Nilichosema "earlier" bado kipo kiangalie nimesema nini. Sisemi maneno kwa kukurupuka kama mtu anayedai mbowa amebaka vitoto na ana kesi mahakamani halafu anashindwa kutaja hata mahakama yenyewe! Kila neno ninalotumia nalipima na kulipanga sisemi kwa kubahatisha.
Kama unakandia JF na kuiona kuwa ni ya Chadema, kwanini unashinda hapa? Hakuna mtu anafungwa kamba na kuburutwa! Hapa ni mahali huru na chadema haihusiki hata chembe; lakini hilo hamlitaki na badala yake mnapaona pabaya patamu!, kutema hamtaki kutema, kumeza hammezi, mmebakia kumumunya!