Je, limbwata lipo?

Je, limbwata lipo?

Bujibuji sikuwa ninaamini haya mambo lakini Wamakonde kutoka Ntwara mpaka Mozambique ni nyoko sana kwa mambo hayo.

Tena washenzi wale wanatumia miti tu. majani, magamba au mizizi na mganga wa kweli anakwambia utanipa asante ukifanikiwa.
Hivi mbaba anaweza kumfanyia mkewe? kama inawezekana itabidi niende mtwara faster.
 
Kwani mpaka leo bado hujawowa Bujibuji
 
Mimi nililetewa hadi mimba nikasamehe, nilishafumania nikasamehe, nilishaitwa majina ya watu katikati ya game nikasamehe.

Sikujua kama ningeweza kuishi bila yule mdada, after six good yrs alipata mwanaume akaniacha nikaweweseka sana mikawa mlevi ni hatari kazini hawanielewi nikakonda kwa mawazo.

Huko alikoenda alitandikwaga hadi akang'olewa jino wengine hawataki ujinga. Akajaribu kurudi kwangu akakuta moyo umekunjamana namuona kama shetani kinyago. Kila nikikumbuka ile hali najiona jinsi nlivokuwaga mjinga.

Usicheze na mapenzi.

Namuomba Mungu hii hali isije ikanirudia tena kwa mwanamke nitayeishi nae.
Kwani bujibuji unaishi mwenyewe?
 
Back
Top Bottom