Equation x
JF-Expert Member
- Sep 3, 2017
- 37,104
- 55,514
Wengi tunakimbilia kuzaa tukiamini huko mbeleni, watoto tunaowazaa watakuja kutusaidia.
Hii inatokana na kutokuwepo kwa kambi za wazee katika huu ukanda wetu, inayopelekea ufikapo uzeeni kukosa mtu wa kukusaidia pale utakapohitaji msaada.
Tumekuwa tukiwazaa watoto, na kuwagharamia kila kitu kwa gharama kubwa, iwe chakula, mavazi, elimu n.k.
Ila wakishakuwa wakubwa, wanakuwa na miji yao na wengine wanakuwa hawana msaada kwa wazazi wao, na kuishia kuwatelekeza.
Sasa najiuliza, kuna umuhimu gani wa kuzaa na kujinyima vitu mbalimbali ikiwapo uwekezaji mbalimbali, kwa ajili ya kumgharamikia mtoto asiyekuja kuwa na msaada na wazazi?
Imekuwa, kuwa na watoto katika familia ni mzigo mkubwa sana inayoathiri uchumi wa wana familia.
Hii imeathiri maisha yetu ya kila siku, ndio maana wengi wetu hatuendi kutalii mbuga za wanyama au kwenda nchi mbali mbali, kwa sababu ya fedha kuwekeza kwa watoto.
Sasa najiuliza, kuwa na watoto kwenye ndoa ni hitaji la msingi?
Hii inatokana na kutokuwepo kwa kambi za wazee katika huu ukanda wetu, inayopelekea ufikapo uzeeni kukosa mtu wa kukusaidia pale utakapohitaji msaada.
Tumekuwa tukiwazaa watoto, na kuwagharamia kila kitu kwa gharama kubwa, iwe chakula, mavazi, elimu n.k.
Ila wakishakuwa wakubwa, wanakuwa na miji yao na wengine wanakuwa hawana msaada kwa wazazi wao, na kuishia kuwatelekeza.
Sasa najiuliza, kuna umuhimu gani wa kuzaa na kujinyima vitu mbalimbali ikiwapo uwekezaji mbalimbali, kwa ajili ya kumgharamikia mtoto asiyekuja kuwa na msaada na wazazi?
Imekuwa, kuwa na watoto katika familia ni mzigo mkubwa sana inayoathiri uchumi wa wana familia.
Hii imeathiri maisha yetu ya kila siku, ndio maana wengi wetu hatuendi kutalii mbuga za wanyama au kwenda nchi mbali mbali, kwa sababu ya fedha kuwekeza kwa watoto.
Sasa najiuliza, kuwa na watoto kwenye ndoa ni hitaji la msingi?