Je, kutumia simu ya mkeo pia ni kosa kisheria, maana haijasajiliwa kwa jina lako?

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Feb 24, 2012
5,011
9,876
Msanii wa Mashairi ya kuongea,’Spoken words poerty, Malle Hanzi, ameandika kuhoji sheria ya makosa ya mtandao ilivyo. Amehoji hili baada ya Msanii wa kuchekesha kushitakiwa kwa kosa la kutumia laini isiyo sajiliwa kwa jina lake.

Amehoji kama kutumia laini isiyosajiliwa kwa jina lako kuna tofauti na kuendesha gari lisilosajiliwa kwa jina lako

Ameendelea kuhoji kuwa, Je, linakuwa kosa hata kama hakuna jinai yoyote uliyotenda kwa kutumia kitu kisicho chako au ni kosa tu kutumia kisichochako? Amefaninisha na gari kuwa unaweza kukamatwa kwa kupewa kosa la kuendesha gari lisilo lako hata kama haujavunja sheria au kusababisha ajali?

Je, inatosha kushtakiwa kwa kutumia laini isiyo na jina lako hata kama haujafanya uhalifu wowote na laini hiyo? Je, ikiwa mtu umeishiwa salio hautaruhusiwa kutumia simu ya rafiki yako au mpenzi wako kwa muda huo?

Amemaliza kwa sentensi ya kishairi kuwa “Kuna muda tunatunga sheria mpaka sheria zenyewe zinatushangaa”
 
Vip ukifanya uhalifu mfano umeua na ushaid ukaonyesha kua marehem kabla hujamuua ulimpigia cm ukakamatwa baada ya kwenda maakaman ukasema Sio wewe ulie husika sababu line ya cm Sio yako Apo lazima ushinde kesi vip kwa mfano huu huon Kama serekal Ina haki ya kuhakikisha kila mtu anatumia line yake?
Msanii wa Mashairi ya kuongea,’Spoken words poerty, Malle Hanzi, ameandika kuhoji sheria ya makosa ya mtandao ilivyo. Amehoji hili baada ya Msanii wa kuchekesha kushitakiwa kwa kosa la kutumia laini isiyo sajiliwa kwa jina lake.

Amehoji kama kutumia laini isiyosajiliwa kwa jina lako kuna tofauti na kuendesha gari lisilosajiliwa kwa jina lako

Ameendelea kuhoji kuwa, Je, linakuwa kosa hata kama hakuna jinai yoyote uliyotenda kwa kutumia kitu kisicho chako au ni kosa tu kutumia kisichochako? Amefaninisha na gari kuwa unaweza kukamatwa kwa kupewa kosa la kuendesha gari lisilo lako hata kama haujavunja sheria au kusababisha ajali?

Je, inatosha kushtakiwa kwa kutumia laini isiyo na jina lako hata kama haujafanya uhalifu wowote na laini hiyo? Je, ikiwa mtu umeishiwa salio hautaruhusiwa kutumia simu ya rafiki yako au mpenzi wako kwa muda huo?

Amemaliza kwa sentensi ya kishairi kuwa “Kuna muda tunatunga sheria mpaka sheria zenyewe zinatushangaa”
 
Ni kosa kisheria! kumbuka fingerprint za mkeo siyo zako!
hivyo ni kosa ukikamatwa unashughulikiwa
 
Vip ukifanya uhalifu mfano umeua na ushaid ukaonyesha kua marehem kabla hujamuua ulimpigia cm ukakamatwa baada ya kwenda maakaman ukasema Sio wewe ulie husika sababu line ya cm Sio yako Apo lazima ushinde kesi vip kwa mfano huu huon Kama serekal Ina haki ya kuhakikisha kila mtu anatumia line yake?
Umeambiwa kama hujafanya uhalifu, mbona husomi maelezo unaanza kutoa hoja kwa mawazo yako!
 
Back
Top Bottom