Lucha
JF-Expert Member
- Aug 24, 2018
- 9,719
- 34,510
Habari zenu?
Wiki kadhaa zilizopita niliamua kuchambua nguo zangu zote ambazo hazivaliki baadhi zilikuwepo nzuri na baadhi zikawepo zilizochakaa sana, nikaamua kugawa zile nzuri na zile chakavu ambazo hazifai nikaamua kubaki nazo, kwasababu zilikuwa zimechakaa na zimechanika sana isingependeza kumpa mtu ingeleta tafsiri mbaya.
Sasa leo nimeamka na kuamua kuchoma zile nguo zangu chakavu zote, sasa wakati nachoma kuna mtu kakuta naendelea na hilo zoezi na akashangaa anasema ni vibaya.
Nikamueleza kuwa zimechakaa sana na haifai kumpa mtu yeyote, akasema bado ni vibaya nimemuuliza kwanini lakini naona hajanipa jibu.
Je, ni kweli kuchoma nguo chakavu ni vibaya? Je, ubaya wake ni nini?
Wiki kadhaa zilizopita niliamua kuchambua nguo zangu zote ambazo hazivaliki baadhi zilikuwepo nzuri na baadhi zikawepo zilizochakaa sana, nikaamua kugawa zile nzuri na zile chakavu ambazo hazifai nikaamua kubaki nazo, kwasababu zilikuwa zimechakaa na zimechanika sana isingependeza kumpa mtu ingeleta tafsiri mbaya.
Sasa leo nimeamka na kuamua kuchoma zile nguo zangu chakavu zote, sasa wakati nachoma kuna mtu kakuta naendelea na hilo zoezi na akashangaa anasema ni vibaya.
Nikamueleza kuwa zimechakaa sana na haifai kumpa mtu yeyote, akasema bado ni vibaya nimemuuliza kwanini lakini naona hajanipa jibu.
Je, ni kweli kuchoma nguo chakavu ni vibaya? Je, ubaya wake ni nini?