Elections 2010 Je, Dr. Willibrod Slaa atatufaa?

Its a very interesting article with some facts. Lakini pia ni habari ambayo haina uzito wowote katika king'ang'anyoro cha Urais cha sasa.

Inanikumbusha Kampeni za Uchaguzi uliopita wa Wamarekani, kilikuwa na aina mbili za Uandishi: Unaomuunga Mkono Obama na Kumponda Mc Cain na ule Unaomuunga Mkono Mc Cain na Kumponda Obama. Hili ndilo linalotokea sasa kati ya JK na WS huku magazeti ya Uhuru; IPP Media; New Habari na yale ya Serikali yakiwa positive zaidi kwa JK wakati yale ya Tanzania Daima; Mwananchi; Mwanahalisi; (Raia Mwema?) yakiwa positive zaidi kwa Slaa nk.

Afterall unaweza kuiangalia glass yenye maji hadi katika kati katika namna mbili: Half-Full au Half-Empty. All these are issues of Mind and Attitudes.

As a matter of Fact utendaji Serikalini huwa haundani sana na maisha binafsi, ndo maana Wamarekani pamoja na Ufirauni na Ufuska wa Bill Clinton bado walimchagua tena kuwa Rais kwa kuwa utendaji wake ulikuwa mzuri..

The future can be made by looking at the past. Katika uongozi, Dr. Slaa ameonyesha njia alipokuwa Mbunge katika kuyashughulikia masuala ya Nchi na amefanikiwa. Palipo na ukweli tuseme ukweli. Katika hili, natofautiana sana na Mwandishi. Pia ikumbukwe kuwa hakuna chama chochote ambacho hakina tofauti baina ya wanachama wake au hata viongozi.

Mwenye Macho haambiwi tazama na wala mwenye masikio haambiwi sikia.
 
Mkulima Mimi said:
Aliyeandika nukuu makala umeacha hii kitu mwishoni "mwandishi wa maoni haya amejitambulisha kama "Chovenge Kipunde" ambaye anasema ni msomaji wa muda mrefu wa raia mwema. Tumeyachapisha maoni haya kwa sababu,pamoja na mambo mengine ndani ya toleo hili kuna mahojiano maalumu ya dk. Wilbroad slaa ambayo mengine yanagusia maoni ya msomaji wetu, kwa mawasiliano naye muandikie katika Kchovenye@yahoo.com


haya maelezo mtoa mada hakupaswa kuyaacha kwani yanatoa pia msimamo wa raia mwema juu ya makala hiyo. All in all majibu yapo kwenye mahojiano yake. Naomba kuwasilisha

Mkulima Mimi,

..tunachohoji hapa ni kwanini Jenerali Ulimwengu akaji-associate na makala za kihuni-huni na kidini-dini kama hizi?

..Raia Mwema siyo kama Jamii Forums ambako anaweza kutokea mkichaa aka-post upupu wakati moderators wako off duty.

..binafsi nilikuwa naliheshimu sana gazeti la Raia Mwema, but not after they published this article.

..labda Jenerali Ulimwengu,Johnson Mbwambo, na waandishi wengine tunao waheshimu wako likizo, na walioachiwa ofisi ndiyo wamefanya madudu haya.
 
Mkulima Mimi,

..tunachohoji hapa ni kwanini Jenerali Ulimwengu akaji-associate na makala za kihuni-huni na kidini-dini kama hizi?

..Raia Mwema siyo kama Jamii Forums ambako anaweza kutokea mkichaa aka-post upupu wakati moderators wako off duty.

..binafsi nilikuwa naliheshimu sana gazeti la Raia Mwema, but not after they published this article.

..labda Jenerali Ulimwengu,Johnson Mbwambo, na waandishi wengine tunao waheshimu wako likizo, na walioachiwa ofisi ndiyo wamefanya madudu haya.
jokaKuu,
Nadhani Mkulima mimi kishajibu,
Makala hii ni personal opinion ya mwandishi. Hicho ndicho kitu Mwanajamii alijaribu kuficha. Jenerali kama publisher na editor asingefanya haki kwa kumnyima huyu jamaa kutoa maoni yake. Kwa hiyo tuliza boli. Now that we know it is a personal opinion and not a news item.
 
Slaa ni mtoto wa nyerere hana jipya :huyu ni ccm , akipata madaraka tutarudi zile enzi za nyerere kukaa foleni ya sigara . Hivi karibuni aliutembelea mzimu wa nyerere kule dodoma . Huyu mtu ni hatari sana .

Nadhani wewe ni hatari kuliko yeyote nimewahi kumsikia! Kama Slaa ni mtoto wa Nyerere na Kikwete ni Mtoto wa nani? na Mkapa? hawa wageni wanalo jambo hapa jamvini, hamna uchambuzi ni hisia hisia tu, bure kabisa
 
Mimi sidhani kama habari kama hii inaleta impact yeyote kwa wapiga kura kwa sababu iko very personal haigusi moja kwa moja maisha ya watu kama vile masuala ya rushwa ufisadi uvunjifi wa katiba wizi wa mali ya umma nk.

Hizi ni propaganda za CCM baada ya kuona uwezekano wa kum corner Slaa kwa issue zenye impact kwa watu ni mdogo. Kwa hiyo wanatumia any available weapon ili waweze kumchafua ukiwemo udini, kumjengea chuki, kujenga makundi ndani ya Chadema, ukabila nk.

Swala la upadri wa Slaa ni jambo dogo sana kwa sababu hata wanaojaribu kulitumia wanajua hata kama watafanikiwa halitawasaidia kwa kiasi wanachofikilia. Naweza kusema kadri wanavyoeneza ukatoliki wake ndivyo wanavyomleta karibu na jamii ya wakatoliki na wakristo ambao si haba kwa Tanzania.

Mwisho naweza kusema sidhani kama makala hii inaweza kuchapishwa kwenye gazeti la Jenerali Ulimwengu bila yeye kujua, anaelewa nini kinaendelea na ameruhusu kwa maslahi yake zaidi. Pamoja na Jenerali kuhusika au kutohusika na makala hii waelewe kuwa kiongozi wa inchi hachaguliwi kwa misingi ya dini.

Kwa historia ya Tanzania hakuna dini yeyote inayoweza kumweka rais madarakani bila kushirikiana na dini nyingine, na vilevile tusisahau kuwa kwa nchi kama yetu ni vigumu sana kupata kiongozi asiye na dini lazima tu atatokea ndani ya dini fulani. Labda cha kujiuliza kwanini mambo ya dini ya mgombea yanajitokeza leo, hatukuyaona wakati wa Mkapa na Kikwete kwenye term ya kwanza.
 
Hakuna atakae mpa kura Padre Slaa, huyu bado ni mtandao wa kanisa katoliki ametumwa, anajaribu kuwafumba macho wananchi kwa kutumia jf, ameshindwa kumkinaisha mkewe ahame ccm, mkewe hadi leo ni ccm damu.

Kumkabidhi padre nchi ni ku-commit suicide, ametumwa na mtandao aweze kusign memorumdum nyingine, watz hawatodanganyika kamwe!!
 
Hakuna atakae mpa kura Padre Slaa, huyu bado ni mtandao wa kanisa katoliki ametumwa, anajaribu kuwafumba macho wananchi kwa kutumia jf, ameshindwa kumkinaisha mkewe ahame ccm, mkewe hadi leo ni ccm damu.

Kumkabidhi padre nchi ni ku-commit suicide, ametumwa na mtandao aweze kusign memorumdum nyingine, watz hawatodanganyika kamwe!!
Acha niwe nimedanganyika kwa kumpa Slaa kura yangu, hata mje kwa gear gani 2010 HATUDANGANYIKI
 
Dada zako walisema hivyo hivyo. Ila siku hizi WANA WATOTO.
Hakuna atakae mpa kura Padre Slaa, huyu bado ni mtandao wa kanisa katoliki ametumwa, anajaribu kuwafumba macho wananchi kwa kutumia jf, ameshindwa kumkinaisha mkewe ahame ccm, mkewe hadi leo ni ccm damu.

Kumkabidhi padre nchi ni ku-commit suicide, ametumwa na mtandao aweze kusign memorumdum nyingine, watz hawatodanganyika kamwe!!
 
Wengi wamekuwa wanajiuliza kuwa Dk. Wilbroad Slaa ni nani? Na anataka au anaweza kuifanyia nini Tanzania. Wanajiuliza kama ni nani na ni nini kinachomsukuma Dk. SLAA kutaka apewe mamlaka ya kuiongoza Tanzania.

Dk. SLAA ni Mtanzania, muumini na Daktari wa Falsafa katika masuala ya dini yake ya Ukristo dhehebu la Katoliki. Alikuwa Kasisi au bado ni Kasisi kwa maana ya Sakramenti isiyofutika, lakini aliasi wakati akiwa Katibu wa Baraza la Maaskofu, nafasi kubwa sana katika kanisa hilo lenye waumini wengi.

Haifahamiki kama alikorofisha nini, ingawa kuna madai kwamba alifanya ufisadi kwenye fedha za kanisa. Inafahamika kwamba alipoondoka kwenye uongozi wa kanisa alioa kama ishara ya kusema sasa ukasisi basi, lakini kanisa lilikataa kubariki ndoa yake kwa maana ile ile kwamba sakramenti hizo hazitolewi mara mbili kwa mtu mmoja.

Asingeweza kupata Sakramenti ya Ndoa baada ya kupata Sakramenti ya Ukasisi. Hakujali akaendelea na shughuli zake na sasa anatarajia kuwa Kasisi wa kwanza kuwa Rais wa Tanzania kama kura zitatosha ifikapo Octoba 31, mwaka huu.

Katika kitabu anachokitumia Dk. SLAA kwa sala, ambacho ni Biblia, yapo maelezo katika Timotheo sura ya tatu mstari wa kwanza hadi wa tano (Tim.3:1-5) kwamba: “Ni neno la kuaminiwa mtu akitaka kazi ya uaskofu; atamani kazi njema. Basi imempasa askofu awe mtu asiyelaumika, mume wa mke mmoja, mwenye kiasi na busara, mtu wa utaratibu, mkaribishaji, ajuaye kufundisha, si mtu wa kuzoelea ulevi, si mpiga watu; bali awe mpole, si mtu wa kujadiliana wala asiwe mwenye kupenda fedha; mwenye kusimamia nyumba yake vema, ajuaye kutiisha watoto katika ustahivu, yaani mtu asiyejua kuisimimia nyumba yake mwenyewe, atalisimamiaje kanisa la Mungu”.

Mchanganuo wa aya hiyo hapo juu unatoa picha tofauti za namna ya kumwelewa Dk. SLAA kama mtu anayetafuta nafasi ya kuwa Rais wa Tanzania. Kwa upande mmoja, hata kama zipo sababu nyingine zilizomwondoa katika nafasi ya Ukatibu wa Baraza la Maaskofu, kuhusishwa kwake na ufisadi wa fedha za misaada kulimwondolea sifa ya kuwa kiongozi kanisa la Mungu, Analaumika.

Naamini hajajitoa kwenye Ukristo bado ni Mkatoliki na zipo taarifa ambazo zimeshaandikwa kwenye baadhi ya vyombo vya habari kwamba kanisa linamuunga mkono katika harakati zake za kutaka uongozi wa juu wa nchi.

Kanisa limeshakanusha kwamba halimuungi mkono kwa sababu Tanzania haina dini na viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) wamekuwa wakisisitiza kwamba Chama chao kisihusishwe na dini kwa maelezo kwamba uongozi wake ni wa watu wa dini zote na hata pengine wale wasio na dini.

Pamoja na ukweli kwamba viongozi waanzilishi wa CHADEMA ni wakristo, kanisa halingeweza kuonyesha kwamba linamuunga mkono, lakini ni vyema ikakubalika kwamba kwa miaka yote kanisa limekuwa likiamini kwamba dini ya mfalme wako ndio dini yako.

Hata kama Dk. SLAA aliukataa Ukasisi na akaonekana muovu mbele ya macho ya uongozi wa kanisa, lakini kwa sasa anaonekana ni mali kwa kuwa jiwe lililokataliwa na wajenzi wote, sasa limekuwa jiwe la msingi wa nyumba. Ukorofi wa Dk. SLAA kwa kanisa wa kuivuruga Sakramenti ya Ukasisi utavumiliwa na haitashangaza kama hata ndoa yake ikabarikiwa na kanisa endapo atafanikiwa kuupata Urais.

Ushahidi wa hali kama hiyo upo. PASTEUR BIZIMUNGU, hakuwa na ndoa na SERAFIN hadi alipoteuliwa kuwa Rais wa Rwanda wakati RPF inaingia madarakani mwaka 1994. Kanisa ndilo lililomtaka afunge ndoa kabla ya kuapishwa kuwa Rais. Kanisa linachotaka ni Dk. SLAA kuwa Rais wa Tanzania. Waraka wa kanisa uliotolewa na Baraza la Maaskofu tarehe 2 Julai, 2010, ulikuwa ni ishara tosha ya kuwajulisha Wakristo kwa ujumla kwamba wana mtu wao na bila shaka ni Dk. SLAA.

Kasisi/Padre anayejiondoa kwenye huduma zake za Kipadre huchukuliwa na kanisa kama mwana mpotevu (Prodigal Son) au kondoo aliyepotea, ambaye wakati wowote anaweza kurudi kundini. Kwa kuwa kazi mojawapo ya kanisa ni kuwatafuta na kuwarudisha kundini kondoo waliopotea, kanisa halijakata tamaa kuhusu uwezekano wa Dk. SLAA kurudia wito wake wa upadre.

Kwa kuzingatia dhamira yake kama mpakwa mafuta (the anointed) si jambo la ajabu ikiwa Dk. SLAA atarudi kwenye utume wake kama padre na kuiacha nchi “solemba”. Hata asiporudia upadre wake, upo uwezekano wa mchungaji huyo, akisukumwa na sauti ya wito wake wa upadre kuiongoza nchi kwa maslahi ya kanisa ambalo limemlea na kuchora moyoni mwake alama ya upadre isiyofutika (indelible mark) kama Kanisa Katoliki linavyoamini.

Wapo baadhi ya Watanzania watakaokumbuka kwamba mara baada ya uhuru wa Zimbabwe kupatikana mwaka 1980, Waziri Mkuu ROBERT MUGABE hakukubaliana na pendekezo la Rais CANAAN BANANA kwamba nchi hiyo iwe ya kikristo. Hakuna uhakika kama hilo haliwezi kutokea Tanzania ikiwa Dk. SLAA atafanikiwa kuwa Rais.

Taarifa ambazo ni vigumu kuzithibitisha na ambazo si vyema kuzipuuza zinaonyesha kwamba baadhi ya maaskofu wamekuwa wakikutana na uongozi wa Chadema kujadili hoja ya uongozi wa kitaifa na suala la uras mwaka 2015. Maoni ni kwamba hata kama urais hautapatikana mwaka 2010, angalau washinde na kuhakikisha kwamba Chadema kinakuwa chama kikuu cha upinzani bungeni ili kutoa nafasi ya kujiandaa kwa urais mwaka 2015.

Taarifa hizo zinaonyesha kwamba ili kufanikisha dhana ya CHADEMA kuwa chama kikuu cha upinzani Bungeni ni vyema MBOWE arudi jimboni kugombea na DK. SLAA agombee Urais hata kama hatafanikiwa, lakini atakuwa kivutio kikubwa cha kuwashawishi wananchi kuchagua Wabunge wengi wa chama hicho.

Mikakati ya kanisa imekuwa haimshirikishi ZITTO KABWE kwa sababu yeye anahofiwa kwamba ama yupo karibu na CCM au anatumia elimu yake kujijenga ili agombee Urais mwaka 2015.

Dk. SLAA alisita sana kuchukua fomu za chama chake kukubali kugombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, na yamkini watu walio wengi walikuwa wanamuuliza ni kwa nini anafanya hivyo, lakini wajuzi wa mambo walitambua kwamba Dk. SLAA alikuwa anasita kwa sababu nyingi ikiwa ni pamoja na kuamini kwamba alishafikishwa mahali pabaya ambapo pande zote mbili na kila upande ukiwa na dhamira yake ulikuwa unataka kumtumia. MBOWE alitaka kumtumia kukijenga Chama na Kanisa kujiimarisha.

Kwa upande mwingine, Dk. SLAA alipokuwa anajiunga na CHADEMA baada ya kuenguliwa CCM alifanya hivyo kwa kuamini kwamba angejijengea wasifu mpya, lakini hakujua kwamba anaingia kwenye Chama cha kifamilia kinachoendeshwa kwa gwanda la kikabila na kuongozwa na MBOWE ambaye naye anatajwa kuwa si msafi sana.

DK. SLAA amekuwa msitari wa mbele kupiga vita ufisadi hususan ndani ya serikali. Katika vita hivyo, Dk. SLAA amekuwa akisema kwamba serikali ya CCM haiwezi kupiga vita rushwa kwa sababau yenyewe imekuwa ikiendesha ufisadi tangu ilipoingia madarakani enzi za TANU. Kwa hoja hii, Dk. SLAA anaonyesha kwamba sio mkweli labda lengo lake ni kuichafua CCM ili ashinde katika uchaguzi huu.
Lakini hata kama hiyo ndiyo dhamira yake, atakuwa anafanya makosa makubwa akijaribu kupuuza juhudi za serikali ya awamu ya nne chini ya Rais KIKWETE katika kupambana na rushwa na ufisadi. Ni mapema mno Dk. SLAA kusahau juhudi za Muasisi wa Taifa hili Mwalimu JULIUS KAMBARAGE NYERERE na Waziri Mkuu MORINGE SOKOINE katika mapambano yao dhidi ya rushwa na wahujumu uchumi.

Kuna wasiwasi kwamba Dk. SLAA amegombea Urais kupitia kwenye chama ambacho hana madaraka na uwezo wa kukemea maovu ya ndani. Hana maelezo ya wazi kwamba ni kwa nini alikubaliana na ukaidi wa MBOWE alipon’gan’gania kwamba ni yeye pekee asimame kama mgombea wa Uenyekiti wa chama hicho na kumlazimisha ZITTO KABWE aondoe jina lake.

Matumizi ya ovyo ya fedha za CHADEMA ni ugonjwa ambao Dk. SLAA ameshindwa kuupatia dawa ingawa anafahamu kwamba ndio uliosababisha kuleta hali ya kutoelewana kati ya MBOWE na aliyekuwa mbunge wa Tarime CHACHA WANGWE ( sasa marehemu).

Ameshindwa kuyavunja makundi mawili ndani ya CHADEMA; kundi moja likiongozwa na Naibu Katibu Mkuu ZITTO KABWE na kundi lingine likiongozwa na Mwenyekiti FREEMAN MBOWE. Makundi yote haya mawili yanaelezewa kwamba kila moja linataka Urais mwaka 2015. Moja ya athari inayotokana na mivutano ya makundi haya ni kushindikana mara tatu kuteua Wabunge wa viti maalum. Hali hiyo ilitokea baada ya wagombea wanaomuunga mkono FREEMAN MBOWE kushindwa isipokuwa mmoja tu ambaye ni mtoto wa PHILEMON NDESAMBURO aliyekuwa Mbunge wa Moshi mjini.

Wote wanaoomunga mkono ZITTO walishinda na hali hiyo ilikuwa inaonekana kuwa tishio kwa Mwenyekiti Mbowe, ambaye alitamka kwamba mkutano huo ni batili. Haifahamiki kama wabunge wa viti maalumu wa CHADEMA watateuliwa lini, lakini swali la msingi na lisilo na jibu ni kwamba kwa nini DK. SLAA amekaa kimya kwenye kadhia hii. DK. SLAA anawashawishi Watanzania waanze kuamini kwamba hata wakimpa mdaraka ya kuiongoza dola ya Tanzania, atakuwa na tabia ya kuuzia masuala ya kitaifa kwa sababu hajiamini. Watanzania wanatakiwa kufikiri sana kabla ya kufanya maamuzi.

Source: Gazeti la Raia mwema Agosti 25 – Agosti 31, 2010

Ni kweli kabisa Slaa ana mkono wa kanisa nyuma yake ukitaka kujua hilo soma gazeti la Tanzania Daima la jana jumatano.Maaskofu wa mkoa wa Kilimanjaro wametoa waraka wa kumuunga mkono bwana Slaa.habari hiyo iko ukurasa wa tatu.
 
Nasikia 2Pac na Michael Jackson wanataka kumuunga mkono MZIRAY, Aisee!!!!

Padri una bahati kweli. Waja leo na waanza kutukana watu leo, mhhhhh!!!!!

Wee ndiyo vile Vibabu vya JF vinaingia upya JF kama mtoto wa Chekechea.

Ila ukiangalia ka uso, KAMEKOMAAA!! Hihiiiiiii

Ukitema mate yanaduna, hruuu hruuuu, unatoa unga....... Welcome Kibabu.

Ni kweli kabisa Slaa ana mkono wa kanisa nyuma yake ukitaka kujua hilo soma gazeti la Tanzania Daima la jana jumatano.Maaskofu wa mkoa wa Kilimanjaro wametoa waraka wa kumuunga mkono bwana Slaa.habari hiyo iko ukurasa wa tatu.
 
Ni kweli kabisa Slaa ana mkono wa kanisa nyuma yake ukitaka kujua hilo soma gazeti la Tanzania Daima la jana jumatano.Maaskofu wa mkoa wa Kilimanjaro wametoa waraka wa kumuunga mkono bwana Slaa.habari hiyo iko ukurasa wa tatu.
Mtajazana sana mwaka huu

Padri
user-offline.png

Junior Member
reputation_pos.png
reputation_pos.png
reputation_pos.png
reputation_pos.png
reputation_pos.png
reputation_highpos.png
reputation_highpos.png
reputation_highpos.png

Join Date Thu Aug 2010
Posts 1
Thanks : 1
Thanked 0 Times in 0 Posts
Rep Power
 
Hakuna atakae mpa kura Padre Slaa, huyu bado ni mtandao wa kanisa katoliki ametumwa, anajaribu kuwafumba macho wananchi kwa kutumia jf, ameshindwa kumkinaisha mkewe ahame ccm, mkewe hadi leo ni ccm damu.

Kumkabidhi padre nchi ni ku-commit suicide, ametumwa na mtandao aweze kusign memorumdum nyingine, watz hawatodanganyika kamwe!!

Tatizo lenu mafisadi wa dini mnajifanya kusahau (kuufumbia macho?) Uislamu wa Kikwete.Msilogwe kuwagawa wapiga kura kwa misingi ya dini kwani mtakaothirika ni nyie (takwimu kuhusu viwango vya elimu kati ya wakristo na wasio wakristo zinajieleza bayana).Katika kutapatapa kwenu mnaweza kujikaanga kwa mafuta yenu wenyewe.

Tumemvumilia Kikwete pamoja na udini wake lakini kwa vile mmeshalamba asali sasa mnataka kuchonga mzinga.Hamtaki kusikia Mkristo akiingia tena Ikulu.Mshindwe na mlegee.

Slaa ahukumiwe kwa uwezo wake wa kutetea maslahi ya Watanzania na sio imani yake ya kidini.Na mkileta hizo personal issues (family,etc),mgombea wenu ana skandali kadhaa ambazo naamini nanyi mnazifahamu.

All in all,hamtofanikiwa.
 
Hakuna atakae mpa kura Padre Slaa, huyu bado ni mtandao wa kanisa katoliki ametumwa, anajaribu kuwafumba macho wananchi kwa kutumia jf, ameshindwa kumkinaisha mkewe ahame ccm, mkewe hadi leo ni ccm damu.

Kumkabidhi padre nchi ni ku-commit suicide, ametumwa na mtandao aweze kusign memorumdum nyingine, watz hawatodanganyika kamwe!!

watu kwa makusudi yenu wenyewe au kwa kutumiwa mnapanda mbegu ya chuki dhidi ya wakatoliki, mnajua mnachafua dr. Slaa na chadema hamjui kuwa mnaandaa chuki dhidi ya wakatoliki kwamba wameamua kusimamisha mgombea. Nadhani hamjui ukubwa na uwezo wa kanisa hilo kama likiamua kufanya kweli kwa kumsimamisha mgombea, kwa jinsi mnavyolishutumu waziwazi nadhani msingesema slaa atashindwa maana nadhani kanisa katoliki ndilo linaongoza kuwa na watu wengi! Kwahiyo wingi wao ni ushindi tayari! Kwa kulishutumu kanisa katoliki sababu ya muumini wake dr slaa kuamua kugombea urais mnaanza kuzua maswali wakatoliki wanaanza kuhoji hivi mkatoliki hapaswi kugombea urais!?
Ila naanza kupata hisia kwamba inawezekana ccm miaka yote ilisapotiwa na kanisa katoliki mwaka huu inavyoonesha kanisa limegoma kwahiyo ccm inahisi moja kwa moja kanisa lipo nyuma ya mgombea wa chadema aliyewahi kuwa padre huo ndio wasiwasi wao mkubwa! Kwani wanaamini kanisa halijawahi kuwa neutral kabisa kwenye uchaguzi mda wote lilikuwa sambamba nao sasa kwanini leo kanisa halitaki kushirikiana nao tena!
Wadanganyika amkeni siasa sio kama ushabiki wa mpira wa simba na yanga hata mkifungwa mnatafuta sababu kuwa mlihujumiwa. Ushabiki huu wa chuki tena kwa makusudi unaweza usiishie hapa kwani kwa kusemasema jambo ambalo halipo mnawasaidia watu kuanza kuona uwezekano wa kufanya hilo huko mbeleni! Kama waliotuhumu hili wataliacha lipite na serikali ikafumbia macho basi mbeleni makanisa na misikiti vitasimamisha wagombea maana haramu imehalalishwa, mnawafunza wale ambao hawana mawazo kuanza kufikiria uwezekano wa kufanya hivyo! Kila mtu na imani yake lakini mambo ya ushabiki usio na maana hautatupeleka popote! Wanafiki endeleeni wanamapinduzi songeni mda utafika kila kitu kitakaa sawa......!!
 
Haiwezekni kigezo kikubwa kuwa ni dini tukiendeleza ubaguzi huu tutaangamia kama taifa watu hawaujui ukatoliki lakini ndo wanaeleza uongozi wa katoliki watu hawa wamefilisika sera badala ya kuongelea masuala kama ufisadi,umaskini,wizi tunajadili watu kama slaa na matukio kama alikuwa padre n.k let us be successful people and not average
 
Back
Top Bottom