Majini ni mashetani ambao wanafuatana na tamaduni za nchi za kiarabu, lakini pia, majini haya yalikuwa ni mashetani yanayofuatana na maji au mikusanyiko ya maji; kwasababu makao yao makuu yalikuwa majini ukisoma, Ezekieli 29:3-5. Na ndio maana mfalme wa Misri, Farao alikuwa anakwenda kuabudu katika maji, Ukisoma, Ezekieli 32:2-3 inaeleza jinsi Farao alivyotegemea miungu ya katika maji kiasi biblia inamwita joka wa majini.
Kwasababu ya mashetani hao wanaokaa majini, mara nyingi maji katika biblia yamekuwa yakitumika kuonyesha uharibifu, Zaburi 18:16. Ndio maana hata kipindi cha Musa alipokuwa anamfuata Farao ili kuomba ruhusa ya kutoka utumwani, maranyingi, alikuwa akimkuta anatoka au anakwenda majini, Kutoka 7:18; 8:20; Ilikuwa ni desturi ya farao kwenda kuabudu katika mikusanyiko ya maji. Maandiko yameonyesha sana kuhusu mashetani wa baharini, katika Ufunuo 14:31; 20:13, Isaya 27:1, Ayubu 3:8.