Je, kuna ubaya kuchoma nguo zako zilizochakaa?

Lucha

JF-Expert Member
Aug 24, 2018
9,719
34,510
Habari zenu?

Wiki kadhaa zilizopita niliamua kuchambua nguo zangu zote ambazo hazivaliki baadhi zilikuwepo nzuri na baadhi zikawepo zilizochakaa sana, nikaamua kugawa zile nzuri na zile chakavu ambazo hazifai nikaamua kubaki nazo, kwasababu zilikuwa zimechakaa na zimechanika sana isingependeza kumpa mtu ingeleta tafsiri mbaya.

Sasa leo nimeamka na kuamua kuchoma zile nguo zangu chakavu zote, sasa wakati nachoma kuna mtu kakuta naendelea na hilo zoezi na akashangaa anasema ni vibaya.

Nikamueleza kuwa zimechakaa sana na haifai kumpa mtu yeyote, akasema bado ni vibaya nimemuuliza kwanini lakini naona hajanipa jibu.

Je, ni kweli kuchoma nguo chakavu ni vibaya? Je, ubaya wake ni nini?
 
Habari zenu?
Wiki kadhaa zilizopita niliamua kuchambua nguo zangu zote ambazo hazivaliki baadhi zilikuwepo nzuri na baadhi zikawepo zilizochakaa sana, nikaamua kugawa zile nzuri na zile chakavu ambazo hazifai nikaamua kubaki nazo, kwasababu zilikuwa zimechakaa na zimechanika sana isingependeza kumpa mtu ingeleta tafsiri mbaya.

Sasa leo nimeamka na kuamua kuchoma zile nguo zangu chakavu zote sasa wakati nachoma kuna mtu kakuta naendelea na hilo zoezi na akashangaa anasema ni vibaya nikamueleza kuwa zimechakaa sana na haifai kumpa mtu yeyote, akasema bado ni vibaya nimemuuliza kwanini lakini naona hajanipa jibu.

Je ni kweli kuchoma nguo chakavu ni vibaya? Je ubaya wake ni nini?
Kabla ya kuzichoma Kama upo DSM peleka sehemu wananunua Machupa unaweza kuwauzia wale jamaa then hela utakayopata utampa MTU ambaye unaona hawezi kupata hata mlo mmoja.


Fanya hivyo mkuu naimani utabarikiwa pia utakuwa umetunza mazingira .

Ila Kama umechoma tayari hiyo haina madhara yoyote .

Siku hizi vitu vingi vinafanyiwa recycle hivyo usitupe kitu hakikisha unauza then hela unafanya charity Kwa jamii yako
 
Kabla ya kuzichoma Kama upo DSM peleka sehemu wananunua Machupa unaweza kuwauzia wale jamaa then hela utakayopata utampa MTU ambaye unaona hawezi kupata hata mlo mmoja.


Fanya hivyo mkuu naimani utabarikiwa pia utakuwa umetunza mazingira .
Asante kwa ushauri mkuu sikufaham kama kuna sehem wananunua nguo chakavu, wakati mwingine nitafata ushauri wako.
Shukran.
 
Habari zenu?
Wiki kadhaa zilizopita niliamua kuchambua nguo zangu zote ambazo hazivaliki baadhi zilikuwepo nzuri na baadhi zikawepo zilizochakaa sana, nikaamua kugawa zile nzuri na zile chakavu ambazo hazifai nikaamua kubaki nazo, kwasababu zilikua zimechakaa na zimechanika sana isingependeza kumpa mtu ingeleta tafsiri mbaya.

Sasa leo nimeamka na kuamua kuchoma zile nguo zangu chakavu zote sasa wakati nachoma kuna mtu kakuta naendelea na hilo zoezi na akashangaa anasema ni vibaya nikamueleza kuwa zimechakaa sana na haifai kumpa mtu yeyote, akasema bado ni vibaya nimemuuliza kwanini lakini naona hajanipa jibu.
Je ni kweli kuchoma nguo chakavu ni vibaya? Je ubaya wake ni nini?
Mkuu ubaya nikwamba hiyo unayo sema imechakaa kupitiliza ujuwe bado kuna mtu anaona inamstahili avae.

Hata hivyo mungu atakuhukumu kwa uungwana wako wenye utu na ubinadamu shekh!
 
Mkuu ubaya nikwamba hiyo unayo sema imechakaa kupitiliza ujuwe bado kuna mtu anaona inamstahili avae.

Hata hivyo mungu atakuhukumu kwa uungwana wako wenye utu na ubinadamu shekh!
Kilichonifanya nisigawe zile zilizochakaa ni imani pia, kwa mujibu wa imani yangu tunatakiwa tutoe sadaka vile vilivyo vizuri , sasa hapo ndo palinibana nikajitathmini nikaona kwa uchakavu wa nguo zile ile haikua sadaka nzuri nikagawa zile nzuri

Japo ni kweli kuna watu bado wana uhitaji lakin hazikua kwenye hali nzuri
 
Pia Serikali iandae au itebgeneze Donation place .

Kuna wakati Watu wanapenda kutoa vitu Kwa jamii yao Kama viatu ,vitabu nguo TV nk Ila wanaishia kutupa n.k

Mfano mtoa mada angejua kuna donation kuna baadhi ya nguo ambazo zinaonesha uhai angeziweka katika Donation house ili wale masikini ambao hawana cha kuvaa zingewafikia .
 
Ungemkamata na kumuweka kizuizini mpaka akwambie kwanini alisema hivyo.

KaziKweliKweli/JobTrueTrue
 
Jifunze kugawa nguo kabla hazijachakaa sana! Ukiona nguo huwezi kuivaa labda imeanza kukubana au imekuwa fupi gawa kwa wahitaji.
Mitumba hii tunayovaa ni zile nguo ambazo wenzetu wa nchi zilizoendelea wanazituma kwa maskini huku Afrika! Na karibu nyingi zinakuwa hazijachakaa.
 
Nguo ikiwa imechakaa ni sawa tu kuchoma, huwezi kugawa kila nguo, kama boxer, chupi, vest, nk hizo ni za kuchoma tu
 
Kiwango cha uchakavu wa nguo hupimwa tofauti tofauti kutoka kwa mtu mwingine na mwingine,ukiona vibaya kuzigawa kwa kuwa machoni pako ni chakavu zaidi zitupe ili wenye uhitaji waziokote
 
Kilichonifanya nisigawe zile zilizochakaa ni imani pia, kwa mujibu wa imani yangu tunatakiwa tutoe sadaka vile vilivyo vizuri , sasa hapo ndo palinibana nikajitathmini nikaona kwa uchakavu wa nguo zile ile haikua sadaka nzuri nikagawa zile nzuri

Japo ni kweli kuna watu bado wana uhitaji lakin hazikua kwenye hali nzuri
Kuna nguo nyingine zinakuwa zimechakaa mpaka unashindwa utaanzaje kumpa mtu. Kuchoma hakuna madhara na wanaosema ni vibaya ni imani tu zilizowekwa ili kufanya watu wapeane badala ya kuchoma.
 
Kabla ya kuzichoma Kama upo DSM peleka sehemu wananunua Machupa unaweza kuwauzia wale jamaa then hela utakayopata utampa MTU ambaye unaona hawezi kupata hata mlo mmoja.


Fanya hivyo mkuu naimani utabarikiwa pia utakuwa umetunza mazingira .

Ila Kama umechoma tayari hiyo haina madhara yoyote .

Siku hizi vitu vingi vinafanyiwa recycle hivyo usitupe kitu hakikisha unauza then hela unafanya charity Kwa jamii yako
hawezi kupata mlo hata mmoja.. point
 
Jifunze kugawa nguo kabla hazijachakaa sana! Ukiona nguo huwezi kuivaa labda imeanza kukubana au imekuwa fupi gawa kwa wahitaji.
Mitumba hii tunayovaa ni zile nguo ambazo wenzetu wa nchi zilizoendelea wanazituma kwa maskini huku Afrika! Na karibu nyingi zinakuwa hazijachakaa.
Inategemea ''ntu na ntu''. Wengine siyo kuwa wanapenda kuzivaa mpaka zichakae sana bali ni uwezo.
 
Jifunze kugawa nguo kabla hazijachakaa sana! Ukiona nguo huwezi kuivaa labda imeanza kukubana au imekuwa fupi gawa kwa wahitaji.
Mitumba hii tunayovaa ni zile nguo ambazo wenzetu wa nchi zilizoendelea wanazituma kwa maskini huku Afrika! Na karibu nyingi zinakuwa hazijachakaa.
Sawa mkuu nashukuru kwa ushauri
 
Kuna nguo nyingine zinakuwa zimechakaa mpaka unashindwa utaanzaje kumpa mtu. Kuchoma hakuna madhara na wanaosema ni vibaya ni imani tu zilizowekwa ili kufanya watu wapeane badala ya kuchoma.
Kwakweli mkuu kwa jinsi zilivyo chakaa nikasema ningempa mtu yale yalikua ni matusi kwa mtu ambae anapokea hizo nguo sidhani kama zingemfariji huenda zingemvunja moyo kabisa
 
Kuchoma ni imani tu ya watu, kuwa ukifanya hivyo ni kosa maana hata mimi niliwahi fanya hivyo nikashangaa wananishangaa

So nikawa nazibadilisha kuwa matambara ya deki ila zilivyozidi uwingi nikawa natupa tu mahali bila kuchoma

Sasa vitu kama boxer na vest unagawaje?
 
Back
Top Bottom