Je kuwaota ndugu au marafiki waliofariki ndivyo wanavyotokea au ni tofauti na kutokewa

Pole sana ndugu. Heri yako wewe inakutokea ndotoni tu. Kuna mtu wangu wa karibu sana aliwahi kutokewa na tatizo kama lako lakini tofauti yake ni kwamba yeye mzazi wake aliyekuwa amefariki miezi kadhaa nyuma alikuwa akimtokea live kabisa (kwa maelezo yake) akiwa barabarani, darasani n.k. na kumwita, kuongea nae, kumnyooshea mkono kisha kutoweka ghafla. Hiyo hali iliendelea kumtokea kama mara nane hivi ndani ya miezi mitatu. Bahati nzuri kuna mzee mmoja hivi mchungaji (kwa sasa ni marehemu) ndiye siku moja alikwenda nyumbani alipokuwa akiishi huyo ndugu yangu na kumwombea "kirafiki kabisa" kwa mwenyezi Mungu na tangu siku hiyo hilo tatizo halikumrudia tena na leo hii ni zaidi ya miaka kumi. Mchungaji alisema hayo ni mashetani yaliyokuwa yakija yakiwa katika sura ya marehemu na kumtesa huyo ndugu yetu. Kwa hiyo nionavyo kama wewe ni mkristo au muislam tafuta kiongozi wako wa dini akuombee tu jambo hilo. Binafsi ni moja ya mambo ambayo yalinishangaza sana na ndiyo maana nionapo watu wanabisha au wanakuwa na mashaka juu ya uwepo wa Mungu pamoja na madhambi yangu yote uwa napata woga sana. Natumaini mwenyezi Mungu ataibariki hii testimony yangu kwa wasomaji wote maana sijawahi kupata mahali pengine pa kuitolea au ujasiri wa kuiweka wazi kwa watu wengine.
Nimebarikiwa na testimony
 
Tatizo la kisaikolojia wakati mwingine ni very tricky. Kupona kunaweza kutegemea akili za mgonjwa jinsi zilivyo tayari kuamini na kupokea matibabu. Siyo kwamba nakupinga mambo ya kuombewa na mizimu lakini nataka tu kutahadharisha kuwa tatizo linaweza kuangaliwa kwa njia nyingine pia.
Nashukuru kwamba angalau ume reserve imani fulani juu ya testimony yangu. Bahati nzuri ni kwamba wengine hatuna tabia ya kuleta habari za uzushi isipokuwa kueleza kwa nia nzuri kile tulichowahi kupitia maishani ili pengine kiweze kuwa msaada kwa wengine pamoja na kwamba sometime we differ depending on the nature of indoctrination and social context we have been subjected to. All in all we are all here just to help each other out of the problems or plight surrounding us.
 
Back
Top Bottom