Je, kuna ukweli kuhusu Phobia na Mental Disorders?

Je, kuna ukweli kuhusu Phobia na Mental Disorders?

Damaso

JF-Expert Member
Joined
Jul 18, 2018
Posts
6,148
Reaction score
10,571
Juzi Jumatatu nilipata taarifa kuwa kuna swahiba yangu alikuwa amelazwa pale hospitali ya Kanda ya Bugando ikanibidi niende kumjulia japo hali. Nilifika salama na tukazungumza mengi sana kuhusu maendeleo ya afya yake, tukacheka na kufurahi sana, namna bora ya kumpa uchangamfu mgonjwa maana alikuwa ana dozi yake ya sindano takribani 10 hivi.
images - 2026-04-08T024751.415.jpeg

Sasa pembeni ya kitanda cha swahiba alikuwepo dogo kama miaka kati ya 18 mpaka 20 hivi, tokea nilipofika huyu dogo alikuwa anaongea kisha anasita na kuweka tusi huku akisindikizia na ishara ya kidole cha kati. Matusi hayakuwa mepesi kwani alikuwa anatoa matusi heavyweight.
images - 2026-04-08T024710.840.jpeg

Ikanibidi niulize kuwa mbona ndugu wa kijana hawamuelekezi kuwa anakosea? Au kukemea tabia hiyo? Nikaambiwa kuwa kijana anaumwa ugonjwa wa Tourette syndrome, kimoyo moyo nikajisemea hizi mambo za Instagram pamoja na TikTok.
images - 2026-04-08T024758.938.jpeg

Nikajisogeza karibu na dogo, nikamsalimia na kumpa pole ila nikapokelewa na tusi la mzazi wangu wa kike pamoja na kidole cha kati. DAAH nikajipa moyo kuwa labda kweli ugonjwa wake ni mkali sana kiasi hicho. Nikamjibu nashukuru sana, dogo akajaa tena kwenye mfumo ananipa tusi jingine kubwa zaidi. Ahh Kimoyomoyo nikasema huyu dogo ni wangu.
What-is-claustrophobia-750x500.jpg

Katika ulimwengu wa leo uliosheheni sayansi na teknolojia ya hali ya juu, kuna jambo moja la kushangaza: ongezeko la kile kinachoitwa matatizo ya kisaikolojia na kihisia. Zamani, mtu alipokuwa na hofu ya kitu, aliambiwa “jikaze!” kama unaogopa giza basi ndio utatumwa kufuata chumvi gizani ukutane na Nsyuka vizuri ama Shumileta kabsa.
images - 2026-04-08T024857.538.jpeg

Huyu dogo alikuwa mpuuzi sana, kwa sababu moja niliamua kuanza naye LIGI ya kutusi huku nikipiga kwenye mshono. Nilimpiga tusi moja dogo akaguna na kukaa kimya kabsa, nikamuuliza, huu ugonjwa wako wa Tourette umeanza lini?
images - 2026-04-08T024932.301.jpeg

Janja akaniambia kuwa yeye hana ugonjwa wala disorder yoyote zaidi disorder ya Tourette syndrome, ila ni vile ameishi na kukulia sana kwenye mazingira ambayo matusi ni Kiunganishi ila pia ni Kivumishi kikuu. Na alipofika Bugando, alikutana na Daktari mmoja raia wa Italia ndiye aliyemwambia kuwa anasumbuliwa na Tourette Syndrome.
images - 2026-04-08T024954.670.jpeg

Katika dunia ya sasa je, kweli tunapiga hatua mbele au tunazidisha mambo yasiyo na msingi? Leo unaweza kukutana na mtu mwenye hofu ya kutazama maji, yaani maji?! mwingine anaogopa majani au matawi ya miti, na mwingine kabisa ana hofu ya nywele!
fruit-phobia-causes-symptoms-and-overcoming-the-fear-of-fruits.webp

Wataalamu watasema tunagundua na kuelewa zaidi afya ya akili kadiri siku zinavyosonga, jambo ambalo ni jema kabisa. Lakini kwa upande mwingine, jamii imeanza kuzoea tabia fulani hadi kushindwa kutofautisha kati ya ugonjwa halisi na mazoea ya mazingira.

Mfano hai ni yule kijana hospitalini anayedaiwa kuwa na Tourette, lakini ukikaa naye kwa dakika chache unagundua kuwa anachofanya ni matokeo ya mazingira aliyokulia—mahali ambapo matusi ni lugha ya kawaida kama “salamu”. Mwishoni dogo nilichapa tusi moja nikaona anatoa machozi nikamwambia hata mimi pia nina Tourette Syndrome..
images - 2026-04-08T024758.938.jpeg

Swali linabaki: je, tunatibu matatizo halisi au tunatengeneza majina mapya kwa tabia za kawaida? Wakati mwingine inaonekana kama dunia imeamua kuvaa miwani ya “diagnosis” kila mahali. Ukikohoa mara mbili—labda una “something syndrome”! Ukiwa haupendi watu wa upinde basi unapewa jina Homophobia, Ukifanya kazi na ukachoka—inaweza kuwa “emotional burnout disorder”.
images - 2026-04-08T024710.840.jpeg

Ni muhimu kutambua kwamba afya ya akili ni jambo nyeti na halipaswi kubezwa. Hata hivyo, tusipokuwa makini, tutafika mahali ambapo kila tabia ya kawaida itahitaji jina la kitaalamu. Na hapo ndipo dunia itakapogeuka kuwa ucheshi mkubwa—ambapo kuogopa jua kutakuwa kawaida kuliko kufurahia mwanga wake.
 
Bandiko zuri tamu kusoma halichoshi
Mie naogopaga kusoma magazeti ila hili nimelisoma lote

Hivi mkuu mfano mimi nachukia kuona vitu visivyo pangwa vizuri mfano nikaingia ndani nikaona vitu vimezagaa zagaa hua najisikia hasira sipendi kuona mavitu ya merundikana hovyo bila mpangilio je huo nao ni ugonjwa?

Naweza kurudi kazin nikikuta hali kama hiyo siwezi kulala bila kuweka sawa
Niliwahi kwenda ugenini nikakuta watuwa hapo wameweka vituu vimezagaa sikuwezi kuhimili kukaa kwa amani nilikua sina raha mpka nikafanya usafi kwanza ndio nikapata amani
Yaan mazingira kama hayo hua najisikia vibaya kuliko mtu anavyoweza kudhani je hii nayo ni shida?
 
Bandiko zuri tamu kusoma halichoshi
Mie naogopaga kusoma magazeti ila hili nimelisoma lote

Hivi mkuu mfano mimi nachukia kuona vitu visivyo pangwa vizuri mfano nikaingia ndani nikaona vitu vimezagaa zagaa hua najisikia hasira sipendi kuona mavitu ya merundikana hovyo bila mpangilio je huo nao ni ugonjwa?

Naweza kurudi kazin nikikuta hali kama hiyo siwezi kulala bila kuweka sawa
Niliwahi kwenda ugenini nikakuta watuwa hapo wameweka vituu vimezagaa sikuwezi kuhimili kukaa kwa amani nilikua sina raha mpka nikafanya usafi kwanza ndio nikapata amani
Yaan mazingira kama hayo hua najisikia vibaya kuliko mtu anavyoweza kudhani je hii nayo ni shida?
Katika ulimwengu wa leo uliosheheni sayansi na teknolojia ya hali ya juu, kuna jambo moja la kushangaza: ongezeko la kile kinachoitwa matatizo ya kisaikolojia na kihisia. Zamani, mtu alipokuwa na hofu ya kitu, aliambiwa “jikaze!” kama unaogopa giza basi ndio utatumwa kufuata chumvi gizani ukutane na Nsyuka vizuri ama Shumileta kabsa.
 
Katika ulimwengu wa leo uliosheheni sayansi na teknolojia ya hali ya juu, kuna jambo moja la kushangaza: ongezeko la kile kinachoitwa matatizo ya kisaikolojia na kihisia. Zamani, mtu alipokuwa na hofu ya kitu, aliambiwa “jikaze!” kama unaogopa giza basi ndio utatumwa kufuata chumvi gizani ukutane na Nsyuka vizuri ama Shumileta kabsa.
Kwahiyo na mimi nijikaze kukaa kwenye mazingira yasiyopangwa vizuri?
Nakuhakikishia ukitaka nichanganyikiwe wewe weka vitu vururu vururu aisee nachukiaaaaaa🙌
 
Katika ulimwengu wa leo uliosheheni sayansi na teknolojia ya hali ya juu, kuna jambo moja la kushangaza: ongezeko la kile kinachoitwa matatizo ya kisaikolojia na kihisia. Zamani, mtu alipokuwa na hofu ya kitu, aliambiwa “jikaze!” kama unaogopa giza basi ndio utatumwa kufuata chumvi gizani ukutane na Nsyuka vizuri ama Shumileta kabsa.
Hii ni OCD mkuu, Kila mtu ana changamoto yake ya Afya ya akili ni vile hajakutana na triggering factor, mfano wa triggering factor ni genetic kama kwenye familia Kuna mtu ana shida ya Afya ya akili tunakua more likely na Sisi kulipuka, kingine ni environmental factors mfano madawa ya kulevya, pombe e t c

Mimi la kwangu ni phobia (uoga) wa kusimama kwenye majengo marefu, ukitaka nife Kwa pressure nipeleke jengo hata la ghorofa 5 tu nitateseka sana siwezi kuangalia chini

So mkuu usijali hiyo Hali Yako Kila mmoja ana yake kikubwa jiepushe na vitu vitakavyokufanya uka run mental health problems

Kuhusu ufanyeje Hali iondoke jibu ni sio rahisi kuiondoa, jitahidi kuishi nayo kikubwa usikere wengine basi
 
Ni muhimu sana kuyafahamu magonjwa ya akili. Bila kuyajua wagonjwa wa akili wanaweza kuangamiza watu. Kama Kibwetere na mama aliyemlisha matango pori, au aliyeua watu Kenya hapa juzi kati au mtu anaanzisha dini mpya kabisa sababu ya kichaa chake. Mnaweza chagua kiongozi kwa kudhani ana maono kumbe ni kichaa.
 
Bandiko zuri tamu kusoma halichoshi
Mie naogopaga kusoma magazeti ila hili nimelisoma lote

Hivi mkuu mfano mimi nachukia kuona vitu visivyo pangwa vizuri mfano nikaingia ndani nikaona vitu vimezagaa zagaa hua najisikia hasira sipendi kuona mavitu ya merundikana hovyo bila mpangilio je huo nao ni ugonjwa?

Naweza kurudi kazin nikikuta hali kama hiyo siwezi kulala bila kuweka sawa
Niliwahi kwenda ugenini nikakuta watuwa hapo wameweka vituu vimezagaa sikuwezi kuhimili kukaa kwa amani nilikua sina raha mpka nikafanya usafi kwanza ndio nikapata amani
Yaan mazingira kama hayo hua najisikia vibaya kuliko mtu anavyoweza kudhani je hii nayo ni shida?
Wewe ni kama mimi tu, mimi sehemu ikiwa imevurugika siwezi kukaa mpaka niipange, hata kama ni ofisini nikiingia nitapanga kwanza ndio nikae kwa kutulia, hata kama nina viatu kukanyaga mchanga kwenye sakafu hakunipi raha kabisa itabidi nifagie kwanza, ndio nikae kwa amani.
 
Kuna mtu hapa tunaye ila tunaamini kalogwa maana hakuwa hivi ghafla tu akawa hasikii haoni vitu kwa mbali na haongei, anacheka mwenyewe kuna siku anaongea vitu havieleweki au aanze kulia, anasahau vitu kila kitu umkumbushe kama mtoto mwaka wa 9 huu😟
 
Bandiko zuri tamu kusoma halichoshi
Mie naogopaga kusoma magazeti ila hili nimelisoma lote

Hivi mkuu mfano mimi nachukia kuona vitu visivyo pangwa vizuri mfano nikaingia ndani nikaona vitu vimezagaa zagaa hua najisikia hasira sipendi kuona mavitu ya merundikana hovyo bila mpangilio je huo nao ni ugonjwa?

Naweza kurudi kazin nikikuta hali kama hiyo siwezi kulala bila kuweka sawa
Niliwahi kwenda ugenini nikakuta watuwa hapo wameweka vituu vimezagaa sikuwezi kuhimili kukaa kwa amani nilikua sina raha mpka nikafanya usafi kwanza ndio nikapata amani
Yaan mazingira kama hayo hua najisikia vibaya kuliko mtu anavyoweza kudhani je hii nayo ni shida?
Atelophobia hiyo mkuu! Pole sana! Nyie ndio watu mnataka mpaka nguzo za fence ziwe kwenye mstari mnyoofu kabsa
 
Ni muhimu sana kuyafahamu magonjwa ya akili. Bila kuyajua wagonjwa wa akili wanaweza kuangamiza watu. Kama Kibwetere na mama aliyemlisha matango pori, au aliyeua watu Kenya hapa juzi kati au mtu anaanzisha dini mpya kabisa sababu ya kichaa chake. Mnaweza chagua kiongozi kwa kudhani ana maono kumbe ni kichaa.
Until today they are roughly 300 recognized mental disorders. 😃
 
Bandiko zuri tamu kusoma halichoshi
Mie naogopaga kusoma magazeti ila hili nimelisoma lote

Hivi mkuu mfano mimi nachukia kuona vitu visivyo pangwa vizuri mfano nikaingia ndani nikaona vitu vimezagaa zagaa hua najisikia hasira sipendi kuona mavitu ya merundikana hovyo bila mpangilio je huo nao ni ugonjwa?

Naweza kurudi kazin nikikuta hali kama hiyo siwezi kulala bila kuweka sawa
Niliwahi kwenda ugenini nikakuta watuwa hapo wameweka vituu vimezagaa sikuwezi kuhimili kukaa kwa amani nilikua sina raha mpka nikafanya usafi kwanza ndio nikapata amani
Yaan mazingira kama hayo hua najisikia vibaya kuliko mtu anavyoweza kudhani je hii nayo ni shida?
Mkuu wewe huna ugonjwa wowote sema unapenda kukaa sehemu tulivu iliyopangwa vizuri.Waafrika sisi magonjwa yetu ni malaria kipindupindu etc hayo magonjwa ya mawazo ni ya wazungu waachie wenyewe.
 
Juzi Jumatatu nilipata taarifa kuwa kuna swahiba yangu alikuwa amelazwa pale hospitali ya Kanda ya Bugando ikanibidi niende kumjulia japo hali. Nilifika salama na tukazungumza mengi sana kuhusu maendeleo ya afya yake, tukacheka na kufurahi sana, namna bora ya kumpa uchangamfu mgonjwa maana alikuwa ana dozi yake ya sindano takribani 10 hivi.
View attachment 3569127
Sasa pembeni ya kitanda cha swahiba alikuwepo dogo kama miaka kati ya 18 mpaka 20 hivi, tokea nilipofika huyu dogo alikuwa anaongea kisha anasita na kuweka tusi huku akisindikizia na ishara ya kidole cha kati. Matusi hayakuwa mepesi kwani alikuwa anatoa matusi heavyweight.
View attachment 3569128
Ikanibidi niulize kuwa mbona ndugu wa kijana hawamuelekezi kuwa anakosea? Au kukemea tabia hiyo? Nikaambiwa kuwa kijana anaumwa ugonjwa wa Tourette syndrome, kimoyo moyo nikajisemea hizi mambo za Instagram pamoja na TikTok.
View attachment 3569129
Nikajisogeza karibu na dogo, nikamsalimia na kumpa pole ila nikapokelewa na tusi la mzazi wangu wa kike pamoja na kidole cha kati. DAAH nikajipa moyo kuwa labda kweli ugonjwa wake ni mkali sana kiasi hicho. Nikamjibu nashukuru sana, dogo akajaa tena kwenye mfumo ananipa tusi jingine kubwa zaidi. Ahh Kimoyomoyo nikasema huyu dogo ni wangu.
View attachment 3569130
Katika ulimwengu wa leo uliosheheni sayansi na teknolojia ya hali ya juu, kuna jambo moja la kushangaza: ongezeko la kile kinachoitwa matatizo ya kisaikolojia na kihisia. Zamani, mtu alipokuwa na hofu ya kitu, aliambiwa “jikaze!” kama unaogopa giza basi ndio utatumwa kufuata chumvi gizani ukutane na Nsyuka vizuri ama Shumileta kabsa.
View attachment 3569131
Huyu dogo alikuwa mpuuzi sana, kwa sababu moja niliamua kuanza naye LIGI ya kutusi huku nikipiga kwenye mshono. Nilimpiga tusi moja dogo akaguna na kukaa kimya kabsa, nikamuuliza, huu ugonjwa wako wa Tourette umeanza lini?
View attachment 3569132
Janja akaniambia kuwa yeye hana ugonjwa wala disorder yoyote zaidi disorder ya Tourette syndrome, ila ni vile ameishi na kukulia sana kwenye mazingira ambayo matusi ni Kiunganishi ila pia ni Kivumishi kikuu. Na alipofika Bugando, alikutana na Daktari mmoja raia wa Italia ndiye aliyemwambia kuwa anasumbuliwa na Tourette Syndrome.
View attachment 3569133
Katika dunia ya sasa je, kweli tunapiga hatua mbele au tunazidisha mambo yasiyo na msingi? Leo unaweza kukutana na mtu mwenye hofu ya kutazama maji, yaani maji?! mwingine anaogopa majani au matawi ya miti, na mwingine kabisa ana hofu ya nywele!
View attachment 3569134
Wataalamu watasema tunagundua na kuelewa zaidi afya ya akili kadiri siku zinavyosonga, jambo ambalo ni jema kabisa. Lakini kwa upande mwingine, jamii imeanza kuzoea tabia fulani hadi kushindwa kutofautisha kati ya ugonjwa halisi na mazoea ya mazingira.

Mfano hai ni yule kijana hospitalini anayedaiwa kuwa na Tourette, lakini ukikaa naye kwa dakika chache unagundua kuwa anachofanya ni matokeo ya mazingira aliyokulia—mahali ambapo matusi ni lugha ya kawaida kama “salamu”. Mwishoni dogo nilichapa tusi moja nikaona anatoa machozi nikamwambia hata mimi pia nina Tourette Syndrome..
View attachment 3569129
Swali linabaki: je, tunatibu matatizo halisi au tunatengeneza majina mapya kwa tabia za kawaida? Wakati mwingine inaonekana kama dunia imeamua kuvaa miwani ya “diagnosis” kila mahali. Ukikohoa mara mbili—labda una “something syndrome”! Ukiwa haupendi watu wa upinde basi unapewa jina Homophobia, Ukifanya kazi na ukachoka—inaweza kuwa “emotional burnout disorder”.
View attachment 3569128
Ni muhimu kutambua kwamba afya ya akili ni jambo nyeti na halipaswi kubezwa. Hata hivyo, tusipokuwa makini, tutafika mahali ambapo kila tabia ya kawaida itahitaji jina la kitaalamu. Na hapo ndipo dunia itakapogeuka kuwa ucheshi mkubwa—ambapo kuogopa jua kutakuwa kawaida kuliko kufurahia mwanga wake.
safi umeelezea vizuri sana KOngole MKUU
kiukweli kuna Phobia nyingi sana Duniani na wengi wanazo ila hawazijui..
ningependa sana ungeendelea kutuletea Mabandiko kama haya watu wajifunze..

japo kwa Tourette syndrome ni rare case sana sidhani kama Tanzania tunazo hizo case hata kwa 0.01

ila zaidi nikupongeze sana umechambua vizuri kila ukisoma unahamaika kusoma tena kinachofuata umeleta Elimu kwa njia ya Hadithi... Nakupa maua yako
 
Mi nahisi nina claustaphobia maana siwezi kukaa hata dakika moja kwenye mapango, napata shida sehemu finyo mfano chumba kiwe na dirisha moja tu halafu ni dogo, vichochoro virefu, kwenye dissorder nina social anxiety dissoder
Sijui ni nini hata kwenye daladala huwa nahisi kusuffocate! Chumbani kwangu sitaki kitu zaidi ya kitanda na kabati sipendi kubanana

Magonjwa ya kizungu😁
 
Mi nahisi nina claustaphobia maana siwezi kukaa hata dakika moja kwenye mapango, napata shida sehemu finyo mfano chumba kiwe na dirisha moja tu halafu ni dogo, vichochoro virefu, kwenye dissorder nina social anxiety dissoder
Ophidiophobia ni fear ya kuwa karibu na nyoka! Hivi kuna mtu ambaye hana Ophidiophobia yaani awe nyoka wa kijani, sijui nyoka gani ila siwezi kukaa karibu na nyoka 🐍
 
safi umeelezea vizuri sana KOngole MKUU
kiukweli kuna Phobia nyingi sana Duniani na wengi wanazo ila hawazijui..
ningependa sana ungeendelea kutuletea Mabandiko kama haya watu wajifunze..

japo kwa Tourette syndrome ni rare case sana sidhani kama Tanzania tunazo hizo case hata kwa 0.01

ila zaidi nikupongeze sana umechambua vizuri kila ukisoma unahamaika kusoma tena kinachofuata umeleta Elimu kwa njia ya Hadithi... Nakupa maua yako
Karibu sana Mkuu
 
Wewe ni kama mimi tu, mimi sehemu ikiwa imevurugika siwezi kukaa mpaka niipange, hata kama ni ofisini nikiingia nitapanga kwanza ndio nikae kwa kutulia, hata kama nina viatu kukanyaga mchanga kwenye sakafu hakunipi raha kabisa itabidi nifagie kwanza, ndio nikae kwa amani.
Mkuu nakuelewa sasa usiombe ukae na mtu asie jali mazingira utakonda kwa depression 😀😀
Wewe ni Twin
 
Back
Top Bottom