Je, ilikuwa ni karamu ya risasi?

Je, ilikuwa ni karamu ya risasi?

Dhulma haijawai kudumu.
Babaake ALITEKWA mapema mwaka huu na jeshi la Polisi, mamaake amekutwa amefariki BAFUNI kwa kupigwa na risasi.

Huyu dogo na mdogo wake wa kike kwasasa ni Yatima. Watasomaje, watakula nini basi ni wao watajua bila kujali umri wao.

Hii ndio hali halisi ya familia nyingi kwasasa Tanzania. Haya ndio maumivu ambayo vijana wa taifa la kesho wanabeba vifuani mwao.

Poleni sana wa dogo zangu Mungu awe nanyie Katika kipindi hicho kigumu
1762667649096.jpg
 
Wale wapigaji sijui walipewa nini huko.. Maana walichojua ni kulenga na kufyatua.. Na shabaha zao zilikuwa zimenyooka mno.. Majeruhi kidogo vifo vingi😭
KMKM ndio nani?
 
Maeneo ya Kigogo...
Kuna nyumba Ina matundu 7 ya risasi....
Bahati nzuri hakuna madhara...
Jirani ndio Kuna madhara ya mtu kuvunjika bega...yupo Muhimbili...
Na ndugu wanahangaika atoke (maana walitonywa na wasamasia wema kwamba wakipata nafuu ni magereza Moja kwa Moja )maana majeruhi wengi wanaweza kufunguliwa kesi ya Uhaini ila walikuwa ndani ya nyumba

Nchii imeshageuka ya kigaidi, mtu amepigwa risasi akiwa nyumbani amejeruhiwa halafu ashitakiwe uhaini, nchi hii nini kimeikumba?? Sababu ya urafi wa madaraka?? Nchi yetu inateketea na inateketezwa na kikundi cha watu wachache wanaojali matumbo yao
 
Nchii imeshageuka ya kigaidi, mtu amepigwa risasi akiwa nyumbani amejeruhiwa halafu ashitakiwe uhaini, nchi hii nini kimeikumba?? Sababu ya urafi wa madaraka?? Nchi yetu inateketea na inateketezwa na kikundi cha watu wachache wanaojali matumbo yao.
 
Nchii imeshageuka ya kigaidi, mtu amepigwa risasi akiwa nyumbani amejeruhiwa halafu ashitakiwe uhaini, nchi hii nini kimeikumba?? Sababu ya urafi wa madaraka?? Nchi yetu inateketea na inateketezwa na kikundi cha watu wachache wanaojali matumbo yao ?
...
Hapo mwisho ungeweka alama ya kuuliza ?
 
HAKIKA MUNGU WETU HATANYAMAZIA HAYA

Askari wenu wanapiga risasi kuwatupa kwenye dimbwi la matope wengine wakiwa mauti lakini wengine wakiwa mahututi. Kisha mnasambaza askari mitaani kukagua simu za watu ili kufuta kila picha inayohusiana na maandamano.

Kama hiyo haitoshi, mnaitumia TCRA na Jeshi la Polisi kutisha watu ili kusudi wasizisambaze picha hizo mkisema ni wakifanya hivyo ni jinai! Mnataka watu waelewe kuwa ninyi mlidungua na kuwaua watu kisha kuwatupa kwenye hayo madimbwi ni wazalendo lakini wanaosambaza picha juu ya unyama wenu ndio wenye kutenda hiyo jinai!

Watu wanahangaika katika mahospitali kwa ajili ya kutafuta miili ya ndugu zao hamuwapi kumbe miingine askari wenu wameitupa huko kwenye madimbwi! Hivi nini kweli mnaabudu katika Mungu wa kweli au mnaabudu shetani?
Hakika kama haya hamtayajutia hadharani kwa kweli ninyi na vizazi vyenu mtapata shida sana na hamtapata wa kuwatetea kutokana na hivi vitendo vya kinyama mlivyowafanyia watoto wa nchi ya Tanzania.

Hamuwezi kustahili kalipio jepesi kutoka kwa askofu linalopungua hili. Jitafakarini haraka na mapema sana kabla kikombe cha ghadhabu cha Mungu hakijaa pomoni.
Je, nini kimekushangaza? Je, nini maoni yako?

Mwana Kondoo Ameshinda! Tumfuate!
Askofu Emmaus Bandekile Mwamakula
Itunge, Dar es Salaam; 9 Novemba 2025; Saa 10:20 jioni
 
Kwamba zilikuwepo silaha mpya na wapigaji waliopewa kuzijaribu kwenye miili ya watu? Je ulikuwa ufundi, umahiri ama mashindano ya kulenga shabaha?

Je ilikuwa ni kamari ya kubashiri nani ataketekeza roho nyingi kwa wakati mmoja? Ama je kulikuwa na silaha zinzokaribia kuisha muda wake wa matumizi hivyo inabidi zitumike haraka kabla ya muda wake kutimia ili zisilete hasara?

Maana roho nyingi zisizo na hatia ziliteketea nje ya maandamano .. Ilikuwa kama mchezo wa kuwinda.. Watu waliviziwa mitaani na majumbani, vichochoroni na hata kwenye veranda za majumba
Ilikuwa ni killing spree..

Karamu ya risasi.. Na kwakweli hazikubagua maana hakuna kundi ambalo halina kilio mpaka sasa.. Zile risasi hazikumuacha yeyote salama..

Wale wapigaji sijui walipewa nini huko.. Maana walichojua ni kulenga na kufyatua.. Na shabaha zao zilikuwa zimenyooka mno.. Majeruhi kidogo vifo vingi😭

Kuna damu bado hazijakauka
Vidonda vingi bado vinavuja damu vingine usaha.. Kuna majereha yameanza kutoa harufu..

Kuna miili imeanza kutoa uvundo mkali
Ardhi ya Tanganyika imenajisiwa.. Damu inanuka kila kona..!View attachment 3498956
Kinachonisikitisha zaidi ni wale wagonjwa waliotolewa hospitali wakaenda kuwachoma kwenye tanuru la Wazo Hill wakiwa hai. Huu ukati hata Idd Amin Dada au Bokasa hawajawahi kuufanya lakini Idd Amin Mama amefanya. Nchi imelaaniwa hii.
 
Aisee...🙆‍♂️
Hadi Askari wa Usalama Barabarani waliamua kushika SMG kuua Watanzania wenzao?
It was soo bad!! The HATE is so MUCH

Hivi kwanini Polisi wa Tanzania hitumia Bunduki za kivita na si silaha ndogo za kudhibiti wahalifu kama Ulaya na Marekani? Tuliiga wapi mfumo huu?

Unawezaje kumdhibiti mtu kwa SMG au LMG bunduki inapiga risasi inaenda mita 800 sasa ukifyatua si unaweza kuua na wengine wengi zaidi wasio eneo hilo na wasio na hatia ya huyo mhalifu uliyetaka kumdhibiti?

Hili la kuwa reviewed..haiwezekani Polisi kuwa VITANI na Raia wao huku nembo yao imeandikwa USALAMA WA RAIA NA MALI ZAO
 
Back
Top Bottom