16,818
- 62,031
Mwalimu Nyerere aliwahi kumwambia Mzee Yusuf Makamba kuwa achague moja, Heshima au Tamaa maana hivyo vitu viwili havikai nyumba moja.
Sasa hii critical moment iko kwa Freeman Mbowe leo, mtu ambaye ana heshima kubwa nchini kama mtu aliyepigania mageuzi, aliyeongoza harakati za kisiasa za kukuza upinzani nchini.
Leo tunaambiwa kuwa yeye ndiye kiongozi anayeogoza genge la kukihujumu chama chake cha CHADEMA, Chama alichokijenga kwa jasho kubwa. Hii hali siyo kwamba inasikitisha na kuhuzunisha lakini kwa kiwango kikubwa inamharibia sifa na Legacy yake.
Pengine nitumie fursa hii kumueleza Mbowe mambo yafuatayo:
1. Je anachagua kuua mtoto wake mwenyewe (CHADEMA) ili kufuata masharti ya mganga (CCM)?
Kama nilivyoeleza, CHADEMA ina jasho jingi tu la Mbowe, itakuwa ni ajabu Mbowe kula njama za kuitoa kafara CHADEMA kwa ajili ya kupata utajiri wa kafara. Kwa kweli Jamii ya Watanzania itahuzunishwa, itachukizwa na kwa kweli itamuondolea heshima kubwa aliyojijengea kwa maka zaidi ya 30 kwenye medani ya siasa za mabadiliko nchini. Move ya kuiua CHADEMA itahesabika kama tamaa na ubinafsi uliopitiliza na kwa kweli Mbowe hatopata heshima kwa kula njama za kuia CHADEMA.
2. Iwapo Mbowe atashiriki kuiua CHADEMA ni kweli atapata fedha lakini atakuwa amewadhulumu watanzania kwa kiwango kikubwa sana.
Nimjulishe tu Mbowe kuwa kujaribu kuidhoofisha CHADEMA kweli kunaweza kumpa yeye pesa , lakini ajue tu kuwa pesa hizo kimsingi zitatokana na pesa zilizokwapuliwa na mafisadi kutoka kwa Watanzania, ama kupitia kodi zao, au kutokana na hongo mafisadi waliyopata kutokana na wao kuuza rasilimali za nchi yetu kwa mikataba ya kilaghai (kama kuuza bandari zetu kwa mikataba mibovu). Hiyo itakuwa ni dhambi kubwa na kwa kweli Mbowe atajibu mbele ya Mwenyezi Mungu kwa ulaghai na kushiriki kuwahujumu Watanzania kwa maslahi binafsi.
3. Mbowe akumbuke tu watu waliomwaga damu zao kwa ajili ya Mabadiliko na CHADEMA. Je yuko tayari kuwasaliti wote hawa kwa ajili ya vipande 30 vya fedha za mafisadi?
Kuna watu wamemwaga damu zaokwa ajili ya mabadiliko nchini hususana kwa ajili ya ustawi wa CHADEMA. Orodha ni ndefu, lakini hebu twambie, Mbowe atamueleza nini Alphonse Mawazo, Elias Michael, Ben Saanane, Deusdedith Soka, Mzee Ali Kibao, Mdude Nyagali na wengine wengi tu waliotekwa na kupotezwa kwa kudai haki na mabadiliko ya kweli nchini wakiwa ni wanachamama wa CHADEMA, iwapo Mbowe atakuwa msitari wa mbele kukisaliti chama chake yeye mwenyewe?.
4. Mbowe ajue tu kuwa Wachumia tumbo waliokuwa wanakula kwa mgongo wake bado wanataka kumtumia ili waendelee kula kupitia yeye, astuke!.
Wachumia tumbo wote aliowapa vyeo ndani ya sekretariat ya CHADEMA, waliowekwa pembeni na uongozi mpya, njaa zao zimeanza kuchachamaa zaidi. Walizoea pesa laini laini za kujichotea ndani ya chama, na kwa kuwa Mbowe hakuwa mkali juu yao, au aliwakingia kifua basi leo dili zimekata na hivyo wanatafuuta namna nyingine ya kupata hela rahisi. Hivyo wachumia tumbo hawa bado wanataka kumtumia Mbowe, wanajaribu kutumia star power yake ili iwe kama ngazi ya kuendelea kula pesa za CCM. Mbowe inabidi astuke, asitumike kama nyavu ya kuwavulia hawa wachumia tumbo samaki za kushibisha matumbo yao.
5. Mbowe afahamu tu kuwa, dignity is better than silver and gold.
Mwalimu Nyerere laiti angetaka kuendelea kutawala hadi kufia madarakani angeweza, kama angetaka ubilionea angeweza, lakini alichagua dignity, maana dignity ni bora kuliko vipande vya fedha. Je Mbowe anadhani hana role ya kuplay ktk nchi hii mpaka awe katika nafasi za uongozi au cheo?, la hasha, huyu ni mtu mwenye uzoefu mkubwa na heshima kubwa mbele ya umma, sasa kwa nini ashawishiwe au kushawishika kuiharibu dignity yake kwa sababu ya maslahi binafsi?
6. Kabla Mbowe hajawaza kuisaliti CHADEMA akumbuke tu ni nani alimuweka jela, je ni wanachadema au CCM?
Hii kitu ndugu Mbowe lazima ajitafakari sana. Je ni nani alimpa heshima kwa miaka zaidi ya 30, Je ni wanaCCM au wanaCHADEMA?. Je ni nani alimpigania kila kukicha kwenye kupaza sauti ili atoke jela, je ni CCM au ni CHADEMA?. Sasa inakuwaje leo anataka kuiumiza CHADEMA na kuipa unafuu wa kisiasa CCM?.
MWISHO:
Mimi nataka nimkumbushe tu ndugu Mbowe kuwa , Mwenyezi Mungu kupitia vitabu vitakatifu ameonya vikali kuhusu usaliti, hongo, hila na hali ya kurudi nyuma katika mapambano ya kuodoa udhalimu. Amana ambayo Watanzania wameiweka kwa Mbowe kwa miaka 30 ni kubwa sana, Mwenyezi Mungu amelishuhudia hili. Kushiriki au kula njama kuidhoofisha CHADEMA ni kuvunja amana na Mwenyezi Mungu ndiye Mlipaji,
Ndugu Mbowe kama una nia au lengo la kuweka maslahi yako binafsi juu ya taasisi ya CHADEMA kwa kufanya kitendo chochote kitakachokwamisha chama hicho basi Mwenyezi Mungu atakuhukumu kwa hukumu stahiki. Maana wanaCHADEMA walikupa imani na amana, tafadhali lifahamu hilo!
Sasa hii critical moment iko kwa Freeman Mbowe leo, mtu ambaye ana heshima kubwa nchini kama mtu aliyepigania mageuzi, aliyeongoza harakati za kisiasa za kukuza upinzani nchini.
Leo tunaambiwa kuwa yeye ndiye kiongozi anayeogoza genge la kukihujumu chama chake cha CHADEMA, Chama alichokijenga kwa jasho kubwa. Hii hali siyo kwamba inasikitisha na kuhuzunisha lakini kwa kiwango kikubwa inamharibia sifa na Legacy yake.
Pengine nitumie fursa hii kumueleza Mbowe mambo yafuatayo:
1. Je anachagua kuua mtoto wake mwenyewe (CHADEMA) ili kufuata masharti ya mganga (CCM)?
Kama nilivyoeleza, CHADEMA ina jasho jingi tu la Mbowe, itakuwa ni ajabu Mbowe kula njama za kuitoa kafara CHADEMA kwa ajili ya kupata utajiri wa kafara. Kwa kweli Jamii ya Watanzania itahuzunishwa, itachukizwa na kwa kweli itamuondolea heshima kubwa aliyojijengea kwa maka zaidi ya 30 kwenye medani ya siasa za mabadiliko nchini. Move ya kuiua CHADEMA itahesabika kama tamaa na ubinafsi uliopitiliza na kwa kweli Mbowe hatopata heshima kwa kula njama za kuia CHADEMA.
2. Iwapo Mbowe atashiriki kuiua CHADEMA ni kweli atapata fedha lakini atakuwa amewadhulumu watanzania kwa kiwango kikubwa sana.
Nimjulishe tu Mbowe kuwa kujaribu kuidhoofisha CHADEMA kweli kunaweza kumpa yeye pesa , lakini ajue tu kuwa pesa hizo kimsingi zitatokana na pesa zilizokwapuliwa na mafisadi kutoka kwa Watanzania, ama kupitia kodi zao, au kutokana na hongo mafisadi waliyopata kutokana na wao kuuza rasilimali za nchi yetu kwa mikataba ya kilaghai (kama kuuza bandari zetu kwa mikataba mibovu). Hiyo itakuwa ni dhambi kubwa na kwa kweli Mbowe atajibu mbele ya Mwenyezi Mungu kwa ulaghai na kushiriki kuwahujumu Watanzania kwa maslahi binafsi.
3. Mbowe akumbuke tu watu waliomwaga damu zao kwa ajili ya Mabadiliko na CHADEMA. Je yuko tayari kuwasaliti wote hawa kwa ajili ya vipande 30 vya fedha za mafisadi?
Kuna watu wamemwaga damu zaokwa ajili ya mabadiliko nchini hususana kwa ajili ya ustawi wa CHADEMA. Orodha ni ndefu, lakini hebu twambie, Mbowe atamueleza nini Alphonse Mawazo, Elias Michael, Ben Saanane, Deusdedith Soka, Mzee Ali Kibao, Mdude Nyagali na wengine wengi tu waliotekwa na kupotezwa kwa kudai haki na mabadiliko ya kweli nchini wakiwa ni wanachamama wa CHADEMA, iwapo Mbowe atakuwa msitari wa mbele kukisaliti chama chake yeye mwenyewe?.
4. Mbowe ajue tu kuwa Wachumia tumbo waliokuwa wanakula kwa mgongo wake bado wanataka kumtumia ili waendelee kula kupitia yeye, astuke!.
Wachumia tumbo wote aliowapa vyeo ndani ya sekretariat ya CHADEMA, waliowekwa pembeni na uongozi mpya, njaa zao zimeanza kuchachamaa zaidi. Walizoea pesa laini laini za kujichotea ndani ya chama, na kwa kuwa Mbowe hakuwa mkali juu yao, au aliwakingia kifua basi leo dili zimekata na hivyo wanatafuuta namna nyingine ya kupata hela rahisi. Hivyo wachumia tumbo hawa bado wanataka kumtumia Mbowe, wanajaribu kutumia star power yake ili iwe kama ngazi ya kuendelea kula pesa za CCM. Mbowe inabidi astuke, asitumike kama nyavu ya kuwavulia hawa wachumia tumbo samaki za kushibisha matumbo yao.
5. Mbowe afahamu tu kuwa, dignity is better than silver and gold.
Mwalimu Nyerere laiti angetaka kuendelea kutawala hadi kufia madarakani angeweza, kama angetaka ubilionea angeweza, lakini alichagua dignity, maana dignity ni bora kuliko vipande vya fedha. Je Mbowe anadhani hana role ya kuplay ktk nchi hii mpaka awe katika nafasi za uongozi au cheo?, la hasha, huyu ni mtu mwenye uzoefu mkubwa na heshima kubwa mbele ya umma, sasa kwa nini ashawishiwe au kushawishika kuiharibu dignity yake kwa sababu ya maslahi binafsi?
6. Kabla Mbowe hajawaza kuisaliti CHADEMA akumbuke tu ni nani alimuweka jela, je ni wanachadema au CCM?
Hii kitu ndugu Mbowe lazima ajitafakari sana. Je ni nani alimpa heshima kwa miaka zaidi ya 30, Je ni wanaCCM au wanaCHADEMA?. Je ni nani alimpigania kila kukicha kwenye kupaza sauti ili atoke jela, je ni CCM au ni CHADEMA?. Sasa inakuwaje leo anataka kuiumiza CHADEMA na kuipa unafuu wa kisiasa CCM?.
MWISHO:
Mimi nataka nimkumbushe tu ndugu Mbowe kuwa , Mwenyezi Mungu kupitia vitabu vitakatifu ameonya vikali kuhusu usaliti, hongo, hila na hali ya kurudi nyuma katika mapambano ya kuodoa udhalimu. Amana ambayo Watanzania wameiweka kwa Mbowe kwa miaka 30 ni kubwa sana, Mwenyezi Mungu amelishuhudia hili. Kushiriki au kula njama kuidhoofisha CHADEMA ni kuvunja amana na Mwenyezi Mungu ndiye Mlipaji,
Ndugu Mbowe kama una nia au lengo la kuweka maslahi yako binafsi juu ya taasisi ya CHADEMA kwa kufanya kitendo chochote kitakachokwamisha chama hicho basi Mwenyezi Mungu atakuhukumu kwa hukumu stahiki. Maana wanaCHADEMA walikupa imani na amana, tafadhali lifahamu hilo!