Wakuu habari ,
Kuna msichana nimeanzisha naye uhusiano kama yapata miezi minne imepita.Nimejaribu kumsoma lakini bado simuelewi. Mara ya kwanza aliniambia anakaa kwa wazazi tukaendelea na life mara zote tulikua tunakutana viwanja tu. Baada ya mwezi akaniambia amepata kazi hotelini mkoa mfulani nilifurahi nikamruhusu aende na nikampa na nauli ya kuendea huko.
Siku moja kulikua na mechi kubwa ya yanga na kwakuwa yeye nimshabiki wa Yanga jioni yake baada ya mechi yanga ilishinda ikibidi nimpigie simu kumpongeza, nilimtania nimekuona uwanjani alishituka sana na akaniambia yupo dar kazi ameacha.Tukatafutana tulipo onanana nimuuliza upo kwa nani sasa jibu lake anakaa na dada na kazi ameacha.
Tangu siku hiyo mpaka leo huyu mtu si muelewi ni wa mizinga kila siku haipiti siku bila kuniomba hela, simuelewi.
Naombeni ushauri