Je, majini ni kitu gani na yanataka nini?

Je, majini ni kitu gani na yanataka nini?

Status
Not open for further replies.
Bado sijakuelewa hebu twende taratibu,anza kueleza kwanza roho ni nini?Na ueleze hao mashetani ndiyo akina nani? Halafu ndiyo uje kueleza hizo roho chafu...anza hapo kwanza.
 
Cheki na mzizi mkavu utajua mengi sana! Mi shajaribu kuliita jini nikabugi step man nilikimbia balaa
 
sihitaji abrakadabla hadi siku nionane nao live niwahoji, maana inakuwaje mtu anakuwa na marohani(majini)afu anakatazwa na hao majini kunywa pombe, umalaya, uhuni, uvutaji sigara nk, kwa manufaa yepi na ya nani
 
Mhh wala sikai hapa nina haraka kidogo nitarudi baadae
 
Bado sijakuelewa hebu twende taratibu,anza kueleza kwanza roho ni nini?Na ueleze hao mashetani ndiyo akina nani? Halafu ndiyo uje kueleza hizo roho chafu...anza hapo kwanza.
Hapa nitakupa maelezo mafupi kuhusu Roho kama ulivyo uliza hpo kwenye post yako.

Kutokana na Biblia na jinsi waandishi wa Biblia walitumia neno la Kiebrania ru′ach au neno la Kigiriki, pneu′ma waliporejelea "roho." Maandiko yenyewe yanaonyesha maana ya maneno hayo. Kwa mfano, andiko la Zaburi 104:29linasema: "[Yehova] ukiiondoa roho [ru′ach] yao, wanakata pumzi, na kurudi katika mavumbi yao." Andiko la Yakobo 2:26 linasema kwamba "mwili bila roho [pneu′ma] umekufa." Katika andiko hilo "roho" inamaanisha kile ambacho huupa mwili uhai. Bila roho, mwili umekufa. Kwa hiyo, katika Biblia neno ru′ach halitafsiriwi tu "roho" bali pia "nguvu" au kani ya uhai. Kwa mfano, Mungu alisema hivi kuhusu Mafuriko ya siku ya Noa: "Ninaleta gharika ya maji duniani ili kuharibu kutoka chini ya mbingu wote wenye mwili walio na nguvu [ru′ach] za uhai ndani yao." (Mwanzo 6:17; 7:15, 22) Hivyo, "roho" inarejelea nguvu isiyoonekana, inayotendesha viumbe vyote vilivyo hai.

Popote neno "roho" limetumika, linaashiria sehemu ya ndani ya mwanadamu ambayo "yakutanika" na Mungu, ambaye Yeya mwenyewe ni Roho (Yohana 4:24).
 
Hayo mapepo na majini yameumbwa na nani?
MWANZO WAO: WALITOKEA WAPI?
Majini au mapepo ni viumbe ambavyo havionekani kwa macho, ni viumbe kama malaika isipokuwa majini na mapepo yalifukuzwa mbinguni pamoja na shetani baada ya kuasi, na yalitupwa duniani yakisubiri siku ya mwisho ya hukumu. Kabla ya wao kuitwa Majini na Mapepo, hao walikuwa ni Malaika wa Mungu. Dhambi ndio iliwafanya wawe Mapepo/Majini/Shetani/

Kumbuka kuwa, Mungu wa Biblia hakuumba dhambi na wala hakuumba Mabaya, bali, kila alicho kiumba kilikuwa safi na kikamilifu.

Shetani na majini, wanajua kabisa kuwa jehanum ya moto ipo kwa ajili yao, ndiyo maana wanafanya kila mbinu wasiingie peke yao huko jehanum, shetani ni mwongo, laghai anawatumia sana wachawi, waganga wa kienyeji, wasoma nyota kupandikiza majini, kuiba nyota yako ya mafanikio, kuchukua watu misukule nk.
AINA ZA MAJINI NA KAZI ZAO:
Kuna aina nyingi za majini baadhi yake ni kama:-

1) Murafari – hili ni jini linalozuia mafanikio ya kupata fedha, mafanikio ya elimu nk.
2) Latifu – hili jini linaloleta ufukara, mateso, hata ukipata pesa matumizi yake yanakuwa ni hovyo
3) Jahari – Jini anayetumiwa kuiba mali na kuzuia biashara kustawi
4) Hasinani – jini hili ni la fujo, ulevi wa pombe, bangi na dawa za kulevya
5) Jube – jini hili linasababisha utasa
6) Subiani – jini la ajali, linasababisha wanawake kutokupata siku zao, na kunyonya damu za akina mama siku zao za hedhi ambapo wanapata maumivu makali sana.
7) Sumil – jini hili huangamiza mimba changa
8) Waidadat – jini hili husababisha wanaume kuvaa hereni kusuka nywele na kutoga masikio.
9) Alibadiri – jini la kifo, likikupata kifo hutokea wakati wowote.
10) Anzura – Linawazuia vijana wa kike na kiume kuolewa/kuoa
11) Maimuna – linawakamata wanaume wenye ndoa zao hadi ndoa inavunjika
12) Makata – linasababisha vifo vya mfululizo kwenye familia
13) Faziur – jini la maandishi. Unaletewa barua ukiisoma tayari umelikwaa
14)Subha – jini hili linasababisha mtu kuwa na kiburi sana na kujiinua.
15) Maulan – jini linalofanya watu kuwa kichaa, au mtu ananuka wakati wowote
16) Al-maul – jini hili linamfanya mtu kuwa ombaomba
17) Zuhura au Zohari – Jini la fujo
18) Araba – Jini hili linafanya mtu apende sana ubani
19) Farkh – jini hili linatumwa hasa kwa wakristo kuangalia kama ana kinga (Wokovu)
20) Baradi – jini hili likikupata basi ndoa yako ni lazima itavunjika.
21) Shamsu – jini hili huvaa umbile la binadamu kwa sura yoyote.(sasa hivi mitaani majini haya yapo mengi sana)
22) Abuni – jini wa hasira
23) Kaimu – jini la kutambua nyota za watu
24) Tajuruni – jini la utajiri wa kichawi – ni lazima utoe kafara ya mwanao, mkeo au kufanya tendo la ndoa na mama yako mzazi
25) Al-taliki – jini hili linapoteza watu katika mazingira ya kutatanisha
26) Naluju – linasimamia lugha
27) Janatusi – linatumwa alfajiri kabla ya adhana kuleta usingizi kwa Wakristo wasifanye sala
28) Riyaron – jini hili linamfanya mtu afanye kila kazi peke yake
29) Zaitun – Jini hili linasababisha wasichana kuwa na maringo
30) Ruyati – jini linalosimamia ndoto mbaya
31) Al-rahabu – jini linalosababisha hitilafu ya umeme
32) Hadharaji – jini hili linafanya kazi ya kukata kichwa cha mtu ili wapate damu
33) Anazihaji – jini hili ndilo linachukua roho yako ukifa kwenye dhambi
34) Nghruk – linasababisha maafa
35)Munkara – jini la makaburini
36) Takadhuru – jini linaloleta mali za masharti.
37) Rabindi – jini la Waislamu pekee yao ili wafanye fujo.
38) Balishebe – jini la magonjwa yasiyopona
39) Sajiduri – jini linalokusaidia kupata pesa, kisha zinapotea kwa haraka
40) Rumiran – linasimamia uwongo
41) Lairlihabi – linasimamia hofu, kutojiamini na kukata tamaa
42) Rohani – jini la mateso na fujo
43) Betrah – jini hili linasimamia mapambo, kwa mwanamke huwa anajipamba isivyo kawaida, halikadhalika mwanaume
44)Hanshari – linatumiwa sana na waarabu kulinda maduka yao
45) Walihuni – linazunguka nyumba likilinda biashara
46) Kurasih – jini la kupoteza fahamu
47) Tarik – huondoa amani nyumbani, kazini. Linafanya watu wasielewane
48) Atha – mungu wa kiarabu wa kuabudu sanamu
49) Munakir – linapoteza watu kimiujiza
50) Malik – jini la kumiliki biashara
51) Ghatabu – jini la kulainisha macho wa wanawake. Wanakuwa wanarembua
52) Khatuh – jini la uchawi wa kuchukua kucha, nywele na nguo za ndani
53) Fanken – jini hili linasimamia mtu kuzunguza kiswahili cha pwani
54) Zamzam – jini la marashi na kusimamia mikataba ya imani. Mkristo anaposilimishwa basi hutupiwa jini hili kupofushwa akili yake.
55) Mukitala – linatumwa kuangalia kinga za watu
56) Laufili – jini la uvivu
57) Al-khah – linakula damu iliyoganda
58 Abasaa – jini la hasira wivu na jeuri
59) Aherumi – jini la homa za mara kwa mara
60) Muba – jini la maradhi ya kuambikiza
61) Kamariram – jini hili linatoa kinga kwa majambazi
62) Zubiran – jini la uongo na uzushi
63) Abadi – Jini la wizi, umalaya na ujambazi
64) Muzamili- jini la matambiko ya kiarabu
65) Ruhadi – jini la wizi, umalaya na umasikini
66 Usuran – jini la wizi, umalaya, ujambazi na umaskini
67)Tubuyali – jini hili linamfanya mtu kuiba vitu vya ndani ya nyumba. Haibi nje ya nyumba
68) Zirach – jini la wizi, umalaya, ujambazi na umaskini
69) Ashuran – jini la utasa na maradhi ya akina mama

JINSI YA KUYASHINDA MAJINI
Kinga ya majini haya ni nyepesi ni KUOKOKA na kusimama katika neno la Mungu. Kama unayo dalili yoyote iliyosababishwa na majini hayo hapo juu na umeokoka, taja jina la hilo jini, ni lazima litaitika, kisha liwashie moto.

Kama hujaokoka usiyarushie mawe au moto yatakuumiza. Mwuone kiongozi yeyote wa kanisa akuongoze sala ya toba, kisha anza kuwasha moto, hakika yatakimbia na kuacha biashara, kazi, ndoa, na watoto wako huru.
 
Cheki na mzizi mkavu utajua mengi sana! Mi shajaribu kuliita jini nikabugi step man nilikimbia balaa
Ndugu yangu, sikushauri wewe uite majini bali utoe majini. Msome Yesu Kristo alipo kuja hapa duniani, yeye alikemea na kutoa pepo chafu, hiyo ndio sifa ya Mtoto wa Mungu. Kinyume chake, wewe unakuwa sio Mtoto wa Mungu.

Wasome Mitume na Manabii wote, hawakuita na kupunga Majini, isipokuwa Nabii wa Allah.
 
Somo: Mapepo/Majini ni nini?
Lengo Kuu: Kujua mapepo na kazi zake.
Lengo Mahsusi: Kujua namna ya kuzishinda roho za kipepo na kazi zake.

MAPEPO
Ni roho chafu, roho za mashetani, ziwaingiazo watu ili kuwatesa kwa magonjwa na mateso anuwai.
“Naye Yesu akisha kuona kuwa mkutano unakusanyika mbio, akamkemea yule pepo mchafu akamwambia, Ewe pepo bubu na kiziwi,mimi nakuamuru mtoke huyu, wala usimwingie tena”(Marko 9:25) pia (Mt 4:24 &7:22).

Sifa kuu ya Mapepo ni kuwa, hayana umbo, nyama wala mifupa. Ni roho, na roho haiwezi kuwa na mwili wala mifupa (Luka 24:39)”....ni shikenishikeni, mwone; kwa kuwa roho haina mwili wala mifupa...” Isipokuwa, Huweza kuingia ndani ya mwili wa kiumbe hai na kuvaa umbo na sura yake.

Kumbuka: Hii ziyo mizimu au Roho za wafu. Mtu akishakufa, roho yake haina uwezo wa kurudi duniani. Usidanganyike. Fuatilia kisa cha tajiri na masikini, roho ya tajiri haikuweza kurudi duniani. (Luka 16:27-31)
Wala, roho hizi(mapepo) siyo malaika walioasi, kwa kuwa wao wametekwa na tayali wako kwenye kamaba zao wakingoja siku ya hukumu (Yuda 1:16,2Petro 2:4)

Swali: Je, mkuu wa mapepo ni nani? Ili kupata jibu fuatana nami.....
Biblia katika kitabu cha Marko 3:22, imeeleza wazi, aliye mkuu wa mapepo. Naye ni Beelzebuli. Hili ni dhahili, kuwa huyu ndiye mkuu wa mapepo na ndiye pepo mkuu.

Je, mapepo yanamfahamu Mungu, yanamchukuliaje?
Mepepo yanafahamu fika kuwa Mungu yupo. Tena yanajua kuwa Mungu anauwezo na nguvu zaidi yao, ndiyo maana humwogopa. (Yakobo 2:19).”Wewe waamuni ya kuwa Mungu ni mmoja; watenad vema.mashetani nao wanaamini na kutetemeka”

Kama vile mapepo yanavyomogopa Mungu na hata kutetemeka, kadharika mtu asiye na roho wa Mungu, huyaogopa mapepo. Je, hujaona mtu anaogopa kulala peke yake ndani, pengine hata mchana huogopa kubaki nyumbani peke yake wengine wanapokuwa hawapo? Hata wanafunzi wa Yesu, kabla ya kumpokea Roho Mtakatifu, walikuwa waoga juu ya pepo. (Mathayo 14:26,Luka 24:37). Hivyo, watu wote, wanapaswa kuokoka na kupokea nguvu ya Roho mtakatifu ili kuwashinda mapepo na kazi zao zote.

Zingatia hili, mapepo yananao uwezo wa kutenda miujiza kupitia watu, vitu na hata wanayama ili kuwadanganya watu na miujiza yao ya uongo (Ufunuo 16:14).

Hakika, kazi za mapepo zikidhibitiwa vilivyo, kazi zote za adui/ shetani zitakuwa zimeshindwa na maangamizi yote ya kipepo hayatapata nafasi tena. Amen.

Je, kuna uhusiano gani kati ya watu/ binadamu na mapepo? Chanzo/asili yake ni nini? Endelea kufuatana nami toleo lijilo.......

Karibuni Eiyer 2013 Mkuu wa chuo MziziMkavu Pasco Lisa Valentine Adiosamigo Rakims Monstgala ........
Tumeshalizungumzia topic kama hii hakuna mpya hapa bonyeza hapa.
https://www.jamiiforums.com/habari-...e-majini-ni-kitu-gani-na-yanataka-nini-2.html

au bonyeza hapa. https://www.google.com/search?clien...jamiiforums.com&affdom=maxthon.com&channel=t5

Samahani sina muda tena wa kyazungumzia mambo ya majini Mkuu Ishmael
 
Last edited by a moderator:
Mhh wala sikai hapa nina haraka kidogo nitarudi baadae
Usiwe na haraka ndugu. Njoo usome na kujifunza tofauti ya Majini katika Ukristo na Uislam. Kwanini kuna tafuki kubwa wakati wengine wanadai kuwa Mungu wa Wakristo na Waislam ni mmoja?

Elimu haina mwisho.
 
Tumeshalizungumzia topic kama hii hakuna mpya hapa bonyeza hapa.
https://www.jamiiforums.com/habari-...e-majini-ni-kitu-gani-na-yanataka-nini-2.html

au bonyeza hapa. https://www.google.com/search?clien...jamiiforums.com&affdom=maxthon.com&channel=t5

Samahani sina muda tena wa kyazungumzia mambo ya majini Mkuu Ishmael

Majini ni mashetani ambao wanafuatana na tamaduni za nchi za kiarabu, lakini pia, majini haya yalikuwa ni mashetani yanayofuatana na maji au mikusanyiko ya maji; kwasababu makao yao makuu yalikuwa majini ukisoma, Ezekieli 29:3-5. Na ndio maana mfalme wa Misri, Farao alikuwa anakwenda kuabudu katika maji, Ukisoma, Ezekieli 32:2-3 inaeleza jinsi Farao alivyotegemea miungu ya katika maji kiasi biblia inamwita joka wa majini.


Kwasababu ya mashetani hao wanaokaa majini, mara nyingi maji katika biblia yamekuwa yakitumika kuonyesha uharibifu, Zaburi 18:16. Ndio maana hata kipindi cha Musa alipokuwa anamfuata Farao ili kuomba ruhusa ya kutoka utumwani, maranyingi, alikuwa akimkuta anatoka au anakwenda majini, Kutoka 7:18; 8:20; Ilikuwa ni desturi ya farao kwenda kuabudu katika mikusanyiko ya maji. Maandiko yameonyesha sana kuhusu mashetani wa baharini, katika Ufunuo 14:31; 20:13, Isaya 27:1, Ayubu 3:8.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom