Je kuwaota ndugu au marafiki waliofariki ndivyo wanavyotokea au ni tofauti na kutokewa

harder king

JF-Expert Member
Jan 21, 2017
3,970
6,898
Habari za weekend wana JF

Poleni na majukumu ya wiki na karibuni kwenye harakati za weekend za kutumia sehemu ya kile ulichopata kwa hizi siku5

Nije kwenye mada.
My story; hii sio simulizi bali ni kitu kinachoniandama karibu kila siku.

Ipo hivi zaidi ya miaka mitatu iliyopita nilimpotenza babu na bibi ambao ndio waliokua walezi wetu baada ya anguko la familia yetu ya(baba na mama) kutengana na kutuacha kwa wazazi wa baba ambao walitulea kwa kwa maadili mema kabisa..

Ila wazazi wetu halisi walikuja rudiana kabla wazee wao(babu na bibi) yetu kuondoka duniani, baada ya sisi kufikia umri wa kujitegemea na kuwapigania mpaka wakarudiana.

Miezi mitatu iliopita nilimpotenza tena baba yangu kipenzi.
Tatizo ni kwamba tangu baba atutoke nimekua nikionana nae ndotoni tena sasa sio yeye tu mpaka babu na bibi..tena kwenye maisha ya kawaida kabisa tuliyowai kuishi nao pale kijijini,hizi ndoto zimeniandama hadi nashindwa kuelewa kama ni tatizo au ni hali ya kawaida?

Kingine ni kwamba siku nikilala nikiwa nimekunywa mbili tatu hili tatizo la kuota sikutani nalo kabisa labda mara chache sana linijie alfajir.

Sasa kingine kilichonisukuma kuja kuwauliza humu ni baada ya jana kwenda nyumbani nikiwa sijagusa maji kabisa..
Nilikaa nikichek movie mpaka saa7 usiku ndio nikaenda kulala,na nilifanya makusudi nikijua nikichelewa kulala sintaotA chochote..

Kweli sikuota ila nilikuja kushtuta saa9;30 alfajiri na usingizi ukakata.
Lakini ilipofika saa11 nilipitiwa na usingizi ulioambatana na ndoto, daah!
Nilimuota tena baba na hawamu hii afya yake imedhohofu,,ni kama nilikua nimetoka safarini na nimefika kijijini kuwaona wazazi
Nilipofika kabla sijaingia seblen nikawaona ndugu wa baba kama wawil wamekaa seblen,lakin ghafla alitokea mtu nyuma yangu akataja jina la baba akitaka kujua kama ameamka.

Lakin walimjibu bado hajaamka,mara nikamuona baba anatoka chumbani akiwa amechoka na afya yake ikiwa mbaya na ghafla akaanguka pale sebleni, wakati huo mimi bado nimesimama nje nikiwa kama sijielewi.

Wale ndugu walijitaid kumuinua lakini ilishindikana.niliingia ili kumuinua baba alinipa mkono kama ishara ya kutaka nimuinue bila kutoa sauti,nilimuinua lakini kabla hajasimama vizuri tuliteleza tukaanguka maana sakafu ilionekana kama ilimwagiwa maji baba akiwa amekaa chini nilikumbatia kwa uchungu nikiwa nimepiga magoti sakafuni huku nikiwa na maumivu makali moyoni juu ya hali ya baba yangu nikamwambia kwa nguvu umepatwa na nini baba yangu !.

Ghafla nikazinduka usingizin ,Cha kushanga ile hali ya kuumia baada ya kuona hali ya baba ndotoni bado nilikua nayo..mapigo yamoyo yalikua juu ad nikawa nayasikia.Nilipoikumbuka ile ndoto machozi yalitoka kwa kasi.kiukweli tangia haya mauzauza ya kuotaota yanianze sijawai kuumia kama nilivyoumia leo.

Nilipoangalia mUda kumbe sikulala Hata dakika 20 tangu ule usingizi na ndoto ziniianze.

Nikaamka nikajiandaa kwenda kanisani japo mimi sio mhudhuriaji mzur wa ibada ila niliona niende kabla ya kwenda kazini maana sikuwa na amani kabisa.

Wana JF hilo ndilo tatizo linaloniandama sijui kama kuna waliowai kukutana na kitu kama hiki na kama wapo wanisaidie cha kufanya pia kama umewai kusikia kwa waliopitia ninayoyapitia uniambie walisaidikaje.


Nb.mm sio muhumini wa imani za kidunia(kichawi,waganga wa jadi) tangu nitambue mema na mabaya.. naomba mtakaonisaidia msiingie huko sana..

Natanguliza shukrani!
 
Pole sana ndugu. Heri yako wewe inakutokea ndotoni tu. Kuna mtu wangu wa karibu sana aliwahi kutokewa na tatizo kama lako lakini tofauti yake ni kwamba yeye mzazi wake aliyekuwa amefariki miezi kadhaa nyuma alikuwa akimtokea live kabisa (kwa maelezo yake) akiwa barabarani, darasani n.k. na kumwita, kuongea nae, kumnyooshea mkono kisha kutoweka ghafla. Hiyo hali iliendelea kumtokea kama mara nane hivi ndani ya miezi mitatu. Bahati nzuri kuna mzee mmoja hivi mchungaji (kwa sasa ni marehemu) ndiye siku moja alikwenda nyumbani alipokuwa akiishi huyo ndugu yangu na kumwombea "kirafiki kabisa" kwa mwenyezi Mungu na tangu siku hiyo hilo tatizo halikumrudia tena na leo hii ni zaidi ya miaka kumi. Mchungaji alisema hayo ni mashetani yaliyokuwa yakija yakiwa katika sura ya marehemu na kumtesa huyo ndugu yetu. Kwa hiyo nionavyo kama wewe ni mkristo au muislam tafuta kiongozi wako wa dini akuombee tu jambo hilo. Binafsi ni moja ya mambo ambayo yalinishangaza sana na ndiyo maana nionapo watu wanabisha au wanakuwa na mashaka juu ya uwepo wa Mungu pamoja na madhambi yangu yote uwa napata woga sana. Natumaini mwenyezi Mungu ataibariki hii testimony yangu kwa wasomaji wote maana sijawahi kupata mahali pengine pa kuitolea au ujasiri wa kuiweka wazi kwa watu wengine.
 
Kuna maagano ya mababu na nguvu za giza yanakutafuta ni ipo siku utajua ni nini hasa!

Hata hivyo mambo ya roho humalizwa na roho nyingine yenye nguvu,
Tafuta msaada wa maombi yenye nguvu ya Damu YESU and you will be disconnected.
Nashukuru sana mkuu
 
Pole sana ndugu. Heri yako wewe inakutokea ndotoni tu. Kuna mtu wangu wa karibu sana aliwahi kutokewa na tatizo kama lako lakini tofauti yake ni kwamba yeye mzazi wake aliyekuwa amefariki miezi kadhaa nyuma alikuwa akimtokea live kabisa (kwa maelezo yake) akiwa barabarani, darasani n.k. na kumwita, kuongea nae, kumnyooshea mkono kisha kutoweka ghafla. Hiyo hali iliendelea kumtokea kama mara nane hivi ndani ya miezi mitatu. Bahati nzuri kuna mzee mmoja hivi mchungaji (kwa sasa ni marehemu) ndiye siku moja alikwenda nyumbani alipokuwa akiishi huyo ndugu yangu na kumwombea "kirafiki kabisa" kwa mwenyezi Mungu na tangu siku hiyo hilo tatizo halikumrudia tena na leo hii ni zaidi ya miaka kumi. Mchungaji alisema hayo ni mashetani yaliyokuwa yakija yakiwa katika sura ya marehemu na kumtesa huyo ndugu yetu. Kwa hiyo nionavyo kama wewe ni mkristo au muislam tafuta kiongozi wako wa dini akuombee tu jambo hilo. Binafsi ni moja ya mambo ambayo yalinishangaza sana na ndiyo maana nionapo watu wanabisha au wanakuwa na mashaka juu ya uwepo wa Mungu pamoja na madhambi yangu yote uwa napata woga sana. Natumaini mwenyezi Mungu ataibariki hii testimony yangu kwa wasomaji wote maana sijawahi kupata mahali pengine au ujasiri wa kuitolea kwa watu wengine.
Dah! Hii dunia kweli bila Mungu ni bure..ubarikiwe mkuu.
 
Kihalisia hawatokei.ila ni kumbukumbu kwa wapendwa wetu au maadui zetu mtu yeyote kama ulikua nae karibu sana au kuna jambo alikutendea na akafa na ktk hali ya kawaida akili yako ikakataa kukubali kuwa amekufa mara nyingi utateta nae ktk njozi bila shaka huo nao pia ni ugonjwa waone madaktari wa akili
 
Kihalisia hawatokei.ila ni kumbukumbu kwa wapendwa wetu au maadui zetu mtu yeyote kama ulikua nae karibu sana au kuna jambo alikutendea na akafa na ktk hali ya kawaida akili yako ikakataa kukubali kuwa amekufa mara nyingi utateta nae ktk njozi bila shaka huo nao pia ni ugonjwa waone madaktari wa akili
nilitaka niandike hivi ila umeniwahi.aliyekufa kafa hizo nyingine ni kumbukumbu tu ukizifuta kichwani ukakubaliana na hali halisi hutaota tena
 
Pole mkuu kwa yanayo kusibu, kwa hiyo ndoto yako ya mwisho kuamka na maumivu sidhani kama hiyo ni ndoto ya kawaida.. Kutakuwa na ualisia mkubwa

Nina rafiki angubalikuwa ananiadidhia majanga ya kama hivi, yeye alikuwa ana ota ndoto ya aina moja, kila siku anaota anakimbizwa na watu watatu kwenye mchanga mwingi sana kila alipostuka ndotoni miguu ilikuwa na vumbi na jasho linamtoka kabisa kama ametoka kukimbia kweli

Baadae baada ya huyu rafk angu kukomaa na imani yake sana alikuja kuota tena lakni safari hiyo aliota anaojiana na wale watu wanao mkimbizaga, alikuwa akiwauliza maswali, kwanini mnanifata mimi kila siku? Kwann kila siku nawaota nyie? na wale watu walimjibu, sisi tumetumwa tuje kukuua kwasababu wewe unaongoza darasani, lakini tumeshindwa kukuua hivyo tutakuacha kwa muda

Hii story ni ndefu siwez kumaliza yote lakini point yangu ilikuwa ni kwenye ndoto hapo!

Ndoto za kuota alafu unamka unaisi kama kweli! Hiyo sio ndoto, ilikuwa ni jambo la kweli aidha walozi wanakuchezea live live au kuna maagano wazee waliweka juu yako kwaiyo wanaona wakufate ile mubashara kabisa muyajenge
 
Pole sana ndugu. Heri yako wewe inakutokea ndotoni tu. Kuna mtu wangu wa karibu sana aliwahi kutokewa na tatizo kama lako lakini tofauti yake ni kwamba yeye mzazi wake aliyekuwa amefariki miezi kadhaa nyuma alikuwa akimtokea live kabisa (kwa maelezo yake) akiwa barabarani, darasani n.k. na kumwita, kuongea nae, kumnyooshea mkono kisha kutoweka ghafla. Hiyo hali iliendelea kumtokea kama mara nane hivi ndani ya miezi mitatu. Bahati nzuri kuna mzee mmoja hivi mchungaji (kwa sasa ni marehemu) ndiye siku moja alikwenda nyumbani alipokuwa akiishi huyo ndugu yangu na kumwombea "kirafiki kabisa" kwa mwenyezi Mungu na tangu siku hiyo hilo tatizo halikumrudia tena na leo hii ni zaidi ya miaka kumi. Mchungaji alisema hayo ni mashetani yaliyokuwa yakija yakiwa katika sura ya marehemu na kumtesa huyo ndugu yetu. Kwa hiyo nionavyo kama wewe ni mkristo au muislam tafuta kiongozi wako wa dini akuombee tu jambo hilo. Binafsi ni moja ya mambo ambayo yalinishangaza sana na ndiyo maana nionapo watu wanabisha au wanakuwa na mashaka juu ya uwepo wa Mungu pamoja na madhambi yangu yote uwa napata woga sana. Natumaini mwenyezi Mungu ataibariki hii testimony yangu kwa wasomaji wote maana sijawahi kupata mahali pengine au ujasiri wa kuitolea kwa watu wengine.
Haya yote siyo miujiza bali na mawazo. Ubongo wa mwanadamu ni kitu complex sana na mawazo unayowaza yanaweza kugeuka kama kitu halisi. Yeye alikuwa anaona anakutana nao live kumbe ni mawazo yake tu. Na huyu nae anaota ndoto. Anaonekana anawafikiria sana wapendwa wake na ndiyo maana akinywa pombe haoti na siyo kuwa marehemu wanaogopa pombe.
 
Haya yote siyo miujiza bali na mawazo. Ubongo wa mwanadamu ni kitu complex sana na mawazo unayowaza yanaweza kugeuka kama kitu halisi. Yeye alikuwa anaona anakutana nao live kumbe ni mawazo yake tu. Na huyu nae anaota ndoto. Anaonekana anawafikiria sana wapendwa wake na ndiyo maana akinywa pombe haoti na siyo kuwa marehemu wanaogopa pombe.
Pengine uko sawa. Na je, kwa nini hilo tatizo liliisha mara tu baada ya kuombewa na leo hii ni zaidi ya miaka kumi bila kumtokea wakati lilikuwa likimtokea mara kwa mara kama nilivyoeleza?
 
Pengine uko sawa. Na je, kwa nini hilo tatizo liliisha mara tu baada ya kuombewa na leo hii ni zaidi ya miaka kumi bila kumtokea wakati lilikuwa likimtokea mara kwa mara kama nilivyoeleza?
Hapo ndiyo niliposema ubongo ni kitu complex sana. Kuombewa kunajenga imani. Imani inabadili ubongo unavyowaza.
 
Hapo ndiyo niliposema ubongo ni kitu complex sana. Kuombewa kunajenga imani. Imani inabadili ubongo unavyowaza.
Mwanzo alikuwa akishauriwa kutumia dawa fulani za hospitali akiamini kuwa tatizo litaisha lakini likawa linaendelea. Ina maana hapo alikuwa hajawa na imani ya kutosha?
 
Ngoja nijaribu kykueleza kulingana na ufahamu wangu

Kuota ndoto ya aina moja au yenye maudhui ya kufanana (ukiota hivyo kwanza kabisa hiyo ndoto sio ya kuicha iende kuna ujumbe muhimu sana inabidi uipate )

Pili ndoto zinakuja kwa sababu kadhaa
1.kutoka kwa Mungu
2.kutoka kwa shetani
3.kuchoka kwa kazi nyingi
Ila hiyo ya kwako inaweza kuwa miongoni mwa hizo sababu mbili za mwanzo

Kama watu waliokufa wanakutokea kwenye ndoto na kuna mazungumzo mnayafanya kati yako na hao waliokwisha kufa inamaana kuna aina ya mambo ambayo roho ya uyo unayomwota alikua anayafanya sasa ndo hiyo roho imekuja kukushawishi ufanye (kua makini )

Kama roho ilikua inatokana na aina ya makubaliano (maagano/matambiko) waliyo yafanya hao waliokufa basi jua hiyo roho inakufatilia kwa kua na wewe ni either sehemu ya makubalianl katika hayo makubaliano au jina lako lilitajwa kwenye hayo makubaliano


Kwa sababu hiyo kuwa makini sana na aina ya maongezi mnayokua mnafanya wewe na hao waliokwisha kufa (hapa kutakua na swali )

Je huwa wanazungumza nini na we we ?

Nikijaribu kupita na hii ndoto ya mwisho uliyoeleza kwamba umemona baba yako akiwa huko hoi na tena AKAANGUKA NAWE UKAENDA kumwamsha lakini ALIKUVUTA nawe UKAANGUKA pamoja Nate hiyo possibly ikawa ishara kwamba kuna vitu ambavyo alikua anafanya mzee wako nawe pia unafanya sasa /utavifanya ila vitu hivyo haviwezi kwenda Mbele vitaanguka/vitakwama au vitaharibika sasa njia ni moja tu ambayo inaweza Ku solve hayo mambo ni kuomba toba kwa Mungu na kuomba rehema zake kwa kufuta aina zote za maagano ambazo we we uliingizwa au ulishiriki na hao Ndugu zako waliokufa na wanakuja kukushawishi uendelee au utekeleze mambo take

Hiyo ilikua upande mmoja wa ndoto kwa upande mwingine sio kila ndoto inayohusishwa na wafu ni mbaya zipo ambazo watu huwa wanapewa taarifa mfano no yesu alipokua akisita kupita njia ya msalaba Musa nabii na Elia Yule mtu WA MUngu walimtokea kufanya nae mazungumzo kumtia moyo




Sasa kwa kua hii ndoto yako inalalia sana kwenye kipengele hicho nilicho eleza kwanza basi hiki kipengele cha pili sio muhimu sana

Nimejaribu kutoa mwanga nilionao katika hili swala ila pia nakupa na uelekeo ambapo kuna maelezo mengi yahusuyo ndoto zinazohusisha watu walikufa tafuta audio/video za semina ya mwakasege 2018 mkoani mbeya hii ameeleza kwa kirefu sana nadhani itakusaidia sana
 
Failure to let it go.. ukaribu, utegemezi nk, ndio unafanya watu wengi tushindwe kukubaliana na ukweli kuwa wapendwa wetu hatukonao tena, na ukishindwa tu Lazima utapata shida.
 
Kamba tu hizi hakuna chochote.

Wabongo bana mnapenda kuja na tu stori twa ajabu ajabu ona sasa, Matapeli nao washaingilia uzi na kuanza kuchafua hali ya hewa.
 
Ngoja nijaribu kykueleza kulingana na ufahamu wangu

Kuota ndoto ya aina moja au yenye maudhui ya kufanana (ukiota hivyo kwanza kabisa hiyo ndoto sio ya kuicha iende kuna ujumbe muhimu sana inabidi uipate )

Pili ndoto zinakuja kwa sababu kadhaa
1.kutoka kwa Mungu
2.kutoka kwa shetani
3.kuchoka kwa kazi nyingi
Ila hiyo ya kwako inaweza kuwa miongoni mwa hizo sababu mbili za mwanzo

Kama watu waliokufa wanakutokea kwenye ndoto na kuna mazungumzo mnayafanya kati yako na hao waliokwisha kufa inamaana kuna aina ya mambo ambayo roho ya uyo unayomwota alikua anayafanya sasa ndo hiyo roho imekuja kukushawishi ufanye (kua makini )

Kama roho ilikua inatokana na aina ya makubaliano (maagano/matambiko) waliyo yafanya hao waliokufa basi jua hiyo roho inakufatilia kwa kua na wewe ni either sehemu ya makubalianl katika hayo makubaliano au jina lako lilitajwa kwenye hayo makubaliano


Kwa sababu hiyo kuwa makini sana na aina ya maongezi mnayokua mnafanya wewe na hao waliokwisha kufa (hapa kutakua na swali )

Je huwa wanazungumza nini na we we ?

Nikijaribu kupita na hii ndoto ya mwisho uliyoeleza kwamba umemona baba yako akiwa huko hoi na tena AKAANGUKA NAWE UKAENDA kumwamsha lakini ALIKUVUTA nawe UKAANGUKA pamoja Nate hiyo possibly ikawa ishara kwamba kuna vitu ambavyo alikua anafanya mzee wako nawe pia unafanya sasa /utavifanya ila vitu hivyo haviwezi kwenda Mbele vitaanguka/vitakwama au vitaharibika sasa njia ni moja tu ambayo inaweza Ku solve hayo mambo ni kuomba toba kwa Mungu na kuomba rehema zake kwa kufuta aina zote za maagano ambazo we we uliingizwa au ulishiriki na hao Ndugu zako waliokufa na wanakuja kukushawishi uendelee au utekeleze mambo take

Hiyo ilikua upande mmoja wa ndoto kwa upande mwingine sio kila ndoto inayohusishwa na wafu ni mbaya zipo ambazo watu huwa wanapewa taarifa mfano no yesu alipokua akisita kupita njia ya msalaba Musa nabii na Elia Yule mtu WA MUngu walimtokea kufanya nae mazungumzo kumtia moyo




Sasa kwa kua hii ndoto yako inalalia sana kwenye kipengele hicho nilicho eleza kwanza basi hiki kipengele cha pili sio muhimu sana

Nimejaribu kutoa mwanga nilionao katika hili swala ila pia nakupa na uelekeo ambapo kuna maelezo mengi yahusuyo ndoto zinazohusisha watu walikufa tafuta audio/video za semina ya mwakasege 2018 mkoani mbeya hii ameeleza kwa kirefu sana nadhani itakusaidia sana
Upo sahihi Mtumishi wa Mungu.
 
  • Thanks
Reactions: a45
Mwanzo alikuwa akishauriwa kutumia dawa fulani za hospitali akiamini kuwa tatizo litaisha lakini likawa linaendelea. Ina maana hapo alikuwa hajawa na imani ya kutosha?
Tatizo la kisaikolojia wakati mwingine ni very tricky. Kupona kunaweza kutegemea akili za mgonjwa jinsi zilivyo tayari kuamini na kupokea matibabu. Siyo kwamba nakupinga mambo ya kuombewa na mizimu lakini nataka tu kutahadharisha kuwa tatizo linaweza kuangaliwa kwa njia nyingine pia.
 
Back
Top Bottom