Kila siku kabla Bunge halijaanza shughuli zake kuna ile dua inasomwaga na Ndugai kabla hajampa nafasi Nkamia, Lusinde, Nchemba, na wengineo kuchangia. Kwenye hiyo dua ya Ndugai kuna Mungu anatajwa humo ambaye nahisi ndiye Mungu wa waTanzania kwani hupelekewa maombi kabla chombo cha wananchi (Bunge) hakijaanza kutekeleza majukumu yake ya kitaifa.
Kuna ubaya gani kwa Chadema na waTanzania wengine kumtumainia huyo Mungu? Au unadhani kuna wenye hatimiliki ya Mungu kama akina Ndugai na kwa wengine ni nongwa? Kama hutaki kumtaja shauri yako ila usiwaonee wivu wengine wanaopenda kumtaja kama akina Ndugai na Chadema pengine wanajua na wameuona ukuu wake kwao.