Je, hivi ndivyo tunavyotaka nchi yetu ionekane?

Je, hivi ndivyo tunavyotaka nchi yetu ionekane?

Dr Adam Francis

JF-Expert Member
Joined
Aug 12, 2011
Posts
710
Reaction score
1,163
Katika utumishi wa umma huwa tunaelekezwa kuzingatia maslahi ya umma katika kutekeleza majukumu yetu.

Utashi huu ni muhimu kwasababu pamoja na kuchochea ufanisi, ubora wa huduma kwa wateja na mahusiano mema mahali pa kazi, husaidia kujenga taswila chanya ya taasisi zetu pamoja na serikali kwa ujumla.

Sina uhakika kama tathmini sahihi huwa inafanyika haswa katika kukabiliana na wananchi wenye mwelekeo wa kuipinga serikali. Wenye dhamana na masuala hayo wakati mwingine wanatuachia maswali kama wanazingatia maslahi ya umma katika utekelezaji wa majukumu yao.

Nadhani tuna kila sababu ya kwenda kujifunza, haswa kwa mzee wetu Rais Kikwete maadam yupo hai. Katika uongozi wake huyu mzee alisemwa sana, lakini hatukusikia makesi yenye ukakasi. Pamoja na mapungufu ya hapa na pale waliowengi wanakubali kuwa kwenye demokrasia alifanya vizuri.

Natamani ifike mahala tuachane na kesi ambazo zinaichafua demokrasia na uhuru wa watu kutoa mawazo katika nchi yetu.


 
Sababu ni Zile Zile Tu.
Kenge hadi Umpasue Masikio ndio akusikie.

1. Utekaji.
2. Mauaji ya kutisha na Mauaji ya Maelfu ya watu ( October 29.)
3. Kupotezwa kwa Watu..
4. Uhuru wa vyombo vya habari.
5. Uhuru wa kutoa maoni.
6. Kubambikia kesi za uongo akina Lissu, Mboye, Bony, Malisa CHADEMA NK
7. Uhuru wa kuabudu.
___________
8. Rushwa.
9. Ufisadi.
10. Ukiukwaji wa Haki za Binadamu.
 
Katika utumishi wa umma huwa tunaelekezwa kuzingatia maslahi ya umma katika kutekeleza majukumu yetu.

Utashi huu ni muhimu kwasababu pamoja na kuchochea ufanisi, ubora wa huduma kwa wateja na mahusiano mema mahali pa kazi, husaidia kujenga taswila chanya ya taasisi zetu pamoja na serikali kwa ujumla.

Sina uhakika kama tathmini sahihi huwa inafanyika haswa katika kukabiliana na wananchi wenye mwelekeo wa kuipinga serikali. Wenye dhamana na maswala hayo wakati mwingine wanatuachia maswali kama wanazingatia maslahi ya umma katika utekelezaji wa majukumu yao.

Nadhani tuna kila sababu ya kwenda kujifunza, haswa kwa mzee wetu Rais Kikwete maadam yupo hai. Katika uongozi wake huyu mzee alisemwa sana, lakini hatukusikia makesi yenye ukakasi. Pamoja na mapungufu ya hapa na pale waliowengi wanakubali kuwa kwenye demokrasia alifanya vizuri.

Natamani ifike mahala tuachane na kesi ambazo zinaichafua demokrasia na uhuru wa watu kutoa mawazo katika nchi yetu.
View attachment 3653676
Mbona unaremba maneno!!?
Unataka kuwa na uhuru wa kutoa maoni huki wewe mwenyewe unaogopa kuufanyia kazi huo ushauri wako!!

Jifunze kuita chepeo ni chepeo na si kijiko kikubwa.
Nakubalia na Prof. M. Assad alivyosema 60+% ya watumishi wa GoT hawana uwezo na hata hao 30+% wenye uwezo, wanaotimiza majukumu yao ni nusu tu.

Tatizo kubwa ni mfumo wa kutegemea utashi wa mtu mmoja, tena mwanasiasa ambaye hata hana weledi wowote, kuendesha nchi/wizara/idara/taasisi.
 
Katika utumishi wa umma huwa tunaelekezwa kuzingatia maslahi ya umma katika kutekeleza majukumu yetu.

Utashi huu ni muhimu kwasababu pamoja na kuchochea ufanisi, ubora wa huduma kwa wateja na mahusiano mema mahali pa kazi, husaidia kujenga taswila chanya ya taasisi zetu pamoja na serikali kwa ujumla.

Sina uhakika kama tathmini sahihi huwa inafanyika haswa katika kukabiliana na wananchi wenye mwelekeo wa kuipinga serikali. Wenye dhamana na maswala hayo wakati mwingine wanatuachia maswali kama wanazingatia maslahi ya umma katika utekelezaji wa majukumu yao.

Nadhani tuna kila sababu ya kwenda kujifunza, haswa kwa mzee wetu Rais Kikwete maadam yupo hai. Katika uongozi wake huyu mzee alisemwa sana, lakini hatukusikia makesi yenye ukakasi. Pamoja na mapungufu ya hapa na pale waliowengi wanakubali kuwa kwenye demokrasia alifanya vizuri.

Natamani ifike mahala tuachane na kesi ambazo zinaichafua demokrasia na uhuru wa watu kutoa mawazo katika nchi yetu.
View attachment 3653676
Leo ndiyo umejua hawa watu ni waouvu?
 
Akili zimeanza kukujia?
Ukiwasaliti wenzio Utaishia Pabaya.

Nadhani umemuona kazungu.
yule wa Tanga.
Kama umeamua kuwa jambazi baki huko huko, ukiwakana wenzio UTAUWAWA.
Inawezekana ww ni mgeni wa kusoma makala zangu. Fanya utafiti ni mara ngapi nimeandika kuhusu demokrasia, haki za binadamu na utawala wa sheria.

Changamoto yako unadhani kuwa CCM ni kukubaliana na kila kitu kinachofanywa na serikali na kuwa mpinzani ni kupinga kila kitu kinachofanywa na serikali.

Mm ninaamini katika uhuru wa kutoa maoni, na nitautumia uhuru huo kadri ya utashi wangu maadamu tu sivunji sheria au kuingilia uhuru wa wengine.
 
Sababu ni Zile Zile Tu.
Kenge hadi Umpasue Masikio ndio akusikie.

1. Utekaji.
2. Mauaji ya kutisha na Mauaji ya Maelfu ya watu ( October 29.)
3. Kupotezwa kwa Watu..
4. Uhuru wa vyombo vya habari.
5. Uhuru wa kutoa maoni.
6. Kubambikia kesi za uongo akina Lissu, Mboye, Bony, Malisa CHADEMA NK
7. Uhuru wa kuabudu.
___________
8. Rushwa.
9. Ufisadi.
10. Ukiukwaji wa Haki za Binadamu.
Kupinga mambo hayo uliyoyataja ni wajibu wa watanzania wote, haswa wana CCM maana wao chama chao ndicho kimeshika dola.

Mtu yeyote anayetetea mambo hayo uliyoyataja ni adui wa Taifa letu. Mambo hayo hayakubaliki ndio maana hata wanaoyafanya wanajificha mpaka wamebatizwa jina wasiojulikana.
 
Natamani ifike mahala tuachane na kesi ambazo zinaichafua demokrasia na uhuru wa watu kutoa mawazo katika nchi yetu.
Afadhali hao wanabambikwa kesi ,ndugu zao wanafahamu wapo, Kuna wengine wanapotezwa kabisa.

Mungu awarehemu wote waliopotezwa.
 
Back
Top Bottom