Ipo siku tutajenga sanamu ya Hayati Magufuli na kufungua Maktaba yake ili vizazi vijifunze Uzalendo

TumainiEl

JF-Expert Member
Jan 13, 2010
6,188
11,219
Mungu wewe unachukua majabali una chukua wanaume ambao kweli jando lao halikuwa la ganzi. Wanaume wenye misuli ya Imani na uwezo wakuona kesho kwa Imani na matendo. Kwa Tanzania Ulitupa Hayati John Pombe Magufuli. Kijana alie zaliwa ktk ufukara ila ukampa kukikalia kiti cha Jamuhuri ya watu Wa Tanzania na kweli akatupa darasa ambalo kamwe kwa tulio Baki hatuto msahau.

Kama ilivyo kwa mzazi alituchapa na alituadabisha kiukweli kweli, akiwa na ndoto za mzazi siku moja siku moja tutamkumbuka nakwenda ktk kaburi lake nakusema baba tunakukumbuka kama Mungu angetupenda basi angalau angekupa mwaka mmoja tu zaidi utuchape viboko ili tuwe na akili zaidi ya hizi tulizipata kwa viboko na adhabu zako. Tungetubu kama mtoto anavyotubu kwa mzazi baada ya kugunduwa viboko alichapwa ndio vimemfanya kuwa Bora leo. Kwa hakika kama sio kifo kilikuwa na nia yakumpa kiti muda wa ziada jambo halikutokea ktk Historian yetu.

Jemedari huyu wa awamu ya Tano aliitikisa nchi ikatikisika, aliitikisa majabali yakatikisika na alivitikisa viti visivyoguswa vikatikisika kwake usawa ndio ilikuwa ndoto. Alipambana na majangili mpaka wanyama Porini na miti maporini ikawa inamuombea kwa Mungu. Alilinda kwa mkono wa chuma mipaka na siri za serikali kiasi kila alie na siri aliona kuliko kuitoa Bora kunywa sumu. Kwake Jamuhuri ndio ilikuwa ibada yake mbele za Mungu wake nawana Jamuhuri walimtambua hivyo. Hakuna mission alipanga Ika fail japo mwisho uwenda some thing wrong happen ktk mission zake itabaki kuwa top secret japo madhara makubwa yatakuwepo huko mbeleni.

Alimanisha alicho Maanisha na hakuwa na utani kwa kile alimanisha. Kwake dam na neno lake vilikuwa nijambo lakuchaguwa na hiyo ndio maana ya kiongozi. Wanafiki na mapandikizi walipata tabu sana maana aliwafanya wajione kama mapanzi mbele ya tai.

Hakuwa na mchezo hakuwa na masihara kwenye kitu kinaitwa hela ya serikali na nidham ya kazi kama ulitaka kuona rangi ya mtawala huyu basi cheza na hela ya serikali na kuwa mzembe kazin utachekea chooni. Watu walirudisha risiti na pesa ilio Baki ya serikali. Watu waliogopa pesa ya serikali kiasi ilifika mahali TUNAKUTANA kwa Mama ntilie Yani mama ntilie alipanda thamani kuliko 5 star hotels ama restaurant ama kwa hakika nchi ilisimama na vitambi vya upigani vilipotea.

Sito sahau story yakutisha ya kijana mmoja jirani kijana alie kuwa misheni town alie kuwa akila kwa kutumia sim yake aka misheni town. Nakama unakumbuka ili kuleta nidham kazin na mtaani Baba alikuwa sahani moja na misheni town. Kijana yule alikuwa akila maisha mjini pasipo kufanya kazi leo Tiss kesho Jwtz ila chini ya Mwamba kwa mara ya kwanza kijana yule alianza kujifungia ndani kama mbwa wakati wa mchana na kujifungulia usiku. Kijana alianza kukonda na mwisho alikufa kifo cha ghafla baada yakukutana na team hatari yakutokomeza wapigaji. Shikamoo Baba it was real top top secret never before. Kuna watu walijimaliza wenyewe baada yakugunduwa wamefanya madudu na adhabu yake ni kifo kwa usaliti wao. Huyo ndio Mwamba Magufuli.

Mbabe huyu alitufanya watu wawe na plan B ktk kila wakifanya na alifanya watu kuheshim mishara yao nakupenda ndoa zao while madada poa wakifa njaa nakutafuta kazi nyingine pasipo shurutishwa na mtu. Nikatika kipindi chake alifanya mageuzi makubwa na yaaina yake kwenye secta ya ajira sio hivyo tu alihakikisha masikini akiingia Ofisi ya serikali awe mfalme asikudanganye mtu masikini na mtu wa chini alikuwa mfalme maana ilikuwa akisikia mtu amedhulumiwa au akionewa na RC walile eneo hakufanyia kazi tatizo lake unakiwa kichwa bila notice. He was Iron Men. Acha chezea hii namba.

Nchi ilizimgirwa na hofu ya kuwa muwovu ktk Taifa lako nikujitafutia adhabu ya kifo jambo lilimfanya kila muhalifu kuacha uhalifu nakuwa Raia mwema kwakufanya kazi kwa bidii ila sio uhalifu ndio ktk kipindi hiki watu walifanya biashara ndogondogo kwa kiwango cha jabu sana Ali push watu kujiajiri nakutafuta ideas na yeye kuwapa nguvu free market. Wapo walimponda ila alikuwa na ndoto ambayo kaburi imeimeza ghafla.

Siwezi simulia au kueleza kile aliwafanya wauza unga ila mtafute muuza unga atakwambia ilikuwa mithili ya picha za CIA na mossad vile aliutokomeza huu mtandao alihakikisha either unalala chini au unaacha mama mkanye mwanao. He was master on Intelligence of finding crime. Nakweli wauza madawa na wala madawa walijikuta soba bila shuruti. Moja ya jambo sitosahau nimla mdawa mmoja kuniambia ameacha dawa maana hakuna dawa zakulevya... Lazima huko usalama huyu jamaa awe reference ya genius president on crime finding.

Hayati Magufuli hakuwa kiumbe cha kawaida hakuwa mwanadam au kiongozi wakawaida alipania na alikumbuka ahadi yake kwa Mungu na akiifanyia kaz kwa dam na jasho kwa ajili ya

Tanzania. Moja maisha yalio watisha wengi nikufanya kaz usiku wakati mwingine usiku mzito sana the guy was not normal human being lazima watu wakaribu watasimulia maajabu ya huyu kiumbe.

Alilijua duka na alikuwa na kila siri ya duka na hili likiwatetemesha wengi japo wazalendo walio mpenda walisema Mungu Asante umetuletea mkombozi. Alizijuwa siri ambazo watangulizi wake uwenda hawakudhani angezijuwa na alisoma sana kila siri wakati mwingine files ZINGINE mezani mwake zilimtisha hata yeye mwenyewe na uwenda ndio maana alituacha ktk wakati hakuna aliamini angetuacha japo Yeye alishakiona kifo.

Mwamba ndio mwanaume alie Jenga hili Taifa kwenye miundo mbinu huwezi simulia miundombinu ya Taifa hili bila kumtaja Mwamba Magufuli. Alitandaza lami mpaka Malaika wa Mbinguni wakasema lazima utaliongoza hili Taifa. Wachambuzi wa mambo wanasema kama angekuwa kibaka uwenda ndio waziri angekuwa na ukwasi wakitisha ktk Taifa hili ila alikuwa wakawaida sana.

Ukikaa nakujiuliza why Kuna kundi lina mchukia sana jibu nimoja tu kitu alicho wafanyia na pin alizowawekea na makofuli aliwafungia milango yao ya ulaji kamwe hawatoweza kuifungua hata baada ya miaka 100 yani aliona zaidi yao mfano nani anapenda mradi wa bwawa la mwalim Nyerere kama unamacho ya mbali Yani huu mradi unawauma watu fulani sana Usiniulize kwanini.

Miaka inakuja Gemedari huyu atakuwa Habari ya Taifa na huwenda siku zinakuja kutakuwa na Magufuli day. Siku zinakuja kumdhihaki nakumsema huyu Mwamba vibaya unakosa kura siku zinakuja hata upinzani watamtaja kwa mema. Wajukuu watamuimba nakumsoma mashuleni.

Maana ndie kiongozi alie sema moyoni mwake kuliko kuishi nakupigiwa mizinga 21 na heshima na kukaa ktk magorofa nakula Pepo za Dunia ni Bora kufa nikiacha alama ambayo kila mtu hatoangalia mabaya yangu ila mema yangu. Nayeye mwenyewe kabla ya kutuacha aliwahi sema "Ipo siku Watanzania Mtanikumbuka sio kwa mabaya yangu ila Mazuri hivyo tuzidi kushikamana na kupenda" Hayati Baba wa Ujenzi wa Taifa la Tanzania John Pombe Magufuli.

Hayati Magufuli ni nyota iliozima wakati wa mchana ila lijapo giza atamulika kwa milele. Asante Baba Asante Mzee Magufuli umetufundisha Uzalendo wa kweli kwa Taifa letu. Amen
Mnara wa kwanza
Tarehe 20.05.2023 tunazindua ikulu mpya Dodoma. Naomba muweke kumbukumbu maono yangu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom