Sote tunazikumbuka tetesi na minong'ono iliyokuwa imezagaa mara tu baada ya kifo cha Magufuli. Tetesi zilidai kundi la watu watiifu kwa Magufuli hawakutaka mama akikalie kiti hicho. Walifanya kila liwezekanalo ili waweke mtu wao.
Ikatokea kundi la "wenye nchi" likawa na akili kubwa na ushawishi mkubwa kwa vyombo vya ulinzi na usalama wakakakomaa na kuhakikisha mama anakalia kiti.
Kufuatia kadhia hiyo, tuliona watu wengi waliokuwa watiifu kwa Magufuli wakionja joto ya jiwe baada ya mama kukikalia kiti. Akina Bashiru, Polepole, Ndugai, Lukuvi, Kabudi, Hapi, Sabaya, n.k waliondolewa kwenye nyadhifa zao ili wasiwe karibu na sinia la mema ya nchi.
Lkn sasa tunaona mwelekeo wa mama ni kulisogeza kundi la mwendazake taratibu kwenye sinia la mema ya nchi. Uteuzi wa Makonda, Biteko na Mnyeti unathibitisha haya.
Swali la kujiuliza ni je, mama analikimbia kundi lililompigania? Kwann?
Ikatokea kundi la "wenye nchi" likawa na akili kubwa na ushawishi mkubwa kwa vyombo vya ulinzi na usalama wakakakomaa na kuhakikisha mama anakalia kiti.
Kufuatia kadhia hiyo, tuliona watu wengi waliokuwa watiifu kwa Magufuli wakionja joto ya jiwe baada ya mama kukikalia kiti. Akina Bashiru, Polepole, Ndugai, Lukuvi, Kabudi, Hapi, Sabaya, n.k waliondolewa kwenye nyadhifa zao ili wasiwe karibu na sinia la mema ya nchi.
Lkn sasa tunaona mwelekeo wa mama ni kulisogeza kundi la mwendazake taratibu kwenye sinia la mema ya nchi. Uteuzi wa Makonda, Biteko na Mnyeti unathibitisha haya.
Swali la kujiuliza ni je, mama analikimbia kundi lililompigania? Kwann?