Uchaguzi 2020 Je, kuna mgombea urais CCM aliwahi kupiga magoti akiomba kura tofauti na Magufuli?

Trust None

JF-Expert Member
Feb 12, 2018
1,260
4,415
Bila shaka kampeni za mwaka huu ni ngumu zaidi ya zile za 2015 na hata za 1995.

Jana tulishuhudia mgombea uraisi kupitia CCM akiwapigia magoti wananchi akiwaomba kura, Je, hii ni heshima kwao au maji ya shingo? Watu haohao anaowapigia magoti, ni haohao wanaoongozwa na Chama Tawala tangu uhuru. Kama hawakuleta maendeleo tangu nyakati hizo, je tatizo lipo UPINZANI au ndani ya CCM yenyewe?

Je, kuna mgombea urais wa CCM aliwahi kuwapigia magoti wananchi tofauti na huyu?

Screenshot_20200930-132117.png
IMG_20200930_133204.jpg
 
Hii inatooa changamoto kwa wale watakaokuja kuwa Marais was baadae kuwa wajikite kwenye maendeleo ya watu ili unaporudi kutafuta kuchaguliwa kwa Mara ya pili usipate shida Kama anayopata jamaa. Magufuli ameshindwa kuwashawishi wapiga kura maana kuwatajia kwamba umenunua madege, umwjenga mabarabara wakati watu wanalala njaa na Hali imekuwa ngumu kwa miaka mitano Ni Kama unawapigia kelele. Hivyo Hana Cha maana zaidi ya kupiga magoti na kuomba msamaha kwa wananchi kutokana na mateso aliyowapatia kwa miaka mitano.
 
usanii mtupu, anaona amekaliwa vibaya na 'Lissu' anaanza kuleta 'ngonjera' zake
 
Back
Top Bottom